UKURASA WA 875; Neno Linalofuata Baada Ya Lakini, Linapinga Lililotangulia Lakini…

By | May 24, 2017

Mimi siyo mnafiki lakini…… maelezo yanayofuata hapo ni ya unafiki mtupu.

Au mimi siyo mbaguzi lakini…. sentensi itakayofuata hapo ni ya kibaguzi.

Nafikiri unapata picha, kama vile, sitaki kupinga lakini…… unajua kinachofuata hapo.

Matumizi yatu ya lugha na maneno yanatuwezesha watu kutusoma wazi, na kujua kile ambacho tunaficha kusema. Na hilo halitusaidii zaidi ya kuwafanya wengine watuone sisi siyo waaminifu.

Unaposema wewe siyo mnafiki, halafu ukatoa maelezo ya kinafiki, unamtengenezea mtu picha gani? Ya kwamba wewe ni mnafiki unayejificha.

SOMA; UKURASA WA 875; Neno Linalofuata Baada Ya Lakini, Linapinga Lililotangulia Lakini…

Nimekukumbusha hili leo rafiki yangu uache kutoa maelezo yanayoipinga yenyewe na kukupunguzia unafiki.

Sema kile unachojua ni sahihi, kile unachosimamia, bila ya kutaka kufichaficha. Watu wanapojua unasimama wapi, wanakuheshimu kwenye kile unachosimamia. Lakini unapokuwa upande huu, mara upande ule, watu wanashindwa kuelewa unasimama wapi, na kukuona wewe siyo halisi.

Sema kile kinachoeleweka, na namna unaowaambia wanavyoweza kuelewa, usijipinge wewe mwenyewe.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Makirita Amani,

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu

Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea www.mtaalamu.net/patablog

Category: KURASA ZA MAISHA

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Leave a Reply

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.