Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3170; Umelipa ada.

By | September 5, 2023

3170; Umelipa ada. Rafiki yangu mpendwa,Hakuna kitu ambacho kinauma kwenye maisha kama kufanya makosa.Na hilo huwa linaumiza zaidi pale makosa yanayofanyika yanapokuwa ya kifedha.Yaani pale unapokosea na kuingia gharama kwenye makosa hayo huwa linaumiza sana. Mwenzetu mmoja hapa amekuwa na safari ya kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kukuza (more…)

3169; Msukumo wa kufanya maamuzi.

By | September 4, 2023

3169; Msukumo wa kufanya maamuzi. Rafiki yangu mpendwa,Kama kuna kitu ambacho watu huwa wanakikwepa sana ni kufanya maamuzi.Kama kuna nafasi ya watu kusubiri kufanya maanuzi, wataitumia kusubiri. Unaweza kuona ni jambo la kistaarabu kuwaacha watu mpaka wawe tayari kufanya maamuzi wao wenyewe.Lakini inapokuja kwenye mambo muhimu, hupaswi kuwa hivyo. Kwa (more…)

3168; Lugha pekee tunayoielewa hapa.

By | September 3, 2023

3168; Lugha pekee tunayoielewa hapa. Rafiki yangu mpendwa,Kuna lugha nyingi ambazo huwa zinaongelewa na wengi.Lakini hapa kwenye programu yetu ya Bilionea Mafunzoni, tunaielewa lugha moja pekee. Ni lugha ambayo sote tumeikubali na ndiyo tunaipambania katika mambo yote tunayoyafanya.Ni lugha ambayo inatuwajibisha kwenye kila kitu tunachokifanya kwenye hii safari. Ndiyo lugha (more…)

3167; Msukumo sahihi.

By | September 2, 2023

3167; Msukumo sahihi. Rafiki yangu mpendwa,Sisi binadamu huwa hatufanyi maamuzi na kuchukua hatua kama hakuna msukumo ndani yetu.Ni lazima kuwe na msukumo kwanza, tena ambao unagusa hisia ndiyo tuweze kuamua na kuchukua hatua.Kadiri maamuzi na hatua tunazochukua zinavyokuwa kubwa, ndivyo msukumo unavyopaswa kuwa mkubwa pia. Kabla ya kuendelea nitakupa mfano (more…)

Barua ya XVIII; Kuhusu sherehe na kufunga.

By | September 1, 2023

Barua ya XVIII; Kuhusu sherehe na kufunga. Rafiki yangu Mstoa, Kwenye mwaka huwa kuna miezi ambayo huwa ina sherehe nyingi.Ni miezi ambayo watu hupumzika kabisa kazi zao na kusherekea.Katika kipindi hicho, watu hula na kunywa mpaka kusaza.Hiyo huwa ni miezi ambayo watu hushindwa kujizuia hasa kwenye nidhamu walizokuwa wanajijengea.Mfano mtu (more…)

3166; Bakiza moja.

By | September 1, 2023

3166; Bakiza moja. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye harakati za kujitafuta, nimewahi kufanya kilimo cha matikiti maji.Nilishirikiana na rafiki yangu mmoja na tulijipanga vyema kuhakikisha tunapata matokeo mazuri. Baada ya kuandaa shamba, kupanda na miche kuanza kutoa matunda, tulitafuta mtaalamu wa kilimo na kwenda naye shambani ili aangalie na kutushauri zaidi mambo (more…)

3165; Huruma

By | August 31, 2023

3165; Huruma Rafiki yangu mpendwa,Huwa kuna taratibu mbalimbali ambazo huwa tumejiwekea kwenye kushirikiana na watu wengine.Kwa taratibu hizo, huwa tuna hatua za kuchukua pale mtu anapokwenda tofauti na anavyopaswa kwenda. Kuna watu ambao wanakuwa wameenda tofauti kabisa na taratibu ambazo tumeweka.Lakini inapokuja kwenye kuchukua hatua zinazopaswa kuchukuliwa, huruma inatuingia.Tunawaonea watu (more…)

3164; Uchumi wa biashara.

By | August 30, 2023

3164; Uchumi wa biashara. Rafiki yangu mpendwa,Biashara nyingi sana zinazoanzishwa huwa zinaishia kufa ndani ya muda mfupi tangu kuanzishwa kwake.Na hata zile ambazo hazifi, nyingi zimekuwa hazipati ukuaji mkubwa, badala yake zinabaki kuwa ndogo. Sababu nyingi zimekuwa zinatolewa juu ya biashara kufa.Na ya kwanza kabisa ambayo imekuwa inasemwa sana ni (more…)

3163; Mazoea na Kujisahau.

By | August 29, 2023

3163; Mazoea na Kujisahau. Rafiki yangu mpendwa,Sisi binadamu tumeumbiwa kusahau.Kusahau kumekuwa na manufaa makubwa sana kwetu kwani kumewezesha kuendelea na maisha licha ya mambo mbalimbali tunayoyapitia. Kama tungekuwa tunakumbuka kila ambacho tumepitia kwenye maisha, tusingeweza kuwa na maisha tulivu.Uzito wa kumbukumbu tunazokuwa nazo ungetuelemea sana kiasi cha kushindwa kufanya maamuzi (more…)

3162; Kufanya na kutokufanya.

By | August 28, 2023

3162; Kufanya na kutokufanya. Rafiki yangu mpendwa,Kila mtu huwa anakosea kwenye maisha.Hayupo hata mmoja ambaye anapatia mara zote.Tunachotofautiana ni aina ya makosa, ukubwa na madhara. Hapa tutaangalia aina ya makosa na jinsi yanavyowatofautisha watu kwenye matokeo wanayopata. Kuna aina mbili za makosa.Aina ya kwanza ni makosa ya kufanya. Hapa ni (more…)