Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2610; Jenga.

By | February 22, 2022

2610; Jenga. Kila kitu tunachonufaika nacho leo hapa duniani ni kwa sababu watu walichukua hatua ya kukijenga. Chakula, mavazi, nyumba, magari na mengine yote, ni matokeo ya watu kujenga. Watu walioweza kujenga yote tunayofurahia sasa, walikuwa na maono makubwa ambayo wengine hawakuamini yangewezekana. Laki kwa kujiamini na kufanyia kazi, mwishowe (more…)

2609; Asili haipendi utupu.

By | February 21, 2022

2609; Asili haipendi utupu. Kama kuna kitu ambacho asili huwa haikipendi kabisa ni utupu. Safisha chumba chako vizuri kisha kifunge na kuondoka. Ukirudi utakuta kuna vitu vimejikusanya, vumbi, utando wa wadudu na vingine. Lima shamba lako na usipande chochote na haitachukua muda magugu mbalimbali yatakuwa yameota kwenye shamba hilo. Usipofanya (more…)

2608; Mategemeo yako kwa wengine.

By | February 20, 2022

2608; Mategemeo yako kwa wengine. Kila mmoja wetu huwa ana mategemeo fulani kwa watu wengine. Lakini sehemu kubwa ya mategemeo hayo huwa siyo sahihi. Kwa sababu hatujui kile kinachoendelea ndani ya mtu. Unaweza kuwa unategemea mtu awe kwa namna fulani yeye akawa kwa namna ya tofauti. Ukadhani labda amefanya kwa (more…)

2607; Kama siyo maamuzi ya kufa na kupona.

By | February 19, 2022

2607; Kama siyo maamuzi ya kufa na kupona. Kuna maamuzi ya kufa na kupona, maamuzi ambayo ukikosea yana madhara makubwa na huwezi kuyabadili tena. Hayo ni maamuzi machache sana kwenye maisha na utakutana nayo mara chache mno katika kipindi chote cha maisha yako. Lakini kwenye maisha ya kila siku, maamuzi (more…)

2606; Washindani siyo shida.

By | February 18, 2022

2606; Washindani siyo shida. Watu wengi huona ushindani ni hatari kubwa kwenye biashara, au kitu kingine chochote. Huona uwepo wa washindani utawaondoa kabisa kwenye kitu hicho. Kufa kwa biashara au kitu chochote kile huwa hakusababishwi na udhindani, bali ni udhaifu wa ndani. Japo kwa nje ushindani ndiyo utaonekana umesababisha, lakini (more…)

2604; Kiashiria kwamba umepotea.

By | February 16, 2022

2604; Kiashiria kwamba umepotea. Kwenye safari ya mafanikio, kiashiria kikubwa kwamba umeshapotea njia ni pale unapojikuta upo upande wa wengi. Iko hivi rafiki, kwenye kila jamii, huwa kuna upande wa wengi, ambao wanakubaliana kwenye mengi ila hawafanikiwi. Halafu kuna upande wa wachache ambao hawakubaliani na yale ya wengi na ndiyo (more…)

2603; Mbona kila mtu anafanya?

By | February 15, 2022

2603; Mbona kila mtu anafanya? Uzuri wa ukweli ni kwamba huwa haujali watu wanauchukuliaje. Ukweli huwa hautumii nguvu kuwalazimisha watu wakubaliane nao. Bali huwa unabaki kuwa ukweli. Uongo huwa unatumia nguvu kubwa sana kuhakikisha kwamba unakubalika. Unakimbilia kuwateka wengi ukijua wengi ni sehemu nzuri ya kujificha na kukubalika zaidi. Ndiyo (more…)