Category Archives: #TAFAKARI YA LEO

#TAFAKARI YA LEO; KUBADILI MAISHA YAKO, BADILI HADITHI YAKO…

By | August 31, 2021

Hadithi unayijiambia kila siku na kuiamini ndiyo inayojenga maisha yako. Kama unataka kuyabadili maisha yako, anza kwa kuibadili hadithi unayojiambia. Tengeneza hadithi mpya inayoendana na kile unachotaka, jiambie hadithi hiyo mara kwa mara na kuiamini. Jipime jinsi unavyoiishi hadithi yako na endelea kuboresha kadiri unavyokwenda. Kwa kusimama kwenye hadithi yako (more…)

#TAFAKARI YA LEO; ISHI MAISHA YAKO…

By | August 30, 2021

Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunajali sana wengine wanatuchukuliaje. Hilo lilikuwa muhimu kipindi cha nyuma, ambapo tuliishi ndani ya kundi lisilozidi watu 150 wanaojuana. Kama kikundi chako kidogo kingekukataa, huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yako. Lakini sasa tunaishi ndani ya kundi kubwa la watu na hakuna mwenye (more…)

#TAFAKARI YA LEO; RAHISI VS SAHIHI…

By | August 29, 2021

Fanya vitu rahisi na utakuwa na maisha magumu. Fanya vitu sahihi na utakuwa na maisha rahisi. Vitu rahisi kufanya siyo sahihi na vitu sahihi kufanya siyo rahisi. Kila unachofanya, jiulize kwanza unakifanya kwa sababu ni rahisi au sahihi? Utajikamata mara nyingi ukifanya vilivyo rahisi wakati vilivyo sahihi vipo mbele yako (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USIPOTEZE KINACHOKUNUFAISHA…

By | August 28, 2021

Sisi binadamu huwa tunazoea vitu haraka, kisha tunavichoka na kutaka kuvibadilisha. Tunapenda vitu vinavyotusisimua na kuibua hisia zetu. Ni katika harakati hizo ndiyo tunajikuta tumeharibu au kupoteza kile kilichokuwa na manufaa kwetu huko nyuma. Unapaswa kuwa makini sana kwenye hili, kwa kuhakikisha unalinda kila ambacho kina manufaa kwako ili usikiharibu (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNAVYOJIANDAA KUUMIA…

By | August 27, 2021

Kutaka mambo yaende kama unavyotaka wewe na kuona hayawezi kwenda tofauti na hivyo ni kujiandaa kuumia. Kwa sababu dunia haipeleki mambo yake kwa kuangalia matakwa ya watu, bali inatumia kanuni zake yenyewe. Unachoweza kudhibiti wewe ni juhudi unazoweka na mchakato unaofanyia kazi. Kwa upande wa matakeo, yatakuja yenyewe kwa namna (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KILA MTEJA NI WA KWANZA KWAKO…

By | August 26, 2021

Kila mteja unayemhudimia, mchukulie ndiye mteja wa kwanza kwako na wa kipekee kabisa. Kwa sababu hivyo ndivyo mteja anavyojichukulia. Wewe unaweza kuwa umeshawahudumia wateja wengi na umechoka, ila mteja mwingine anapokuja hajui wala kujali yote hayo. Ukimpa huduma mbovu hataangalia umehudumia wateja wangapi vizuri, yeye atakachojua ni kimoja, hujamhudumia vizuri (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UPANDE WA PILI WA MAFANIKIO…

By | August 25, 2021

Tunapoyatafuta mafanikio, huwa tunaangalia upande mmoja pekee, ambao ni upande mzuri wa kupata kile tunachotaka. Lakini mafanikio huwa yana upande wa pili, ambao ni kuwapoteza baadhi ya watu wako wa karibu. Kuna watu walikuwa na wewe kabla hujafanikiwa, lakini baada ya kufanikiwa wanageuka kuwa maadui. Unapaswa kujua hili, kwamba kadiri (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HASIRA NI MATATIZO BINAFSI…

By | August 24, 2021

Kinachokufanya ukasirike siyo kile alichofanya mtu au kilichotokea, bali ni matatizo yako binafsi. Unakasirika kwa sababu kuna namna unataka vitu viwe na havijawa, hivyo kupelekea kujiumiza zaidi. Kuondokana na hasira, anzia ndani yako mweyewe, acha kutaka vitu viwe kama unavyotaka wewe na vipokee kama vinavyokuja kwako. Pia usikubali tu kuchukua (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NI KUKOSA UMAKINI…

By | August 23, 2021

Kama umewahi kudanganywa, kuibiwa au kutapeliwa, ni kwa sababu kuna umakini ambao uliukosa. Watu huwa wanadanganya kwa maneno, lakini vitendo vyao huwa wazo kabisa. Ukiwa makini, lazima utaona tofauti kati ya unachosikia na unachoona. Mtu anakuambia kuna fursa yenye manufaa mahali, wakati ukimuangalii hafananii na mwenye kujua fursa ya aina (more…)

#TAFAKARI YA LEO; TATIZO LINAANZIA KWENYE KUTOKUJIAMINI…

By | August 22, 2021

Mstoa Marcus Aurelius amewahi kusema anashangazwa na tabia ya binadamu, huwa tunajipenda wenyewe zaidi ya tunavyowapenda wengine, lakini tunayathamini maoni ya wengine kuliko yetu wenyewe. Hili ni tatizo linaloanzia kwenye kutokujiamini. Unapokuwa hujiamini wewe mwenyewe, kile unachofanya na kule unakotaka kufika, unashindwa pia kuyaamini maoni yako mwenyewe. Unaona maoni ya (more…)