Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2270; Mapema Iwezekanavyo Ni Sasa…

By | March 19, 2021

Kama kuna kitu unajiambia unataka kuanza kukifanya mapema iwezekanavyo, basi jua mapema hiyo ni sasa. Kama utajiambia kuna mapema nyingine zaidi ya sasa, jua hutafanya hicho ulichopanga kufanya au utachelewa sana kuanza kiasi kwamba unapokuja kukifanya, fursa inakuwa imekuacha. Hivyo unapaswa kubadili kauli zako, kwa yale muhimu, badala ya kujiambia (more…)

2269; Kujenga Uaminifu…

By | March 18, 2021

Njia pekee ya kujenga uaminifu kwa wengine, kwenye jambo lolote lile ni kuwa mkweli, kusimama kwenye ukweli. Mara nyingi watu hudanganya kwa nia njema, kwa kuona wakitoa ukweli mapema wanaweza kuwaumiza watu. Lakini ukweli haujawahi kushindwa, ukweli hujitokeza hadharani tu, hivyo kuuficha sasa kwa sababu hutaki watu waumie, hujawazuia kuumia, (more…)

2268; Kwa Nini Siyo Rahisi Kuyaishi Maisha Yako…

By | March 17, 2021

Huwezi kufanikiwa kama huyaishi maisha yako, kama huwi wewe, ambaye hakuna anayeweza kukushinda kwa kuwa wewe. Lakini kuyaishi maisha yako ni rahisi kusema kuliko kutenda. Na hiyo ni kwa sababu jamii imeshakuweka kwenye boksi fulani, inatulia unapokuwa umekaa kwenye boksi hilo. Lakini siku utakayoamua kutoka kwenye boksi hilo, dunia nzima (more…)

2266; Unasimama Wapi?

By | March 15, 2021

Ni asili yetu binadamu kutaka kupendwa na kila mtu, hivyo huwa tunajitahidi kufanya kile ambacho kitawafurahisha walio wengi. Lakini kila tunapojaribu kufanya hivyo, tunaishia kufanya kisichokuwa na msimamo na kisichomfurahisha yeyote. Kama tunataka kupata wafuasi au watu wanaokubaliana na sisi kwenye maisha, lazima tuchague msimamo ulio wazi kwa wote. Kwa (more…)

2265; Umuhimu Wa Kupenda Unachofanya…

By | March 14, 2021

Kupenda unachofanya ni kitu ambacho kimekuwa kinashauriwa sana kama mtu anataka kufanikiwa kwenye jambo lolote lile. Lakini ushauri huo haumaanishi kwamba hutaumia kwenye kukifanya, utaumia sana, ila kwa kuwa unakipenda, utayavumilia mateso unayokutana nayo. Mafanikio makubwa yanahitaji gharama kubwa, gharama ambayo kama huna msukumo mkubwa kutoka ndani yako, hutaweza kuilipa. (more…)

2264; Kutokujua Sheria Siyo Kinga…

By | March 13, 2021

Wanasheria huwa wana msemo kwamba kutokujua sheria siyo kinga ya kutokuhukumiwa na sheria hiyo. Unaweza kuona hilo siyo sawa, lakini ndivyo asili inavyofanya kazi. Maisha yetu yote, tumekuwa tunajifunza kwa kujaribu na kukosea, maana hiyo ndiyo njia pekee tunayoielewa. Ulipokuwa mtoto uliimbiwa sana usichezee moto, lakini hukusikia, mpaka siku ulipokuunguza (more…)

2263; Kuwaangalia Wengine Ndiyo Kunakupoteza…

By | March 12, 2021

Mwekezaji bilionea Warren Buffett amewahi kusema kinachopelekea maanguko ya uchumi ni tabia ya watu kufuata kundi. Anasema watu wengi huwa hawawezi kutulia pale wanapoona kundi kubwa la watu likifanya kitu, huwa hawataki wapitwe, hivyo hukimbilia kufanya na kuishia kuanguka. Ndiyo maana watu wengi hununua hisa wakati zinapanda bei na kuziuza (more…)

2262; Mtu Asiye Na Madhaifu…

By | March 11, 2021

Kila mtu huwa ana madhaifu yake, ni wale wanaoyatambua na kuhakikisha hayawi kikwazo kwao ndiyo hufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yao. Wale wanaoyakataa madhaifu yao huwa ni kiburi tu walichonacho au ujinga wa kutokujitambua, lakini huwa hawafanikiwi. Kwa sababu hata wapate fursa nzuri kiasi gani, madhaifu yao huwa kikwazo. Kila (more…)

2261; Tumia Thamani Badala Ya Uhaba…

By | March 10, 2021

Utajiri wa zamani ulijengwa kwenye misingi ya uhaba, kwamba rasilimali muhimu ni chache, wachache wanazihodhi na kunufaika kwa kiwango kikubwa. Hivyo ndivyo zama za kilimo zilivyofanya kazi, wachache walimiliki mashamba na wengi kuwa wafanyakazi au watumwa kwenye mashamba hayo. Kadhalika zama za viwanda zikarithi hilo, kumiliki kiwanda ilihitaji mtaji mkubwa, (more…)