https://www.kisimachamaarifa.co.tz/2017/11/06/kurasa_kumi-za-kitabu-leo-jinsi-ya-kufufua-na-kuchochea-udadisi-kitabu-how-to-think-like-leonardo-da-vinci-michael-j-gelbukurasa-57-66-watoto-wadogo-huwa-wanakuwa-na-maswali-mengi-sana-hu/
#KURASA_KUMI ZA KITABU LEO; Jinsi ya kufufua na kuchochea udadisi.KITABU; How to Think Like Leonardo da Vinci / Michael J. GelbUKURASA; 57 - 66.Watoto wadogo huwa wanakuwa na maswali mengi sana. Huwa wanahoji na kudadisi kila kitu. Lakini kadiri wanavyokua, ndivyo udadisi wao unavyopungua. Maswali yanaisha na wanakubaliana na majibu wanayoyapata au kile wengine amekubali.Hali hii wanakuwa wamejifunza, kutokana na majibu waliyopokea wakati wa udadisi na maswali mengi. Huenda ni kukatishwa tamaa au kukemewa na kuambiwa waache usumbufu.Kila mtu anaweza kufufua na kuchochea udadisi ambao upo ndani yake. Na njia ya kufanya hivyo ni kuanza kuhoji maswali. Kuanza kuhoji kila kitu na kuchunguza kwa kina.Badala ya kukubaliana na majibu rahisi yanayotolewa na kukubaliwa na wengine, unahitaji kuhoji zaidi.Zoezi hili kinakuwa bora zaid kama ukiwa na kijitabu cha kuandika maswai uliyonayo. Hapa unaandika yale maswali unayojiuliza au kudadisi chochote unachokutana nacho.Leonardo da Vinci anasifika kwa kuwa na vijitabu vingi ambavyo alikuwa akiandika maswali yake. Kila alichohoji na kudadisi alikiandika, na hili lilimwezesha kupiga hatua zaidi.Njia bora zaidi ya kuhakikisha unahoji maswali muhimu ya udadisi ni zoezi la maswali 100. Hapa unajihoji na kuandika maswali 100 muhimu zaid kwako. Maswali haya hayahitaji kuwa na umaalumu wowote, bali ni kuihoji akili yako mpaka itoe maswali 100.Zoezi hili litakuwezesha wewe kujijua kwa undani na kujua kile hasa unachoamini na hata kujali pia.Mara zote kuwana kijitabu, na mara zote hoji na dadisi, utajifunza mengi sana.Rafiki na Kocha wako,Dr. Makirita Amani,www.amkamtanzania.com/kurasa