Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (13/366); Bobea kwenye vitu vidogo.

By | November 13, 2021

#SheriaYaLeo (13/366); Bobea kwenye vitu vidogo. Pale unapokuwa umekabiliwa na mapungufu badala ya uimara, huu ndiyo mkakati unaopaswa kufanyia kazi; puuza udhaifu wako na kataa ushawishi wa kutaka kuwa kama wengine. Badala yake weka juhudi zako zote kwenye vitu vidogo vidogo ambavyo uko vizuri katika kuvifanya. Usihangaike na mambo makubwa (more…)

#SheriaYaLeo (11/366); Nini Kinakupa Shauku Zaidi?

By | November 11, 2021

#SheriaYaLeo (11/366); Nini Kinakupa Shauku Zaidi? Kila mmoja wetu kuna kitu ambacho akikifanya anajisikia vizuri zaidi na kupata msukumo wa kuendelea kukifanya kwa muda mrefu bila kuchoka. Katika kufanya kitu hicho, mtu unakuwa na nguvu kubwa na ubunifu ambao wengine wanaushangaa. Wakati kwa wengine kufanya kitu hicho ni kazi ngumu, (more…)

#SheriaYaLeo (10/366); Kubali na Ishi Uajabu Wako.

By | November 10, 2021

#SheriaYaLeo (10/366); Kubali na Ishi uajabu wako. Kuna namna ambavyo uko tofauti kabisa na watu wengine. Utofauti huo umewafanya watu wakuone wewe ni mtu wa ajabu. Uajabu wako huo umekuwa unawafanya baadhi ya watu wakuchukie, wakudharau, wakupinge na hata wakukosoe. Kwa sababu tunapenda sana kukubalika na wengine, huwa tunakuwa tayari (more…)

#SheriaYaLeo (9/366); Pata hamasa kutoka kwa mashujaa wako.

By | November 9, 2021

#SheriaYaLeo (9/366); Pata hamasa kutoka kwa mashujaa wako. Kuna watu ambao ukiwaona wanavyofanya kazi zao unapata hamasa kubwa sana ndani yako. Unavutiwa sana na aina ya maisha wanayoishi na yale wanayofanya. Watu hao wanakupa hamasa na msukumo wa kufanya makubwa kama wao wanavyofanya. Hao ndiyo mashujaa wako, ambao ukiwatumia vizuri (more…)

#SheriaYaLeo (8/366); Kubali Na Ishi Utofauti

By | November 8, 2021

#SheriaYaLeo (8/366); Kubali Na Ishi Utofauti Wako. Kila mtu ana utofauti fulani ambao upo ndani yake. Kuna namna ya ufanyaji wa mambo ambayo ni ya tofauti kabisa. Na pia kuna vitu vya tofauti kabisa vinavyomvutia mtu tofauti na wengine. Kwa walio wengi huwa wanapuuza utofauti wao na kuchagua kufanya yale (more…)

#SheriaYaLeo (7/365); Pesa Na Mafanikio.

By | November 7, 2021

#SheriaYaLeo (7/365); Pesa Na Mafanikio. Kwa walio wengi, hitaji la kupata pesa na mafanikio linaweza kuwa motisha mkubwa kwao kuwasukuma kufanya makubwa. Kwa watu wa aina hii huona hakuna haja ya kuhangaika kulijua kusudi la maisha yao. Huona huko ni kupoteza muda na hivyo huachana na hilo na kuhangaika na (more…)

#SheriaYaLeo (6/366); Mabadiliko Ni Sheria.

By | November 6, 2021

#SheriaYaLeo (6/366); Mabadiliko Ni Sheria. Mabadiliko ni sheria ya maisha. Hakuna kitu chochote kinachobaki kilivyo, kila kitu kinabadilika. Katika kukabiliana na mabadiliko kwenye kazi na biashara zako, endana na mabadiliko badala ya kuyapinga. Tambua kwamba hujafungiwa kwenye kufanya kitu cha aina fulani pekee. Uaminifu wako siyo kwenye kazi, biashara au (more…)

#SheriaYaLeo (5/366); Jua kinachokuvutia na zama

By | November 5, 2021

#SheriaYaLeo (5/366); Jua kinachokuvutia na zama ndani. Kama umefanyia kazi sheria 4 zilizopita, utakuwa umeshajua ni kitu au vitu gani unavyovutiwa sana kuvifanya. Vitu vinavyotokana na sauti yako ya ndani, ambavyo huchoki kuvifanya na upo tayari kuvifanya bila kujali wengine wanasema au kufanua nini. Hivyo ndiyo vitu ambavyo vinatoka ndani (more…)

#SheriaYaLeo (4/366); Tayari Iko Ndani Yako.

By | November 4, 2021

#SheriaYaLeo (4/366); Tayari Iko Ndani Yako. Kujua wito na kusudi la maisha yako, huhitaji kwenda kutafuta mahali popote pale. Tayari hilo lipo ndani yako. Kama bado hujajua ni kwa sababu imefukiwa na miaka mingi uliyoishi kwa kupuuza kile kilicho ndani yako. Hivyo unachopaswa kufanya sasa ni kuchimba kile kilicho ndani (more…)