#SheriaYaLeo (99/366); Tawala hisia zako.

By | February 7, 2022

#SheriaYaLeo (99/366); Tawala hisia zako. Watu wenye hasira huwa wanaishia kudharauliwa na kuonekana hawana maana kwa sababu hisia zao huwa haziendani na kile kilichotokea. Hasira huwafanya watu wafanye mambo ambayo baadaye huja kuyajutia. Wanayapa mambo uzito uliopitiliza na hatimaye kujibu kwa kupitiliza. Wengi huona hasira ni sifa na kiashiria cha (more…)

2594; Rahisi kufanya.

By | February 6, 2022

2594; Rahisi kufanya. Kitu ambacho ni rahisi kufanya huwa kinafanywa na watu wengi. Kitu ambacho kinafanywa na watu wengi huwa kinakuwa na ushindani mkali. Kitu chenye ushindani mkali huwa kinakuwa na faida kidogo. Hii haimaanishi uende kufanya mapya kabisa. Bali inamaanisha chochote unachofanya, hakikisha kuna namna unafanya ambavyo wengine hawawezi (more…)

#SheriaYaLeo (98/366); Usiwe mkosoaji na mkatishaji tamaa.

By | February 6, 2022

#SheriaYaLeo (98/366); Usiwe mkosoaji na mkatishaji tamaa. Kwa wale unaoshirikiana nao, onyesha kukubali kazi zao. Usiwe mtu wa kukosoa na kuwakatisha tamaa wengine kwenye kila kitu. Kwani hilo litakujengea sifa mbaya na wengi watakuwa wanakukwepa. Hilo litaathiri ushirikiano wako na wengine na kuathiri kazi zako pia. Kadiri unavyokuwa mkosoaji na (more…)

#SheriaYaLeo (97/366); Jifanye mjinga.

By | February 5, 2022

#SheriaYaLeo (97/366); Jifanye mjinga. Kama lengo lako ni kufika ngazi za juu kabisa na kwa sasa uko ngazi za chini, kujionyesha kwamba ni mjuaji hakutakusaidia. Zaidi kutakuwa kikwazo kwako, kwani wale walio juu watakuona wewe ni hatari kwao na kutumia kila njia kukuzuia usipande juu. Lakini ukijifanya mjinga, walio juu (more…)

2592; Kula pipi na kubaki nayo.

By | February 4, 2022

2592; Kula pipi na kubaki nayo. Kutaka kula pipi na wakati huo huo kubaki nayo ndiyo kikwazo kikubwa kwa wengi kupata mafanikio makubwa. Yaani mtu anataka apate ambacho hana, lakini pia hataki kupoteza alichonacho. Hilo ni jambo lisilowezekana kwa namna yoyote ile, huwezi kupata ambacho huna bila kupoteza kile ambacho (more…)

#SheriaYaLeo (96/366); Jijenge Upya Kitabia.

By | February 4, 2022

#SheriaYaLeo (96/366); Jijenge Upya Kitabia. Tabia ulizonazo na vile watu wanavyokuchukulia siyo kilema ambacho hakiwezi kubadilishwa. Una nguvu ya kujijenga upya kitabia ili uweze kupata nguvu na madaraka ya kufika kule unakotaka kufika. Mara nyingi tabia unazokuwa nazo na vile watu wanavyokuchukulia inakuwa kikwazo kikubwa kwako kufika kule unakotaka kufika. (more…)

2591; Hakuna jipya.

By | February 3, 2022

2591; Hakuna jipya. Sisi binadamu wakati mwingine huwa tunashangaza sana. Tunapenda kufanya vitu kwa mazoea, lakini inapokuja kwenye kufanikiwa, tunapenda vitu vipya vipya. Kufanya kitu kile kile kwa kurudia rudia na kwa muda mrefu huwa inawachosha wengi. Wanakimbilia kutafuta vitu vipya vya kufanya, ambavyo vinawasisikua kwa upya wake, lakini haviwi (more…)

#SheriaYaLeo (95/366); Jua wakati wa kutoa na kupokea sifa.

By | February 3, 2022

#SheriaYaLeo (95/366); Jua wakati wa kutoa na kupokea sifa. Huwa tunapenda kupewa sifa kwa kile ambacho tumewezesha kifanyike au kikamilike. Ni kawaida kwetu binadamu kupenda kusifiwa, kwani huwa tunaona tumethaminiwa zaidi. Kama ambavyo tunajisikia vizuri tukisifiwa, ndivyo pia wengine wanajisikia vizuri wanaposifiwa. Na hapa ndipo unapaswa kujua wakati gani wa (more…)

2590; Kujipendekeza.

By | February 2, 2022

2590; Kujipendekeza. Sisi binadamu ni viumbe wa kihisia, huwa tunafanya maamuzi kwa hisia na kisha kuyahalalisha kwa mantiki. Chochote unachotaka kwenye maisha yako kinatoka kwa watu wengine. Unawategemea sana watu wengine, hakuna unachoweza peke yako. Ukiwafanya watu wajisikie vizuri, watakuwa tayari kukupa unachotaka. Ukiwafanya wajisikie vibaya hawatakuwa tayari kukupa unachotaka. (more…)