#TAFAKARI YA LEO; KILA MAISHA YANA GHARAMA…

By | April 20, 2021

Ukiwa masikini unaweza kuona matajiri wana maisha rahisi kuliko wewe, kwa kuwa wanaweza kupata chochote wanachotaka. Ukiwa tajiri unaweza kuona masikini wana maisha rahisi kuliko yako, kwa sababu hawasumbuki na mambo mengi. Ukweli ni kwamba kila maisha yana gharama ambayo lazima ilipiwe, hakuna maisha ya bure. Hivyo usihangaike kutafuta maisha (more…)

2301; Kinachokukasirisha kikutofsutishe…

By | April 19, 2021

2301; Kinachokukasirisha kikutofsutishe… Sheria ya kwanza na muhimi sana kwenye biashara ni kuwa na kitu kinachokutofautisha na wafanyabiashara wengine. Kuwa na kitu au vitu ambavyo wateja wanavipata kwako tu na hawawezi kuvipata sehemu nyingine yoyote. Yaani hata kama bidhaa au huduma yako itaondolewa jina na nembo, bado mteja aweze kuitambua (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USHAURI USIO SAHIHI…

By | April 19, 2021

Watu watajitolea kukupa ushauri mbalimbali ambao hata hujawaomba. Wataona wanajua jinsi unavyopaswa kuyaishi maisha yako kuliko wewe unavyojua. Chunga sana usishawishiwe na kila ushauri watu wanakupa. Kipaumbele cha kwanza kwenye maisha yako ni kupata kile unachotaka na hivyo ushauri unaohitaji ni wa kukusaidia kufika huko. Kama bado hujapata unachotaka, ushauri (more…)

2300; Kama hujafika unakotaka kufika…

By | April 18, 2021

2300; Kama hujafika unakotaka kufika… Huna wakati wa anasa na mambo yasiyokuwa na umuhimu. Kila dakika unapaswa kuiweka kwenye juhudi za kukufikisha unakotaka kufika. Unapaswa kutumia kila fursa iliyopo mbele yako katika kufikia malengo yako. Ushauri pekee unaohitaji katika kipindi hicho ni ule wa kukufikisha unakotaka kufika. Sahau kuhusu mlinganyo (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USHAWISHI WA WENGINE…

By | April 18, 2021

Kila unachosikia, kuona au kusoma, kuna ushawishi kinasababisha ndani yako. Hakuna kinachoingia kwenye akili yako bila kuacha madhara fulani. Hivyo unapaswa kuwa makini sana na watu unaowasikiliza, unaowaangalia na unaowasoma. Wale wenye ushawishi usio mzuri kwako, kaa nao mbali sana. Pia kuwa na msingi wako imara unaoufuata ambao mara zote (more…)

2299; Kupewa, kupata na kutengeneza…

By | April 17, 2021

2299; Kupewa, kupata na kutengeneza… Inapokuja kwenye fedha, maneno hayo matatu yana maana na tofauti kubwa. Kuna ambao wanaingiza fedha kupitia kupewa na wengine, mfano walioajiriwa. Watu hawa hawana nguvu kubwa ya kuamua wapewe kiasi gani, kwa kuwa wanategemea kupewa, yule anayetoa ndiye anayeamua kiasi gani awape. Hii siyo njia (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUTAKA KUBEMBELEZWA…

By | April 17, 2021

Kama unachotaka ni kubembelezwa, umeshapishana na mafanikio. Kama hutaki kabisa kuumia, huwezi kuyafikia mafanikio makubwa. Hatua ya kwanza ya kufanikiwa ni kusimama kwenye ukweli na ukweli huwa unaumiza. Uongo unaweza kukubembeleza, ila ni kwa muda tu, ukweli utakuumiza, lakini utakuweka huru. Mara zote simama kwenye ukweli, ndiyo njia pekee ya (more…)

2298; Kusikia unachotaka kusikia…

By | April 16, 2021

2298; Kusikia unachotaka kusikia… Mwandishi mmoja amewahi kusema, kusoma vitabu vingi vya maendeleo binafsi (personal development/self help) ni sawa na kufanya punyeto, unaweza kujisikia vizuri ila hakuna kinachobadilika kwenye maisha yako. Hilo lina ukweli kwa sehemu kubwa kwa sababu vitabu vingi vya maendeleo binafsi na hata wahamasishaji walio wengi huwa (more…)