Author Archives: Deogratius Kessy

About Deogratius Kessy

Deogratius Kessy ni mwandishi,Mhamasishaji, mwalimu na pia mjasiriamali.Anaandika kupitia mtandao wake wa www.mtaalamu.net/kessydeo lakini pia huwa anaandika katika mtandao wa amka mtanzania Mara moja kwa wiki unaoendeshwa na Makirita Amani.Aidha, mpaka sasa mwandishi Deogratius Kessy ameshatoa kitabu kimoja kiitwacho Funga ndoa na Utajiri. kitabu hiki kipo katika mfumo wa nakala tete ambacho baadae kitakuwa kinapatikana kwa mfumo wa kawaida yaani Hard copy.Deogratius Kessy, alihamasishwa kuandika na Makirita Amani tokea mwaka 2014 mpaka leo. Amechagua falsafa ya kuandika na kujifunza kila siku.vilevile, amejitoa kutumika na kusaidia watu wengine kupitia maandiko yake anayoandika kupitia vitabu na kwenye mitandao.mwandishi Deogratius, anavipaji kama vile kuandika, kuongea, kufundisha na uongozi. mwisho, Haya ni machache tu kati ya mengi anayofanya Deogratius Kessy. Asante sana.

Utalivuka Daraja Pale Utakapolikuta

By | September 30, 2023

Habari njema mstoa mwenzangu, Huwa tunahofia sana vitu vya mbele yetu. Kabla hata hatujalifikia jambo, tayari tumeshajipa presha juu ya kitu hicho kitakuwaje. Kufikiria mambo yajayo kabla hata hatujalifikia huwa linatukosesha kuishi katika hali yetu ya uwepo wa hali ya sasa. Tunafikiria yajayo na tunaacha kuishi leo na matokeo yake (more…)

Ukimpenda Mtu Huyu Mmoja, Umewapenda Watu Wote

By | September 23, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Maandiko ya kiimani yanasema kwamba, huwezi kumpenda Mungu usiyemwona kama huwezi kumpenda jirani yako. Mafundisho mengi yanatufundisha sisi kuwapenda wengine. Ndiyo maana hata mtu akipata fedha, anaanza kuwalipa watu wengine kwanza na kujisahau yeye mwenyewe. Watu wengi hatujafundishwa kujipenda sisi wenyewe kwanza. Na matatizo mengi kwenye maisha (more…)

Hiki Ndiyo Chanzo Cha Matatizo Mengi Zama Hizi

By | September 16, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Tunaishi katika zama za kelele. Na ni ngumu katika zama hizi mtu kuonekana kuwa mpweke, kukaa bila kuwa na kitu cha kufanya. Zama hizi mtu anayekaa kimya bila kupiga kelele kwenye mitandao ya kijamii au kuchangia kwenye hoja mbalimbali anaonekana kama vile amepitwa na wakati. Kwa lugha (more…)

Kataa Hisia Za Maumivu Na Maumivu Yataondoka Yenyewe

By | September 9, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Mchezo mzima wa maisha yetu huwa unaanzia kwenye akili. Akili yetu inatupa kile ambacho kimetawala mara nyingi kwenye akili yetu. Ukiwa na hisia za kushindwa utapata matokeo ya kushindwa. Ukiwa na hisia za kupata zaidi utashangaa na akili yako inakuletea matokeo ya ushindi kwako. Ukiwa na hisia (more…)

Jinsi Ya Kumjibu Mtu Anayekuletea Umbea

By | September 2, 2023

Rafiki yangu katika Ustoa, Tunaishi kwenye jamii yenye maneno, karibu kila siku tunasikia maneno yakisemwa juu yetu sisi wenyewe na hata watu wengine. Kuna wakati tunayasikia maneno mabaya na kuna wakati tunasikia maneno mazuri yakisemwa. Hatuwezi kuwazuia wengine wasituseme kwani hakuna mtu ambaye hasemwi, kama maiti inasemwa sembuse wewe uliye (more…)

Wavumilie Wengine Lakini Siyo Wewe

By | August 26, 2023

Pale mtu anapoanza kujifunza falsafa ya Ustoa na kupata uelewa kidogo, kila mtu anayemuona haishi falsafa ya Ustoa anakuwa anaona kama kuna kitu anakosa. Anataka alazimishe hata watu ambao wanahusiana nao, waishi pia falsafa ya Ustoa kwa nguvu. Ni kama vile mtu ambaye anasoma kitabu kimoja kuhusu mafanikio, anatoka hapo (more…)

Jinsi Ya Kuepuka Kununua Matatizo

By | August 19, 2023

Mstoa mwenzangu, Kama tulivyojifunza jana kwenye makala ya kwanza ya ustoa, tunapaswa kuwa wanafalsafa kwa kuishi falsafa kwa matendo na siyo maneno.Falsafa ni kupenda hekima,na hekima ni kupenda kujifunza na kuchukua hatua. Huwezi kuwa na furaha kama huna hekima. Ukiwa huishi falsafa, utakua ni mtu wa kununua matatizo ya watu (more…)

Kwa Nini Dini Zote Zinapaswa Kuwa Na Uvumilivu

By | August 12, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Jana kwenye falsafa ya kwanza ya Ustoa tulijifunza umuhimu wa kuwa na afya ya akili, mwili na roho. Na tuliona kwamba , binadamu huwezi kukamilika kama hujakamilika kwenye maeneo hayo. Eneo la kiroho ndiyo eneo ambalo watu wengi bado hawajalipatia na linawafanya watu wengi kukosa shukrani na (more…)

Yajue Yaliyo Ndani Ya Uwezo Wako Na Yaliyo Nje Ya Uwezo Wako

By | July 29, 2023

Habari njema rafiki yangu mstoa mwenzangu, Mchezo mzima maisha yetu uko hapa. Kama tukiweza kuyajua yale ambayo yako ndani ya uwezo wetu na yale ambayo yako nje ya uwezo wetu tutaweza kuishi maisha yetu kwa uhuru zaidi.Mambo mengine yanatokea yanatupa hofu kwa nini yametokea bila kujua hata hatuwezi kuyadhibiti kutokea (more…)