Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (93/366); Mfanye bosi wako ajione yuko juu zaidi.

By | February 1, 2022

#SheriaYaLeo (93/366); Mfanye bosi wako ajione yuko juu zaidi. Katika kujenga ubobezi na kufanya makubwa, kuna watu ambao wako juu yako, ambao wana nguvu fulani kwenye hatua unazotaka kupiga. Kitendo tu cha wewe kufanya makubwa, kinawaweka wao kwenye hatari, kwa kuwafanya wajione hawana umuhimu kwako.Hilo litaibua hisia mbaya kwao na (more…)

#SheriaYaLeo (92/366); Usimzidi Bosi Wako.

By | January 31, 2022

#SheriaYaLeo (92/366); Usimzidi Bosi Wako. Sisi binadamu huwa tuna tabia ya wivu na kutokujiamini. Pale mtu mwingine anapofanya vizuri kuliko sisi tunaona anapata fursa nyingi na nzuri zaidi. Unapojihusisha na watu wengine, hupaswi kujali sana kuhusu hilo, wewe pambana kuwa bora na kuzalisha matokeo makubwa. Lakini inapokuja kwa bosi wako, (more…)

#SheriaYaLeo (91/366); Sikiliza Sauti Yako Ya Ndani.

By | January 30, 2022

#SheriaYaLeo (91/366); Sikiliza Sauti Yako Ya Ndani. Ubobezi hautokani na uwezo ambao mtu amezaliwa nao au bahati. Bali ni matokeo ya mtu kusikiliza sauti yake ya ndani na kufuata vile inavyomsukuma. Kila mtu ana sauti hiyo ya ndani, ambayo inajua nini anataka kwenye maisha yake. Ni sauti inayotokana na uwezo (more…)

#SheriaYaLeo (90/366); Ona Zaidi Ya Kinachoonekana.

By | January 29, 2022

#SheriaYaLeo (90/366); Ona Zaidi Ya Kinachoonekana. Watu wa kawaida ambao hawajafikia ubobezi, huwa wanaona yale tu yanayoonekana. Hiyo ni kwa sababu wanakuwa hawajaweka umakini mkubwa kwenye kitu na kukielewa kwa undani. Lakini wale waliofikia ubobezi wa hali ya juu kwenye kile wanachofanya, huwa wanaona zaidi ya kinachoonekana. Kwa sababu wanakuwa (more…)

#SheriaYaLeo (89/366); Unganisha akili na machale.

By | January 28, 2022

#SheriaYaLeo (89/366); Unganisha akili na machale. Kadiri unavyozama kwenye kukifanya kitu, unapata uelewa wa ndani kabisa na kuweza kuona vitu ambavyo wengine hawaoni kirahisi. Unakuwa na machale yanayokuwezesha kujua vitu ambavyo huwezi kuvielezea. Unapata hisia fulani pale kitu kinapokuwa sahihi au siyo sahihi. Unakuwa na uwezo wa kuiona dunia na (more…)

#SheriaYaLeo (88/366); Nenda zaidi ya akili.

By | January 27, 2022

#SheriaYaLeo (88/366); Nenda zaidi ya akili. Wakati wa kuanza kufanya kitu, mtu anatumia zaidi akili kufikiri na kufanya. Hilo linapelekea mtu kufanya kwa namna ambayo wengine pia wanafanya. Ni baada ya kufikia ubobezi wa hali ya juu ndiyo mtu anakuwa amezama kweli kwenye kile anachofanya, kiasi kwamba ufanyaji unakuwa sehemu (more…)

#SheriaYaLeo (87/366); Nguvu ya kuzama kwenye ufanyaji.

By | January 26, 2022

#SheriaYaLeo (87/366); Nguvu ya kuzama kwenye ufanyaji. Ugumu mkubwa uliopo kwenye safari ya ubobezi ni muda mrefu unaohitajika kwenye kufanya kile ulichochagua kufanya. Huku pia ukiwa unashawishiwa na tamaa mbalimbali za vitu vinavyoweza kuwa na manufaa ya muda mfupi ila siyo ya muda mrefu. Unalazimika ujitoe kweli kweli na utoe (more…)

#SheriaYaLeo (86/366); Angalia kinachokosekana.

By | January 25, 2022

#SheriaYaLeo (86/366); Angalia kinachokosekana. Ni kawaida yetu binadamu kuangalia kile kilichopo na kisha kufikiri kwa namna hiyo. Kwa kutumia kilichopo ndiyo tunafanya maamuzi mbalimbali. Lakini kuna taarifa nyingi kwenye yale yanayokosekana. Kuna vitu ambavyo vilitakiwa viwepo ila havipo. Kwa kuanza kuvofikiria vitu hivyo, tunaweza kuja na ubunifu wa kipekee. Kwenye (more…)

#SheriaYaLeo (85/366); Jenga uwezo wa kupokea usiyokubaliana nayo.

By | January 24, 2022

#SheriaYaLeo (85/366); Jenga uwezo wa kupokea usiyokubaliana nayo. Ni kawaida kwetu binadamu tukishajenga mazoea fulani ndiyo huwa tunaendelea nayo. Tunaona hiyo ndiyo namna sahihi ya kufanya kitu husika. Pale tunapokutana na namna ya tofauti na tulivyozoea, huwa tunaikosoa na kuipinga kwamba siyo sahihi. Tunatetea namna yetu kwa kuona ndiyo sahihi (more…)

#SheriaYaLeo (84/366); Akili kama msuli.

By | January 23, 2022

#SheriaYaLeo (84/366); Akili kama msuli. Akili zetu huwa zipo kama msuli. Msuli unapotumika unakua na kuimarika. Na msuli usipotumika unasinyaa na kuwa dhaifu. Akili ikitumika inakua na kuimarika na isipotumika inasinyaa na kuwa dhaifu. Kinachofanya akili isinyae isipotumika ni mambo mawili. Moja ni kupenda mazoea. Tukishakuwa na fikra au njia (more…)