Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3057; Kwa nini nataka uuze.

By | May 15, 2023

3057; Kwa nini nataka uuze. Rafiki yangu mpendwa,Kama ambavyo nimeshakuandikia mara kwa mara, una malengo makubwa matatu kwenye biashara yako.Malengo hayo ni kujenga mfumo wa kuiendesha biashara, kujenga timu imara na kujenga wateja waaminifu. Ili uweze kutekeleza malengo hayo, kuna majukumu makuu mawili ambayo unapaswa kuyatekeleza. Na majukumu hayo yanakutaka (more…)

3056; Unajivuruga mwenyewe.

By | May 14, 2023

3056; Unajivuruga mwenyewe. Rafiki yangu mpendwa,Kutokana na ugumu na changamoto za safari ya mafanikio, watu wengi huwa wanatafuta watu wa kuwapelekea lawama pale mambo yao yanavyokwenda tofauti na matarajio. Hapo watu huona wazi kwamba wamevurugwa na wengine ambao wamefanya tofauti na walivyotarajia. Lakini huo siyo ukweli, hakuna mtu yeyote yule (more…)

3055; Usijipe kazi usizoziweza.

By | May 13, 2023

3055; Usijipe kazi usizoziweza. Rafiki yangu mpendwa,Safari ya mafanikio ambayo tupo ni safari ngumu na ndefu.Ugumu wa safari hii ni kazi kubwa tunayopaswa kuweka ili kupata matokeo makubwa tunayotaka kuyapata. Wengi huwa wanashindwa kazi hiyo, siyo kwa sababu haiwezekani, bali kwa sababu wanachoka kwa kazi nyingine wanazokuwa wamejipa. Yaani wanakuwa (more…)

Barua ya II; Usumbufu Kwenye Usomaji.

By | May 12, 2023

Barua ya II; Usumbufu Kwenye Usomaji. Rafiki yangu Mstoa,Maisha ni darasa ambalo halina kuhitimu. Hiyo ina maana kwamba kila wakati mtu unapaswa kuwa unajifunza. Zipo njia nyingi za kujifunza, na moja iliyo kuu na ambayo imedumu kwa miaka mingi zaidi ni kusoma vitabu. Tangu enzi na enzi, maarifa yamekuwa yanashirikishwa (more…)

3054; Uhakika wa ushindi.

By | May 12, 2023

3054; Uhakika wa ushindi. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye safari ya maisha ya mafanikio, ushindi ndiyo kitu ambacho kila mtu anakitaka.Lakini pia kimekuwa ndiyo kitu adimu sana. Ni watu wachache mno ndiyo wamekuwa wanapata mafanikio wanayoyataka. Kwa jinsi ambavyo mafanikio yamekuwa adimu, yanaonekana kama ni kitu cha kubahatisha, ambacho mtu hawezi kuwa (more…)

3053; Turudi kwenye misingi.

By | May 11, 2023

3053; Turudi kwenye misingi. Rafiki yangu mpendwa,Iwapo unajenga nyumba ya ghorofa, lakini kila unapojaribu kwenda ngazi za juu zaidi unakwama, hapo inabidi urudi kwenye msingi.Unapaswa kuangalia msingi mzima ambapo ghorofa hiyo imejengwa na kama utagundua msingi siyo sahihi basi unapaswa kuuboresha kwanza kabla hujaendelea. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye kila (more…)

3052; Siyo unachotaka, bali unachotoa.

By | May 10, 2023

3052; Siyo unachotaka, bali unachotoa. Rafiki yangu mpendwa,Karibu kila mtu kwenye maisha anataka kupata mafanikio makubwa.Lakini kwenye uhalisia ni watu wachache sana wanaopata mafanikio makubwa wanayoyataka. Tafiti nyingi zimefanywa ili kujua nini kinawatofautisha wanaofanikiwa na wanaoshindwa.Vitu vingi vya nje ambavyo wengi walidhani ndiyo vinawatofautisha wanaofanikiwa na wanaoshindwa, vimeonekana kutokuwa na (more…)

3051; Kupanda na kushuka.

By | May 9, 2023

3051; Kupanda na kushuka. Rafiki yangu mpendwa, Safari ya mafanikio huwa ina kupanda na kushuka.Hizo ni pande mbili za safari hiyo, ambazo huwa hazifanani.Upande mmoja unahitaji kazi kubwa wakati upande mwingine hauhitaji kazi yoyote. Kupanda kunahitaji kazi, kunahitaji juhudi kubwa kuwekwa ili kuvuka nguvu kubwa ya mvutano inayofanya vitu vibaki (more…)

3050; Wateke.

By | May 8, 2023

3050; Wateke. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye malengo makubwa matatu tunayoyafanyia kazi kwenye kujenga biashara, yaani MFUMO, TIMU na WATEJA, lengo la TIMU ndiyo limekuwa gumu zaidi. Kila ambaye ameshachukua hatua kwenye kujenga timu, amekutana na changamoto nyingi sana.Changamoto ya kwanza ni kukosekana kwa watu sahihi ambao wanaweza kutekeleza majukumu yaliyopo.Changamoto ya (more…)

3049; Mambo ambayo huhitaji kukumbusha, lakini inabidi.

By | May 7, 2023

3049; Mambo ambayo huhitaji kukumbusha, lakini inabidi. Rafiki yangu mpendwa,Kuna mambo ya msingi kabisa kwenye safari ya maisha na mafanikio ambayo huhitaji kuwa unakumbushwa kila mara.Haya ni mambo ambayo unapaswa kuwa unayaelewa kutoka ndani kabisa ya moyo wako. Lakini kwa sababu binadamu tuna tabia ya kusahau mambo, hata yale ya (more…)