UKURASA WA 847; Wenye Uhitaji Zaidi Ndiyo Wasiotaka…

By | April 26, 2017

Kuna watu ambao wanahitaji sana msaada, lakini jaribu kutaka kuwasaidia, watakataa kabisa kwamba hawahitaji msaada wako. Hili ni jambo la kushangaza sana, lakini ndivyo ukweli ulivyo. Kadiri mtu anahitaji kitu sana, ndivyo inavyokuwa vigumu kwake kukikubali.

IMG-20170314-WA0016

Kwa mfano, mtu asiyejua, au anayefanya kitu kwa viwango vya hovyo sana, ukijaribu kumwelewesha na kumshauri njia bora zaidi ya kufanya, atakukatalia kabisa. Atakuwa mbishi sana na hatochukua ushauri wake, ataendelea kufanya yale anayofanya.

Mtu ambaye ni masikini kupindukia, unakuta ndiyo wa kwanza kukataa na kupinga pale anapopewa njia ya kuondoka kwenye umasikini aliopo. Atakuja na sababu kwa nini unachomwambia hakifai, au hakimfai yeye.

SOMA; Huhitaji Kila Mtu, Unahitaji Watu Sahihi…

Hili liko hivyo kwa sababu watu hao ndivyo walivyo, umewakuta pale walipo kwa sababu siku zote wamekuwa wanakataa kutoka hapo walipo. Kikubwa wanachokazana kufanya, ni kuhakikisha hawatoki pale ambapo wapo.

Ninachotaka kwako rafiki ni ujiangalie kwenye kila eneo la maisha yako, je yapo maeneo ambayo unahitaji msaada kweli lakini unaukataa? Vipo vitu ambavyo hujui, lakini wanaojua wanapojaribu kukujulisha unakuwa mbishi? Huwezi kujua hili kama hutakaa chini na kujihoji bila ya hisia. Fanya zoezi hilo ili ujue maeneo yapi yanakukwamisha na uweze kuyavuka na kusonga mbele.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Makirita Amani,

Kwa ushauri na Coaching bonyeza maandishi haya kupata utaratibu.

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)

Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea MTAALAMU NETWORK

Category: KURASA ZA MAISHA

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Leave a Reply

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.