Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2550; Mtu rahisi kumdanganya.

By | December 24, 2021

2550; Mtu rahisi kumdanganya. Mtu rahisi kabisa kumdanganya kwenye maisha yako ni wewe mwenyewe. Unaya ni hutajua wakati unajidanganya, ni mpaka baadaye sana na mambo yakiwa yameshaharibika ndiyo unagundua ulikuwa unajidanganya. Kwanza, kama unataka sana kitu kiwe kweli au kiwe sahihi kwako, hayo ndiyo utakayoona. Kutakuwa na viashiria kama kitu (more…)

2549; Taarifa ya upande mmoja.

By | December 23, 2021

2549; Taarifa ya upande mmoja. Pale ambapo kuna jambo linalohusisha pande mbili, kamwe usikubali taarifa ya upande mmoja pekee. Hata kama inashawishi na kuaminika kiasi gani, taarifa yoyote ile haijakamilika kama haina pande zote zinazohusika. Sisi binadamu huwa ni rahisi kuona makosa ya wengine lakini ni wagumu sana kuona makosa (more…)

2548; Kutulia siyo tu kwenye kile unachofanya, bali na kwenye maisha pia.

By | December 22, 2021

2548; Kutulia siyo tu kwenye kile unachofanya, bali na kwenye maisha pia. Tumezungumza mara nyingi hapa umuhimu wa kuchagua fursa moja na kutulia nayo kwa muda mrefu ndiyo uweze kupata matunda mazuri. Tunapaswa kuacha kuhangaika na kila fursa mpya, maana huko ni kupoteza nguvu kusiko na tija. Wapo wanaofanya hivyo, (more…)

2547; Safari ya mafanikio haitofautiani na maisha.

By | December 21, 2021

2547; Safari ya mafanikio haitofautiani na maisha. Kwenye maisha, huwa tunajua jinsi vitu vilivyo na kuenda navyo kwa namna vinavyoenda. Kama umeoa au kuolewa, umekaa na mwenza wako kwa muda mrefu na mtaendelea kukaa kwa muda mrefu. Hukai naye ukijiambia kuna kitu fulani unataka kukipata kisha kutokuendelea naye tena. Mwenzako (more…)

2546; Kila kitu kina umuhimu.

By | December 20, 2021

2546; Kila kitu kina umuhimu. Jambo moja kuhusu maisha ni kwamba kila kitu kina umuhimu. Lakini kwa bahati mbaya sana, huwa hatuoni umuhimu wa kitu mpaka pale tunapokuwa tumeshakipoteza. Unapokuwa na kitu unakizoea na kuona ubaya au madhaifu yake kuliko manufaa yake. Ni mpaka pale unapokuwa umekipoteza ndiyo unaona jinsi (more…)

2545; Kuwa fursa inayotafutwa.

By | December 19, 2021

2545; Kuwa fursa inayotafutwa. Kwenye maisha kuna watu wa aina mbili. Aina ya kwanza ni wale ambao kila wakati wanatafuta fursa mpya. Kila wakati kuna kitu kipya wanafanyia kazi. Hawakai kwenye kitu kimoja kwa muda mrefu, kwa sababu wanaposikia kuna kingine kipya na kizuri zaidi, wanaacha walichokuwa wanafanya na kwenda (more…)

2544; Hujuma.

By | December 18, 2021

2544; Hujuma. Kama unaweka juhudi kubwa ili uweze kufanikiwa, lakini juhudi hizo hazileti matunda mazuri na kila wakati unakutana na vikwazo na magumu mbalimbali, jua kuna hujuma zinaendelea. Kuna nguvu kubwa inayopinga kila juhudi unazoweka na ndiyo maana hupati matokeo mazuri. Hujuma zinaweza kuwa zinatoka ndani yako mwenyewe au kutoka (more…)

2543; Zima Washa.

By | December 17, 2021

2543; Zima Washa. Kifaa chochote cha kielektroniki kikikusumbua, kabla hujapeleka kwa fundi, huwa unashauriwa kufanya kitu kimoja, kukizima kisha kukiwasha (restart). Iwe ni siku, redio, tv, kompyuta na vinginevyo, zoezi la kuzima na kuwasha huwa linatatua sehemu kubwa ya matatizo. Mara nyingi vifaa hivyo hukaa sawa baada ya kuzima na (more…)

2542; Tiba Muda.

By | December 16, 2021

2542; Tiba Muda. Kuna mambo unaweza kuwa unalazimisha yawe kwa namna fulani lakini inashindikana. Unaweka juhudi za kila aina ili kupata matokeo unayotaka lakini inashindikana. Unaamua kuachana nayo kwa muda na baadaye unakuja kugundua yamejitatua yenyewe na matokeo yamepatikana bila hata ya kuhangaika sana. Muda ni tiba ya mambo mengi (more…)

2541; Unakopotezea nguvu zako.

By | December 15, 2021

2541; Unakopotezea nguvu zako. Waangalie watoto wadogo, huwa hawawezi kutulia sehemu moja kwa muda mrefu. Waweke watoto mahali na baada ya muda mfupi utawakuta wakirukaruka na kukimbizana. Hiyo ni kwa sababu ndani yao kuna nguvu kubwa inayochemka na inayotafuta mahali pa kutokea. Hiyo ndiyo inayowasukuma wafanye yale wanayofanya. Nguvu hiyo (more…)