Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (103/366); Watumie Maadui Zako.

By | February 11, 2022

#SheriaYaLeo (103/366); Watumie Maadui Zako. Haijalishi unafanya nini, kuna watu ambao hawatakubaliana na wewe. Watakuona ni mbaya, hufai na watatangaza uadui na wewe. Kwa hali ya kawaida ya kibinadamu na wewe utasukumwa kutangaza nao uadui. Ila jua kufanya hivyo hakuna manufaa kwako au kwao. Mtasumbuana bila ya kuwa na manufaa (more…)

#SheriaYaLeo (102/366); Kupata Unachotaka, Wape watu kile wanachotaka.

By | February 10, 2022

#SheriaYaLeo (102/366); Kupata Unachotaka, Wape watu kile wanachotaka. Katika safari yako ya mafanikio, kuna mengi unayoyahitaji kutoka kwa watu wengine. Hapo ndipo wengi huwa wanajisahau na kudhani watu wana wajibu wa kuwapa kile wanachotaka. Lakini hivyo sivyo binadamu tulivyo. Sisi binadamu ni wabinafsi, huwa tunajali zaidi mambo yetu kuliko mambo (more…)

#SheriaYaLeo (101/366); Usiongee sana.

By | February 9, 2022

#SheriaYaLeo (101/366); Usiongee sana. Unapotaka kuwashawishi watu kwa kutumia maneno, kadiri unavyoongea sana ndiyo unavyoonekana wa kawaida na kukosa udhibiti. Kadiri unavyoongea sana ndivyo unavyojiweka kwenye hatari ya kuongea kitu cha kijinga. Pia kwa kuongea sana watu wanakuzoea na kuona ni mtu wa maneno tu. Kwa kuongea sana unatabirika kirahisi. (more…)

#SheriaYaLeo (100/366); Linda Sifa Yako.

By | February 8, 2022

#SheriaYaLeo (100/366); Linda Sifa Yako. Sifa yako ni eneo muhimu sana la maisha yako. Unaweza kupata au kukosa fursa mbalimbali kutokana na sifa uliyonayo. Watu watakuchukulia kulingana na sifa uliyonayo. Kukuheshimu au kukudharau kutatokana na sifa yako. Katika safari yako ya mafanikio, ni muhimu sana kujenga na kulinda sifa yako. (more…)

#SheriaYaLeo (99/366); Tawala hisia zako.

By | February 7, 2022

#SheriaYaLeo (99/366); Tawala hisia zako. Watu wenye hasira huwa wanaishia kudharauliwa na kuonekana hawana maana kwa sababu hisia zao huwa haziendani na kile kilichotokea. Hasira huwafanya watu wafanye mambo ambayo baadaye huja kuyajutia. Wanayapa mambo uzito uliopitiliza na hatimaye kujibu kwa kupitiliza. Wengi huona hasira ni sifa na kiashiria cha (more…)

#SheriaYaLeo (98/366); Usiwe mkosoaji na mkatishaji tamaa.

By | February 6, 2022

#SheriaYaLeo (98/366); Usiwe mkosoaji na mkatishaji tamaa. Kwa wale unaoshirikiana nao, onyesha kukubali kazi zao. Usiwe mtu wa kukosoa na kuwakatisha tamaa wengine kwenye kila kitu. Kwani hilo litakujengea sifa mbaya na wengi watakuwa wanakukwepa. Hilo litaathiri ushirikiano wako na wengine na kuathiri kazi zako pia. Kadiri unavyokuwa mkosoaji na (more…)

#SheriaYaLeo (97/366); Jifanye mjinga.

By | February 5, 2022

#SheriaYaLeo (97/366); Jifanye mjinga. Kama lengo lako ni kufika ngazi za juu kabisa na kwa sasa uko ngazi za chini, kujionyesha kwamba ni mjuaji hakutakusaidia. Zaidi kutakuwa kikwazo kwako, kwani wale walio juu watakuona wewe ni hatari kwao na kutumia kila njia kukuzuia usipande juu. Lakini ukijifanya mjinga, walio juu (more…)

#SheriaYaLeo (96/366); Jijenge Upya Kitabia.

By | February 4, 2022

#SheriaYaLeo (96/366); Jijenge Upya Kitabia. Tabia ulizonazo na vile watu wanavyokuchukulia siyo kilema ambacho hakiwezi kubadilishwa. Una nguvu ya kujijenga upya kitabia ili uweze kupata nguvu na madaraka ya kufika kule unakotaka kufika. Mara nyingi tabia unazokuwa nazo na vile watu wanavyokuchukulia inakuwa kikwazo kikubwa kwako kufika kule unakotaka kufika. (more…)

#SheriaYaLeo (95/366); Jua wakati wa kutoa na kupokea sifa.

By | February 3, 2022

#SheriaYaLeo (95/366); Jua wakati wa kutoa na kupokea sifa. Huwa tunapenda kupewa sifa kwa kile ambacho tumewezesha kifanyike au kikamilike. Ni kawaida kwetu binadamu kupenda kusifiwa, kwani huwa tunaona tumethaminiwa zaidi. Kama ambavyo tunajisikia vizuri tukisifiwa, ndivyo pia wengine wanajisikia vizuri wanaposifiwa. Na hapa ndipo unapaswa kujua wakati gani wa (more…)

#SheriaYaLeo (94/366); Jua  nani mwenye mamlaka.

By | February 2, 2022

#SheriaYaLeo (94/366); Jua nani mwenye mamlaka. Katika eneo lolote lile, iwe ni taasisi, biashara au jamii, kuna watu wachache au mmoja ambaye ndiye mwenye mamlaka makubwa. Mara nyingi mtu au watu hao siyo wale wanaoonekana kuwa viongozi, wanaweza kuwa watu wengine kabisa, ambao wanafanya mambo yao nyuma ya pazia. Unapotaka (more…)