#TAFAKARI YA LEO; JINSI YA KWENDA NA WENYE IMANI NA ITIKADI KALI…

By | May 29, 2021

Kwenye maisha yako utakutana na watu wenye imani na itikadi kali juu ya kitu ambacho unajua kabisa siyo sahihi. Ushahidi uko wazi kabisa kwamba wanachoamini watu hao siyo sahihi, lakini bado wanakiamini na kukisimamia. Unaweza kuona ni wajibu wako kuhakikisha unawashawishi waachane na imani hizo, lakini utakuwa umefanya makosa sana (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia kilimo.

By | May 28, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia kilimo. Kilimo ni sekta yenye uhitaji mkubwa kwa sababu ndipo tunapopata chakula. Na kadiri idadi ya watu inavyoongezeka duniani huku watu wakiishi miaka mingi, mahitaji ya chakula yanaongezeka. Hapa ni mawazo kumi ya kuingiza kipato kupitia kilimo. Kuingia shambani na kulima moja kwa moja. (more…)

2340; Ukomavu Wa Kiroho…

By | May 28, 2021

2340; Ukomavu Wa Kiroho… Kama kuna kitu muhimu unachohitaji kwenye hii safari ya mafanikio basi ni ukomavu wa kiroho. Unapoianza safari hii ya mafanikio unakuwa mchanga kiroho, unakuwa na msukumo mkubwa wa kubadili maisha yako na kutaka kila anayekuzunguka abadilike mara moja. Utawalazimisha wabadilike na utawashangaa pale ambapo hawaelewi unachowashawishi. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAHALI PA KUPATA USHAURI MZURI…

By | May 28, 2021

Umekuwa unahangaika sana kutafuta ushauri kwa watu wasiojua chochote kuhusu wewe na unachofanya, wakati yupo anayekujua vizuri na kuweza kukushauri vyema kabisa.Sauti iliyo ndani yako ni mshauri mzuri kwako, sauti hiyo inakujua wewe tangu unazaliwa, inakumbuka kila ambacho umewahi kupitia na inajua nini kizuri kwako.Sauti hiyo imekuwa inajaribu kuwasiliana na (more…)

2339; Mlango Wa Sita Wa Hisia…

By | May 27, 2021

2339; Mlango Wa Sita Wa Hisia… Tumeizoea milango mitano ya fahamu. Macho yanayoona. Masikio yanayosikia. Pua inayonusa. Ulimi unaoonja. Ngozi inayohisi. Milango hiyo mitano ndiyo tunayotumia kuwasiliana na dunia ya nje. Upo mlango wa sita wa fahamu ambao wengi hawaujui. Mlango huo siyo wa kuwasiliana na dunia ya nje, bali (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNALISHA NINI AKILI YAKO….

By | May 27, 2021

Hebu fikiria umekaa mwezi mzima bila kula chakula kabisa, mwili wako utakuwa katika hali gani? Vipi ukikaa mwezi mzima bila kuoga kabisa? Hutafikisha hata mwezi, mwili utakuwa umeharibika kabisa. Sasa pata picha ni kwa kiasi gani unaharibu akili yako kwa kutokuilisha chakula sahihi. Matokeo ya mwili yanaonekana haraka kwa sababu (more…)

Mawazo 10 Ya Kuingiza Fedha Kama Mwalimu.

By | May 26, 2021

Mawazo 10 Ya Kuingiza Fedha Kama Mwalimu. Kupitia taaluma ya ualimu, kuna njia nyingi za kuingiza kipato. Hapa ni njia kumi ambazo mtu anaweza kutumia kuingiza kipato kwa taaluma hiyo. Kuajiriwa kama mwalimu. Kufundisha wanafunzi masomo ya ziada (tuition). Kujiajiri kama mwalimu kwa kufungua shule au chuo chako. Kuandika kitabu (more…)

2338; Maisha Kama Kombolela…

By | May 26, 2021

2338; Maisha Kama Kombolela… Kama unaukumbuka mchezo wa kombolela, una siri kubwa sana ya mafanikio kwenye maisha. Japo hatukuwa tunajua funzo lililo kwenye mchezo huo wakati tunacheza. Katika kucheza mchezo huo, kama wewr ndiye unayewatafuta wengine, kwanza lazima uwajue wote wanaoshiriki kwenye mchezo. Ukishawajua, lazima uwe na viashiria vya wapi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAISHA YA USHINDI….

By | May 26, 2021

Kupata ushindi kwenye maisha yako kazana kulata ushindi kwenye siku zako. Kazana kuiishi kila siku kwa ushindi kwa kuwa na vipaumbele sahihi na kuvifanyia kazi hivyo. Kila siku hakikisha kuna kitu unafanya ambacho ni cha ushindi na kumbukumbu yake itaendelea kuwepo. Huwezi kuwa na maisha ya ushindi kama unazipoteza siku (more…)