Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (109/366); Watoe maadui mafichoni.

By | February 17, 2022

#SheriaYaLeo (109/366); Watoe maadui mafichoni. Unaweza kuwa na maadui ambao wamejificha. Ambao kwa nje wanaonekana kama marafiki, lakini kwa ndani wana uadui mkubwa. Wanakuwa wanasubiri wapate fursa ili wakumalize. Na kwa kuwa hujui, basi inakuwa rahisi kwako kuwapa fursa ya kutimiza lengo lao. Katika safari ya mafanikio, adui usiyemjua ni (more…)

2604; Kiashiria kwamba umepotea.

By | February 16, 2022

2604; Kiashiria kwamba umepotea. Kwenye safari ya mafanikio, kiashiria kikubwa kwamba umeshapotea njia ni pale unapojikuta upo upande wa wengi. Iko hivi rafiki, kwenye kila jamii, huwa kuna upande wa wengi, ambao wanakubaliana kwenye mengi ila hawafanikiwi. Halafu kuna upande wa wachache ambao hawakubaliani na yale ya wengi na ndiyo (more…)

#SheriaYaLeo (108/366); Usijiingize kwenye migogoro ya wengine.

By | February 16, 2022

#SheriaYaLeo (108/366); Usijiingize kwenye migogoro ya wengine. Mara zote epuka sana kujiingiza kwenye migogoro ya watu wengine.Hilo halina manufaa kwako kwenye malengo yako ya kupata mafanikio makubwa. Watu watajaribu kukuvuta na kukushawishi uwe upande wao, lakini epuka sana ushawishi huo. Onyesha kuwaelewa na kujali, lakini epuka sana kujiingiza kwenye migogoro (more…)

2603; Mbona kila mtu anafanya?

By | February 15, 2022

2603; Mbona kila mtu anafanya? Uzuri wa ukweli ni kwamba huwa haujali watu wanauchukuliaje. Ukweli huwa hautumii nguvu kuwalazimisha watu wakubaliane nao. Bali huwa unabaki kuwa ukweli. Uongo huwa unatumia nguvu kubwa sana kuhakikisha kwamba unakubalika. Unakimbilia kuwateka wengi ukijua wengi ni sehemu nzuri ya kujificha na kukubalika zaidi. Ndiyo (more…)

#SheriaYaLeo (107/366); Usichukue upande wowote.

By | February 15, 2022

#SheriaYaLeo (107/366); Usichukue upande wowote. Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunapenda kuwa ndani ya kundi na hivyo huwa tunakimbilia kuchukua upande fulani katika pande zinazokuwepo. Lakini hilo huishia kukunyima wewe nguvu na fursa za kufanya makubwa zaidi. Unapochukua upande mmoja na watu wakaona wanakumiliki, wanakuchukulia kawaida. Unakuwa mtumwa (more…)

#SheriaYaLeo (106/366); Tengeneza wafuasi wanaokukubali.

By | February 14, 2022

#SheriaYaLeo (106/366); Tengeneza wafuasi wanaokukubali. Kwenye safari ya mafanikio unawahitaji watu. Unahitaji kuwa kiongozi ambaye una wafuasi wanaokukubali. Wafuasi ambao wanaendana na maono makubwa uliyonayo na ambao wapo tayari kuyasimamia na kuyapambania. Uzuri ni kwamba, kiongozi hahitaji kuwashawishi wafuasi. Wafuasi tayari wapo, wanachotafuta ni kiongozi wa kuambatana naye. Hivyo unapoyaweka (more…)

#SheriaYaLeo (105/366); Ione dunia kama hekalu lililoungana.

By | February 13, 2022

#SheriaYaLeo (105/366); Ione dunia kama hekalu lililoungana. Dunia ni hatari na maadui wako kila mahali. Siyo kila mtu anakutakia mema. Na kadiri unavyopambana kufanikiwa, ndivyo unavyotengeneza maadui wengi zaidi. Hilo linaweza kukufanya ujitenge na watu na kuamua kufanya mambo yako kivyako. Utadhani kufanya hivyo kunawanyima maadui zako fursa ya kukudhuru. (more…)