#TAFAKARI YA LEO; MAARIFA YALIYO MUHIMU…

By | November 17, 2020

“The most important knowledge is that which guides the way you lead your life.” – Leo Tolstoy Tunaishi kwenye zama za mafuriko ya maarifa na taarifa. Vitabu vilivyoandikwa ni vingi mno, kiasi kwamba hakuna anayeweza kusoma hata asilimia 1 tu ya vitabu vyote. Makala, video na sauti zenye mafunzo mbalimbali (more…)

2147; Msongo Ni Pale Ambapo Huwezi Kujidanganya Tena…

By | November 16, 2020

Watu wengi wamekuwa wanapitia msongo wa mawazo kwenye maisha yao na wasijue nini chanzo. Wanajikuta wamezama kwenye msongo huo na kushindwa kuondokana nao kwa sababu hawajui chanzo. Kuna sababu kubwa mbili, ya kwanza ni kulazimisha mambo, kutaka mambo yawe tofauti na yalivyo au nje ya uwezo wako, sababu hii hatutaijadili (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KINACHOFANYIKA KWA UPENDO, KINAFANYIKA VYEMA…

By | November 16, 2020

“Whosoever loves much performs much, and can accomplish much, and what is done in love is well done!” – Van Gogh Yule mwenye upendo zaidi, anaweka juhudi zaidi na kuzalisha matokeo makubwa zaidi. Kile kinachofanyika kwa upendo, kinafanyika kwa ubora wa hali ya juu. Kwenye KISIMA CHA MAARIFA, imani yetu (more…)

2146; Unaweza Kwenda Kwa Muda Gani?

By | November 15, 2020

Watu huwa wanalalamikia hamasa wanazopata kutoka kwa wengine zimekuwa hazidumu. Mfano mtu anahudhuria semina au kusoma kitabu na kuhamasika sana, anatoka akiwa na mipango mikubwa ya kwenda kubadili kabisa maisha yake. Lakini siku chache baadaye hamasa ile inakuwa imeisha kabisa na kurudi kwenye mazoea. Wengi hufikiri tatizo liko kwenye hamasa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; SIYO KUFANYA ZAIDI…

By | November 15, 2020

“It’s not always that we need to do more but rather that we need to focus on less.” — Nathan W. Morris Tunaishi kwenye zama ambazo kila mtu anasukumwa kufanya zaidi. Lakini kadiri watu wanavyofanya mambo mengi zaidi, ndivyo wanavyochoka zaidi na kutokufanikiwa. Kwa asili, matokeo makubwa hayatokani na kufanya (more…)

2145; Njia Ya Uhakika Ya Kufika Na Kubaki Kwenye Utajiri…

By | November 14, 2020

Watu waliopo kwenye safari ya kuelekea kwenye utajiri ni wengi, lakini kati yao, wachache ndiyo wanaofika kwenye utajiri. Na katika kundi la wale wanaofika kwenye utajiri, ni wachache ambao hudumu na utajiri huo. Wengi huupata utajiri na baadaye kuwapotea, kuanguka kutoka kwenye utajiri. Wale wanaoshindwa kufika kwenye utajiri ni kwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NJITI YA KIBERITI HAIWAKI YENYEWE…

By | November 14, 2020

“Each of us is born with a box of matches inside us but we can’t strike them all by ourselves.” — Laura Esquivel Njiti ya kibeririti ina uwezo mkubwa wa kuanzisha moto, lakini haiwezi kuanzisha moto huo yenyewe. Ni lazima isubuliwe na kitu kingine ndiyo iweze kuanzisha moto. Chuma pia (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USIKILIZE MWILI WAKO, UNA MENGI YA KUKUAMBIA…

By | November 13, 2020

“A man is well equipped for all the real necessities of life if he trusts his senses, and so cultivates them that they remain worthy of being trusted.” – Johann Wolfgang von Goethe Miili yetu sisi binadamu huwa ina milango mingi ya fahamu. Acha ile mitano ambayo kila mtu anaijua (more…)