2360; Unakokimbilia Ni Wapi?

By | June 17, 2021

2360; Unakokimbilia Ni Wapi? Ni rahisi kujikuta ukiharakisha mambo unayoyafanya, lakini umewahi kujiuliza unakokimbilia ni wapi? Hebu fikiria mtu anayeharakisha kufanya kazi yake, anashindwa hata kuifanya kwa umakini, halafu anakokimbilia ni kwenda kubishana. Au fikiria mtu anayeharakisha kumhudumia mteja kwenye biashara, anaharakisha mteja aondoke, ili tu aingie kwenye mitandao na (more…)

Photo from Kocha Dr Makirita Amani

By | June 17, 2021

Hakuna kitu chenye gharama kubwa kwako kama usumbufu unaokuzunguka. Huwezi kuona gharama hiyo haraka kwa sababu akili yako inapata raha kirahisi. Ni baada ya muda mrefu ndiyo unakuja kugundua umekuwa unafanya kazi za kawaida na zisizo na ubunifu. Kutaka kwako kujua kila kinachoendelea kumepunguza umakini wako kwenye yale unayofanya na (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia ufundi wa

By | June 16, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia ufundi wa simu. Karibu kila mtu sasa anatumia simu ya mkononi. Kwa mazingira ya wengi, simu zao zimekuwa zinaharibika mara kwa mara na kuhitaji matengenezo. Hilo linatoa fursa mbalimbali za kuingiza kipato kupitia ufundi wa simu. Hapa kuna mawazo kumi ya kuingiza kipato kupitia (more…)

2359; Jipe Zawadi Ya Umakini…

By | June 16, 2021

2359; Jipe Zawadi Ya Umakini… Kama kuna zawadi bora kabisa unayoweza kujipa kwenye maisha yako, ni kuweka umakini wako wote kwenye kile unachofanya. Kadiri unavyoweka umakini wako kwenye kile unachofanya, ndivyo unavyoweza kukifanya kwa ubora wa hali ya juu sana. Na kama hiyo haitoshi, inakupunguzia kuhofia mambo yasiyo na umuhimu (more…)

#TAFAKARI YA LEO; JINSI UNAVYOYAHARIBU MAISHA YAKO…

By | June 16, 2021

Unachagua mwenyewe kuyaharibu maisha yako kwa namna unavyochagua kuyaishi. Kila unachofanya kwenye eneo lolote la maisha yako, kinaathiri kila eneo la maisha yako. Ukifanya kazi yako hovyo, maisha yako yanakuwa hovyo. Ukiwa na mahusiano yasiyo mazuri, maisha yako yanaathirika pia. Unapaswa kujiwekea viwango vya juu kabisa kwenye kila unachofanya na (more…)

2358; Fanya kwa ubora au usifanye kabisa…

By | June 15, 2021

2358; Fanya kwa ubora au usifanye kabisa… Una nafasi moja tu ya kuishi. Kila siku inayoisha ni siku unayoipunguza kwenye maisha yako, hutaweza kuipata tena. Kwa ukomo huo mkubwa ulionao, unapaswa kuwa makini sana na matumizi ya siku zako. Chochote unachochagua kufanya, kifanye kwa ubora wa hali ya juu kabisa. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WANAKUKWEPA KIRAHISI…

By | June 15, 2021

Watu huwa siyo wepesi kusema hapana, wanajua wakikuambia hapana watakuumiza. Hivyo wanatafuta kauli ya kukuambia hapana bila kukuumiza. Na kauli rahisi huwa wanakuambia watakutafuta wakiwa tayari. Ukikubaliana na kauli hiyo na kusubiri wakutafute, utasubiri sana na hawatakutafuta. Badala ya kukubaliana nao tu kirahisi, waombe wakuambie lini watakuwa tayari, wakupe tarehe (more…)

2357; Jiweke kwenye fikra zao…

By | June 14, 2021

2357; Jiweke kwenye fikra zao… Mtu akikuambia nitakutafuta, usisubiri mpaka akutafute, utakuwa umechagua kumpoteza. Hasa pale wewe ndiye unayekuwa unahitaji zaidi kitu kutoka kwake. Ipo kauli inayosema kisichoonekana huwa kinasahaulika. Kadhalika kwa wale wanaokuambia watakutafuta, ni rahisi kusahau kama hakuna kinachowafanya wakukumbuke. Na hapo ndipo unapaswa kujiweka kwenye fikra zako, (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia biashara ya

By | June 14, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia biashara ya nguo. Hakuna siku watu watatembea uchi duniani, hivyo mavazi yanabaki kuwa hitaji la msingi kabisa kwa wanadamu. Japo ni biashara yenye changamoto kubwa ya ushindani, maana wengi huona ndiyo biashara rahisi kwao kuingia na kufanya. Hapa kuna mawazo 10 ya kuingiza fedha (more…)