Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2260; Kutaka Fedha Kusikupe Upofu…

By | March 9, 2021

Uliwahi kufanyika utafiti kwa wale wanaofanya utapeli. Utafiti huo ulitaka kujua iwapo watu wanaofanya hivyo hawasutwi nafsi zao kwa kuwaibia na kuwatapeli wengine. Mmoja wa watu waliohojiwa kwenye utafiti huo alitoa jibu ambalo liliwafanya watafiti wapate mtazamo ambao hawakuwa nao awali. Mtu huyo aliwaambia ni kweli tabia ya utapeli inamuumiza (more…)

2259; Linda Juhudi Unazoweka Sasa Unufaike Nazo Baadaye…

By | March 8, 2021

Asili ina kanuni zake nyingi, huwezi kupanda mbegu na kuivuna hapo hapo ukaila. Lazima uwe na subira, lazima uipe mbegu hiyo muda, ikue, izae mbegu nyingi zaidi ndipo uvune na kuweza kula. Sasa pata picha umekuwa unaona shamba liko mahali, lina rutuba nzuri na hakuna anayelilima. Unaona unaweza kutumia shamba (more…)

2258; Hakuna Anayekusumbua, Bali Unajisumbua Mwenyewe…

By | March 7, 2021

Huwa situmii kabisa mitandao ya kijamii, hivyo ninapokutana na watu wakilalamikia yale wengine wanafanya kwenye mitandao hiyo huwa nawashangaa. Unakuta mtu analalamika kwamba hapendezwi na yale wengine wanafanya kwenye mitandao hiyo. Mimi huwa nina swali moja kwao, mtu huyo unayemlalamikia amekuja nyumbani kwako na kufanya kitu hicho? Au amekulazimisha umfuatilie (more…)

2257; Hujui Dunia Ina Nini Kwa Ajili Yako…

By | March 6, 2021

Huwa tunahangaika na kujisumbua na mambo ambayo bado hayajatokea, kwa kutabiri namna ambavyo mambo yatatokea. Lakini mara zote dunia hutushangaza, kwani kinachokuja kutokea ni tofauti kabisa na tulivyokuwa tunategemea na hivyo kuhofia. Mifano ni mingi uliyonayo kwenye maisha yako, ya mambo ambayo ulihofia sana, lakini yakaja kutokea tofauti na ulivyotegemea. (more…)

2256; Mazoea Ndiyo Yanayokupoteza…

By | March 5, 2021

Mazoea ni tabia, pale unaporudia rudia kufanya kitu, akili inakariri na hivyo unajikuta unaweza kukifanya bila hata ya kufikiri. Kuna mambo mazoea ni mazuri kwa sababu inapunguza mzigo kwa akili kufikiri kila jambo. Mfano shughuli ndogo ndogo na za kawaida unazofanya kila siku. Lakini kuna mambo ambayo ukiweka mazoea tu (more…)

2255; Mashindano Yasiyo Na Zawadi…

By | March 4, 2021

Jamii ikitaka kututega tufanye kitu, huwa inakiweka kwa namna ya mashindano. Kukishakuwa na hali ya kushindana, hata kama ushindi hauna zawadi, mtu utasukumwa kushindana ili ushinde. Unafikiri nini kinafanya mitandao ya kijamii ipate watumiaji wengi na wanaoitumia kwa muda mrefu? Ni hali ya mashindano, pale mmoja anapoona mwenzake ana wafuasi (more…)

2254; Wakati Sahihi Wa Kuvuka Daraja…

By | March 3, 2021

Ipo kauli ya kihenga inayosema kwamba tunavuka daraja pale tunapolifikia. Ni kauli fupi lakini yenye ujumbe mkubwa mno kuhusu maisha. Mara nyingi huwa tunahangaika na mambo ambayo siyo tu hayapo karibu, bali pia hatuna cha kufanya kuhusu mambo hayo kwa wakati tunasumbuka nayo. Chukua mfano wa ujenzi, kama unajenga nyumba (more…)

2253; Rasilimali Ulizonazo Zinatosha Kufanya Makubwa…

By | March 2, 2021

Wakati taifa la Marekani linapeleka mtu kwa mara ya kwanza mwezini, hawakuwa na kompyuta yenye uwezo kama simu unayotumia sasa. Vitabu bora kabisa tunavyosoma mpaka leo, viliandikwa zaidi ya miaka elfu mbili iliyopita, wakati bado watu wanaandika kwenye mawe na magome ya miti. Viongozi bora kabisa walioendesha mataifa na taasisi (more…)

2252; Kama Huwezi Kuamua, Hujui Unachosimamia…

By | March 1, 2021

Nimewahi kukutana na ujumbe huu mtandaoni ambao ulinifikirisha sana, ujumbe unasema; kama uko njia panda kati ya kunichagua mimi au kumchagua mtu mwingine, usinichague mimi. Huo ni ujumbe mfupi na mzito sana ambao unahitaji muda uweze kuuelewa vizuri. Lakini ujumbe mkubwa uliopo ndani yake ni kwamba kama inabidi umchague mtu (more…)

2251; Vitu Rahisi Kuonekana Kwa Waliofanikiwa…

By | February 28, 2021

Kwa kila aliyefanikiwa, huwa kuna mengi yanasemwa kuhusu wao. Kuna hadithi nyingi watu watakuambia kuhusu waliofanikiwa. Lakini nyingi ni za yale mambo yanayoonekana, ambayo siyo ukweli kamili kuhusu watu hao. Iwe yanayosemwa ni mazuri au mabaya, siyo ukweli kamili. Kuna mengi ambayo waliofanikiwa wanakuwa wamepitia ambayo hakuna anayeweza kuyaona na (more…)