2372; Tunategemeana Sana…

By | June 29, 2021

2372; Tunategemeana Sana… Pata picha hii, Kumetokea janga kubwa kabisa duniani na watu wote wamekufa isipokuwa wewe mwenyewe tu ndiye umebaki hai. Kwa kifupi wewe ndiye unayeimiliki dunia, iko wazi kwamba utakuwa ndiye tajiri namba moja na pekee kwenye hii dunia, maana unamiliki kila kitu. Sasa hebu pata picha unawezaje (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USIRIDHIKE…

By | June 29, 2021

Adui mkubwa wa mafanikio na maendeleo ni kuridhika na kile ambacho mtu ameshapata. Ugunduzi na hatua zote ambazo tumepiga kama wanadamu, ni kwa sababu watu hawakuridhika na kile walichokuwa nacho, japo kilikuwa bora. Iphone ya kwanza kutengenezwa yalikuwa mapinduzi makubwa mno, kila mtu alipenda namna teknolojia ilivyopiga hatua. Leo kuna (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KWA NINI MAFANIKIO SIYO RAHISI?

By | June 28, 2021

Kwa sababu yanahitaji umakini mkubwa ambao wengi hawapo tayari kuuweka. Kwa sababu yanahitaji mtu afuatilie kwa kina kila anachofanya kitu ambacho wengi hawakitaki. Kwa sababu yanahitaji juhudi kubwa ambazo wengi hawapo tayari kuziweka. Na kwa sababu hayataki mazoea, kitu ambacho wengi wanakipenda sana. Huwezi kufanikiwa kwa kufanya vile unavyojisikia kufanya (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia mauzo.

By | June 27, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia mauzo. Kama kuna watu wamefanikiwa kuleta mabadiliko makubwa duniani basi ni watu wa mauzo. Wagunduzi mbalimbali waliweza kugundua vitu vizuri, lakini ni watu wa mauzo ndiyo walioweza kuwashawishi watu wakubali kununua vitu hivyo. Kwa kuwa watu wana mahitaji mbalimbali, sehemu ya mauzo ni muhimu (more…)

2370; Nje Na Ndani…

By | June 27, 2021

2370; Nje Na Ndani… Kwa kila unachofanya, kuna namna mbili za kukiangalia. Kukiangalia kwa nje na kukiangalia kwa ndani. Unakiangalia kitu kwa ndani pale unapofuatilia kila kinachofanyika kwa undani kwenye kitu hicho. Hapo unajali mambo madogo madogo yanayokijenga kitu hicho. Unakiangalia kitu kwa nje pale unapoangalia picha kubwa unayotaka kufikia (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUFANYA MAAMUZI SAHIHI KWAKO…

By | June 27, 2021

Ili uweze kufanya maamuzi sahihi kwako, unapaswa kuondoa kila aina ya ushawishi wa watu wengine. Kuna kampeni za makusudi kabisa zinazoendeshwa na wengine ili kukushawishi wewe ufanye maamuzi ya aina fulani. Maamuzi hayo unayoshawishiwa kufanya yanakuwa na manufaa kwa watu wengine. Ili ufanikiwe, lazima uweze kufanya maamuzi yako mwenyewe. Kufanya (more…)

2369; Mambo Yanayoathiri Maamuzi Unayofanya…

By | June 26, 2021

2369; Mambo Yanayoathiri Maamuzi Unayofanya… Sehemu kubwa ya maamuzi unayofanya kwenye maisha yako, siyo maamuzi yako binafsi. Japo unaweza kujiambia umeyafanya mwenyewe, kuna vitu vingi vinavyoathiri maamuzi yako na kukushawishi ufanye maamuzi ya aina fulani. Maamuzi yoyote unayofanya ukiwa kwenye kundi kubwa la watu, ni tofauti kabisa na yale unayofanya (more…)