Author Archives: Deogratius Kessy

About Deogratius Kessy

Deogratius Kessy ni mwandishi,Mhamasishaji, mwalimu na pia mjasiriamali.Anaandika kupitia mtandao wake wa www.mtaalamu.net/kessydeo lakini pia huwa anaandika katika mtandao wa amka mtanzania Mara moja kwa wiki unaoendeshwa na Makirita Amani.Aidha, mpaka sasa mwandishi Deogratius Kessy ameshatoa kitabu kimoja kiitwacho Funga ndoa na Utajiri. kitabu hiki kipo katika mfumo wa nakala tete ambacho baadae kitakuwa kinapatikana kwa mfumo wa kawaida yaani Hard copy.Deogratius Kessy, alihamasishwa kuandika na Makirita Amani tokea mwaka 2014 mpaka leo. Amechagua falsafa ya kuandika na kujifunza kila siku.vilevile, amejitoa kutumika na kusaidia watu wengine kupitia maandiko yake anayoandika kupitia vitabu na kwenye mitandao.mwandishi Deogratius, anavipaji kama vile kuandika, kuongea, kufundisha na uongozi. mwisho, Haya ni machache tu kati ya mengi anayofanya Deogratius Kessy. Asante sana.

Furaha Yako Inategemea Kitu Hiki

By | October 14, 2023

Sina uhakika kama itakufaa lakini kila mtu anapenda kuwa na furaha kwenye maisha yake. Vyote tunavyovifanya na malengo tunayoweka na pale tunapoyatimiza huwa tunajisikia furaha. Furaha yetu inategemea kitu kimoja na kitu hicho ni ubora wa mawazo yetu. Kama tukiwa na mawazo hasi basi itatupelekea kukosa furaha. Na kama tukiwa (more…)

Chanzo Cha Ukatili

By | October 13, 2023

Siyo mara yako ya kwanza kusikia ukatili na umeshaona watu wengi sana wakifanyiwa ukatili. Vitu vingi ambavyo unaona mtu anakufanyia kwenye maisha yako, jua anafanya hivyo kwa sababu na yeye alishawahi kufanyiwa hivyo. Anaona ni sehemu ya maisha yake kufanya hivyo. Kwa sababu tokea anakuwa anaona wengine wakifanyiwa ukatili na (more…)

Fadhila Yenye Nguvu Na Mafanikio Makubwa Kwenye Maisha Yako

By | October 6, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Sina uhakika kama itakufaa lakini wewe ni mtu mwenye bahati sana na ujasiri mkubwa mpaka hapa ulipofikia. Kwa sababu kuishi ni ujasiri mkubwa mno, mpaka hapa ulipo umeshavuka vikwazo vingi na umevipita. Pata picha changamoto mbalimbali ulizoweza kukabiliana nazo. Ni wangapi walioshindwa kufikia hapo wewe ulipo? Unaona (more…)

Utalivuka Daraja Pale Utakapolikuta

By | September 30, 2023

Habari njema mstoa mwenzangu, Huwa tunahofia sana vitu vya mbele yetu. Kabla hata hatujalifikia jambo, tayari tumeshajipa presha juu ya kitu hicho kitakuwaje. Kufikiria mambo yajayo kabla hata hatujalifikia huwa linatukosesha kuishi katika hali yetu ya uwepo wa hali ya sasa. Tunafikiria yajayo na tunaacha kuishi leo na matokeo yake (more…)

Ukimpenda Mtu Huyu Mmoja, Umewapenda Watu Wote

By | September 23, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Maandiko ya kiimani yanasema kwamba, huwezi kumpenda Mungu usiyemwona kama huwezi kumpenda jirani yako. Mafundisho mengi yanatufundisha sisi kuwapenda wengine. Ndiyo maana hata mtu akipata fedha, anaanza kuwalipa watu wengine kwanza na kujisahau yeye mwenyewe. Watu wengi hatujafundishwa kujipenda sisi wenyewe kwanza. Na matatizo mengi kwenye maisha (more…)

Hiki Ndiyo Chanzo Cha Matatizo Mengi Zama Hizi

By | September 16, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Tunaishi katika zama za kelele. Na ni ngumu katika zama hizi mtu kuonekana kuwa mpweke, kukaa bila kuwa na kitu cha kufanya. Zama hizi mtu anayekaa kimya bila kupiga kelele kwenye mitandao ya kijamii au kuchangia kwenye hoja mbalimbali anaonekana kama vile amepitwa na wakati. Kwa lugha (more…)

Kataa Hisia Za Maumivu Na Maumivu Yataondoka Yenyewe

By | September 9, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Mchezo mzima wa maisha yetu huwa unaanzia kwenye akili. Akili yetu inatupa kile ambacho kimetawala mara nyingi kwenye akili yetu. Ukiwa na hisia za kushindwa utapata matokeo ya kushindwa. Ukiwa na hisia za kupata zaidi utashangaa na akili yako inakuletea matokeo ya ushindi kwako. Ukiwa na hisia (more…)

Jinsi Ya Kumjibu Mtu Anayekuletea Umbea

By | September 2, 2023

Rafiki yangu katika Ustoa, Tunaishi kwenye jamii yenye maneno, karibu kila siku tunasikia maneno yakisemwa juu yetu sisi wenyewe na hata watu wengine. Kuna wakati tunayasikia maneno mabaya na kuna wakati tunasikia maneno mazuri yakisemwa. Hatuwezi kuwazuia wengine wasituseme kwani hakuna mtu ambaye hasemwi, kama maiti inasemwa sembuse wewe uliye (more…)

Wavumilie Wengine Lakini Siyo Wewe

By | August 26, 2023

Pale mtu anapoanza kujifunza falsafa ya Ustoa na kupata uelewa kidogo, kila mtu anayemuona haishi falsafa ya Ustoa anakuwa anaona kama kuna kitu anakosa. Anataka alazimishe hata watu ambao wanahusiana nao, waishi pia falsafa ya Ustoa kwa nguvu. Ni kama vile mtu ambaye anasoma kitabu kimoja kuhusu mafanikio, anatoka hapo (more…)