Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2240; Marehemu Alisema…

By | February 17, 2021

Nakumbuka wakati tuko shule ya msingi, kama mwalimu alitoa kazi na hujaifanya, ulikuwa unatafuta kisingizio ili kukwepa adhabu. Kisingizio rahisi ilikuwa ni kuangalia mwanafunzi ambaye hajaja shule siku hiyo na kusema alichukua daftari yako. Watu wasiokuwepo na ambao hawawezi kujitetea, huwa wanasingiziwa vitu vingi mno. Vingi ya hivyo huwa siyo (more…)

2239; Jinsi Ya Kuepuka Gereza Walipo Wengi…

By | February 16, 2021

Gereza kubwa ambalo mtu anakuwa amefungiwa maisha yake yote, huwa amelitengeneza yeye mwenyewe. Gereza hilo huwa linatokana na matarajio ambayo mtu anakuwa nayo kwenye maisha yake. Kinachowafungia watu kwenye gereza hilo ni nguvu kubwa mbili, maumivu na raha. Watu hufanya vitu vinavyowapa raha na kuepuka vitu vinavyowapa maumivu. Jamii nzima (more…)

2238; Kiki, Propaganda Na Wahamisha Mada…

By | February 15, 2021

Mimi huwa siyo msikilizaji wa redio au mfuatiliaji wa habari au mitandao ya kijamii kwa namna yoyote ile. Ila siku za karibuni nimejikuta kwenye mazingira ambayo unakuwa na watu wengine wanaosikiliza redio na hivyo sikuwa na njia ya kukwepa hilo. Nilishangazwa sana na vitu ambavyo vilikuwa vinapewa uzito kwenye karibu (more…)

2237; Mtu Wa Kumtupia Lawama…

By | February 14, 2021

Kwenye kila jamii, huwa kuna mtu au watu ambao hutengwa kwa ajili ya kutupiwa lawama pale mambo yanapokuwa hayaendi vizuri. Hilo halijaanza leo, limekuwepo yangu enzi na enzi, ni watu wakutupiwa lawama ndiyo wamekuwa wanabadilika. Kuna kipindi kuwatafuta wachawi na kuwachoma ilikuwa kitu maarufu, pale jamii ilipopata majanga, wengi waliamini (more…)

2235; Umeamua Kuwakera Watu Gani?

By | February 12, 2021

Kwenye maisha, lazima kuna watu utawakera, hata kama lengo lako ni kumfurahisha kila mtu, bado hutaweza kufanya hivyo. Hivyo chochote unachofanya kwenye maisha, jua kuna watu utawakera, kuna watu watakupinga na kukataa kwa kile unachosimamia. Lengo lako halipaswi kuwa kutokuwakera watu au kukubaliwa na kila mtu, hilo haliwezekani. Lengo lako (more…)

2234; Kuficha Hakusaidii…

By | February 11, 2021

Watu huwa wanapenda kuficha matatizo, ili wengine wasiyajue au kuyaona, kwa kudhani wanawalinda kwa kufanya hivyo. Lakini watu siyo wajinga, wanakuwa wanajua pale mambo yanapokuwa hayaendi sawa, hivyo kuwaficha ni kujidanganya mwenyewe. Watu watakuheshimu zaidi kama utakuwa muwazi, mkweli, mwaminifu na unayeshirikisha mkakati wa kutatua tatizo lililotokea. Watakuwa tayari kukuunga (more…)

2233; Hofu Ya Kifo Ni Ukomo Kwenye Maisha….

By | February 10, 2021

Kitu pekee ambaa uhakika nacho kwenye maisha ni kwamba kila mmoja wetu atakufa, itakuwa lini hiyo ndiyo siri ambayo siyo rahisi mtu kung’amua. Sasa kwa kuwa hatujui hilo litatokea lini, wengi wamekuwa wanaishi kwa hofu kubwa, kitu ambacho kinakuwa ukomo kwao kuyaishi maisha yao kwa ukamilifu wake. Kwa kuhofia kifo, (more…)

2232; Mahali Pa Kupumzisha Akili Yako…

By | February 9, 2021

Akili yako inahitaji kupata mapumziko, hasa baada ya kufanya kazi nzito za kujifunza, kufikiri na kufanya maamuzi. Lakini haitapata mapumziko hayo kwa kutumia vilevi, hivyo huchosha zaidi mwili na akili. Pia akili haitapata mapumziko kwa kuangalia tv au kuperuzi mitandao ya kijamii, huko utaisisimua zaidi akili na kuichosha. Kadhalika akili (more…)

2231; Kusudi La Kufanya Kitu…

By | February 8, 2021

Huwa tunajenga tabia, halafu tabia zinatujenga. Tunapoanza kufanya kitu mara ya kwanza huwa ni kigumu, baadaye tukishazoea huwa tunajikuta tunafanya bila ya ugumu kabisa. Kwenye siku yako, zaidi ya asilimia 60 ya vitu unavifanya bila ya kufikiri kabisa, unavifanya kwa mazoea kiasi kwamba unajikuta umeshafanya bila hata ya kujua. Hivyo (more…)