Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (23/366); Yagawe malengo yako

By | November 23, 2021

#SheriaYaLeo (23/366); Yagawe malengo yako makubwa kwenye vipande vidogo. Kuwa na malengo makubwa na ya muda mrefu kunakupa msukumo na umakini mkubwa wa kuyafikia. Malengo hayo ambayo ni makubwa, mfano biashara kubwa ya kujenga huwa yanakupa shauku kubwa na kukusukuma uwe bora zaidi. Lakini pia malengo hayo makubwa huwa yana (more…)

#SheriaYaLeo (22/366); Tumia ukinzani na magumu.

By | November 22, 2021

#SheriaYaLeo (22/366); Tumia ukinzani na magumu. Ufunguo wa mafanikio kwenye tasnia yoyote ile ni kujijengea ujuzi wa aina mbalimbali kisha kuchanganya ujuzi huo kwa namna ya kipekee. Lakini mchakato wa kufanya hivyo unaweza kuwa mgumu, wenye maumivu na kukatishwa tamaa. Maana kadiri unavyokwenda unagundua ukomo na ukosefu wa ujuzi muhimu. (more…)

#SheriaYaLeo (21/366); Kuwategemea wengine ni

By | November 21, 2021

#SheriaYaLeo (21/366); Kuwategemea wengine ni tatizo. Hakuna kitu kibaya kama kuweka mategemeo yako yote kwa watu wengine. Utegemezi unakuweka kwenye hatari ya kuathiriwa na hisia hasi kama usaliti, kukatishwa tamaa, kuvurugwa na msongo. Hisia hizi huharibu sana utulivu wa akili yako. Kujitegemea mwenyewe ni muhimu sana kwa utulivu na mafanikio (more…)

#SheriaYaLeo (20/366); Ona Ubobezi Kama Ukombozi.

By | November 20, 2021

#SheriaYaLeo (20/366); Ona Ubobezi Kama Ukombozi. Dunia imejaa matatizo mbalimbali, na sehemu kubwa ya matatizo hayo tumeyatengeneza wenyewe. Kutatua matatizo hayo kunahitaji juhudi na ubunifu mkubwa. Kutegemea mazoea, teknolojia na kuwa mwema haitatusaidia. Tunahitaji nguvu ya kuweza kuyatambua matatizo hayo na kutengeneza taasisi mpya zinazoweza kukabiliana na mabadiliko tunayopitia. Ni (more…)

#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya

By | November 19, 2021

#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya Ndani. Upo hapa duniani siyo tu kwa ajili ya kutimiza tamaa zako na kutumia vile wengine wametengeneza, bali pia kuchangia, kutimiza kusudi kubwa. Ili kuweza kutimiza kusudi hilo, lazima utengeneze kile cha kipekee ndani yako. Acha kusikiliza sana maneno na maoni ya wengine wanaokuambia (more…)

#SheriaYaLeo (18/366); Acha Kutaka Kumfurahisha Kila Mtu.

By | November 18, 2021

#SheriaYaLeo (18/366); Acha Kutaka Kumfurahisha Kila Mtu. Utalipa gharama kubwa sana kwa kutaka kumfurahisha kila mtu na kuonekana kujali kuliko kuyaishi maisha yako halisi na kuonyesha kivuli chako. Kuyaishi maisha yako; Kwanza kabisa unapaswa kuheshimu maoni yako kuliko ya wengine, hasa inapokuja kwenye eneo lako la ubobezi, eneo ambalo umechagua (more…)

#SheriaYaLeo (17/366); Chanzo sahihi cha ubunifu.

By | November 17, 2021

#SheriaYaLeo (17/366); Chanzo sahihi cha ubunifu. Unapaswa kubadili dhana yako ya ubunifu na kuuangalia kwenye kona mpya. Mara nyingi watu huhusianisha ubunifu na akili au namna fulani ya kufikiri. Ukweli ni kwamba ubunifu ni kitendo kinachohusisha nafsi yako nzima – kuanzia hisia, nguvu, tabia na fikra. Kuja na uvumbuzi mpya, (more…)

#SheriaYaLeo (16/366); Hakuna Wito Bora Zaidi Ya Mwingine.

By | November 16, 2021

#SheriaYaLeo (16/366); Hakuna Wito Bora Zaidi Ya Mwingine. Tambua kwamba mchango wako kwenye jamii unaweza kuja kwa namna tofauti tofauti. Siyo lazima uwe mjasiriamali mkubwa, kiongozi mkubwa au mvumbuzi ndiyo uweze kuleta mchango mkubwa kwenye jamii. Unaweza kufanya makubwa ukiwa peke yako au ukiwa ndani ya taasisi kubwa. Muhimu ni (more…)

#SheriaYaLeo (15/366); Acha Kusudi Likuongoze.

By | November 15, 2021

#SheriaYaLeo (15/366); Acha Kusudi Likuongoze. Kitu muhimu ambacho watu wengi wanakikosa kwenye zama tunazoishi sasa ni kusudi kubwa la maisha yao. Kipindi cha nyuma watu walipewa kusudi la maisha na dini au jamii zao. Kwa sababu kipindi hicho dini na jamii zilikuwa na nguvu kubwa ya kuwaamulia watu maisha yao. (more…)

#SheriaYaLeo (14/366); Epuka Njia Ya Uongo.

By | November 14, 2021

#SheriaYaLeo (14/366); Epuka Njia Ya Uongo. Njia ya uongo ni ile ambayo inatuvutia kwa sababu zisizo sahihi – fedha, umaarufu, kuwaridhisha wengine na kadhalika. Sababu hizo zinakusukuma kufanya kitu ambacho siyo sahihi kwako, ambacho kinakuzuia usiishi kusudi na wajibu wako. Kama unafanya kwa ajili ya umaarufu, unaishia kuona utupu ulio (more…)