2334; Ushujaa Siyo Kupambana Pekee…

By | May 22, 2021

2334; Ushujaa Siyo Kupambana Pekee… Watu wengi hudhani ili wawe mashujaa lazima wapambane kwenye kila linalowakabili. Lakini ushujaa siyo kupambana pekee, wakati mwingine kuepuka mapambano ni njia sahihi na yenye manufaa kwako. Sun-Tzu aliyekuwa mwandishi wa kivita wa China ya kale na aliyeandika kitabu cha Art of War alishauri unaposhambuliwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; IPE AKILI MAZOEZI…

By | May 22, 2021

Moja ya nadharia ya mageuzi (evolution) ni kwamba kiungo cha mwili kinachotumiwa sana kinakuwa imara na kile kisichotumiwa kinakuwa dhoofu. Ndiyo maana kama unatumia sana mkono wa kulia, unakuwa na nguvu kuliko wa kushoto. Kadhalika ndivyo ilivyo kwenye akili, ukiitumia sana inakuwa imara, usipoitumia inakuwa dhoofu. Akili dhoofu haiwezi kufanya (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia simu yako.

By | May 21, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia simu yako. Kama unatumia simu janja (smartphone) na una mtandao wa intanetu, una fursa nyingi za kuingiza kipato. Hapa kuna mawazo kumi unayoweza kutumia kuingiza fedha kwa simu yako. Fursa ya kujifunza zaidi. Kujifunza na kubobea kwenye chochote unachofanya ni njia ya uhakika ya (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUKUTANA NA BAHATI…

By | May 21, 2021

Kila anayefikia mafanikio makubwa kwenye maisha, huwa kuna bahati anakutana nazo kwenye safari yake ya mafanikio. Lakini bahati hizi haziendi kwa aliyelala, bali zinaenda kwa aliye kwenye mapambano. Kwa kuwa hujui lini bahati itakufikia, wajibu wako mkubwa ni kuhakikisha uko hai na uko kwenye mapambano ili bahati inapokuja ikukute. Ukikata (more…)

2332; Kupata Unachotaka…

By | May 20, 2021

2332; Kupata Unachotaka… Kutaka ni rahisi, kila mtu anataka kitu fulani kwenye maisha. Kila mtu anataka fedha zaidi, anataka maisha mazuri zaidi na anataka kufanikiwa zaidi. Lakini wachache ndiyo wanapata kile wanachotaka, huku wengi wakiwa hawana budi bali kukubali maisha ya kawaida ambayo ni ya chini kabisa. Kuna hatua muhimu (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NI VIWANGO ULIVYOJIWEKEA…

By | May 20, 2021

Kile ambacho wengine wanakupa kwenye maisha yako, ni kulingana na viwango ulivyojiwekea wewe mwenyewe. Ukijiwekea viwango vya juu na kuvisimamia, watakupa kadiri ya viwango hivyo. Hakuna anayekudharau au kukutukana kama huvumilii vitu hivyo. Kupata kile unachotaka, jiwekee viwango vyako kisha kataa kabisa kupokea au kuvumilia chochote chini ya viwango hivyo. (more…)

2331; Hupati Unachostahili, Bali Unachovumilia…

By | May 19, 2021

2331; Hupati Unachostahili, Bali Unachovumilia… Huo ndiyo ukweli wa maisha, wanachokupa wengine siyo kile unachkstahili, bali ambacho unakipokea, kukikubali na kukivumilia. Kujiamini kwako ndiyo kunakuwekea viwango vyako. Kama hujiamini na uko tayari kupokea viwango vya chini, hivyo ndiyo wengine watakupa. Kama unajiamini na unakubali viwango vya juu pekee ndivyo utapewa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUWA WEWE…

By | May 19, 2021

Huwezi kupata mafanikio makubwa kwa kuyaiga maisha ya wengine. Hata kama watu hao wamefanya vitu fulani au kuishi kwa namna fulani wakafanikiwa, haimaanishi na wewe utafanikiwa kwa kuiga jinsi walivyofanya. Badala yake unapaswa kujifunza kutoka kwao, kisha kuishi uhalisia wako ili uweze kufanikiwa sana. Kwa kuishi uhalisia wako, hakuna anayeweza (more…)

2330; Nguzo Tano Za Kujijenga Binafsi…

By | May 18, 2021

2330; Nguzo Tano Za Kujijenga Binafsi… Umekuwa unasikia sana ushauri wa kwamba kama unataka kufanikiwa kwenye maisha basi unapaswa kuwa wewe, unapaswa kuwa halisi kwako na siyo kuiga maisha ya wengine. Kwa wengi ushauri huo huwa unaishia kuwachanganya badala ya kuwasaidia. Hapa tunakwenda kujifunza nguzo tano za kujijenga binafsi. Kwa (more…)