Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2250; Yasiyoonekana Ambayo Huyapi Uzito…

By | February 27, 2021

Rasilimali zote muhimu huwa zina uhaba au ukomo, hivyo zinapotumika eneo moja, haziwezi kutumika tena eneo jingine. Rasilimali hizo zinaweza kuonekana kufanya vizuri kwa matumizi fulani, lakini zingetumiwa kwa namna nyingine zingefanya kilicho bora zaidi. Unapoona kizuri na kukifurahia, unakuwa hujaona kilicho bora zaidi na hivyo hukipi uzito. Chukua mfano (more…)

2249; Njia Rahisi Ya Kukuza Ufanisi Na Uzalishaji Wako…

By | February 26, 2021

Zama tunazoishi sasa ni zama za mvurugano, ni vigumu mno kupata utulivu wa kufanya jambo lolote lile unalopanga kufanya. Tunazungukwa na usumbufu mwingi ambao unaingilia mengi tunayopanga kufanya, kitu kinachoathiri ufanisi na uzalishaji wetu. Unaweza kuhangaika kupangilia mambo yako mengi, lakini kwa usumbufu unakuzunguka usiweze kuyafanya mambo hayo. Wengi wamekuwa (more…)

2247; Uchaguzi Wa Pili Muhimu Kwenye Maisha Yako…

By | February 24, 2021

Nilishakuambia uchaguzi wa kwanza muhimu kabisa kwenye maisha yako ni kujichagua wewe mwenyewe. Kujipigia kura wewe kama kiongozi mkuu wa maisha yako, mtu pekee wa kukutoa hapo ulipo sasa na kukufikisha kule unakotaka kufika. Naamini hilo ulilielewa vizuri, ilishajichagua na sasa unaweka juhudi kufika unakotaka kufika. Kuna uchaguzi wa pili (more…)

2246; Mhimili Usioyumbishwa…

By | February 23, 2021

James Altucher, mwandishi na mwekezaji wa nchini Marekani amekuwa akiandika kuhusu makosa mbalimbali aliyofanya kwenye maisha yake na yakapelekea apate matokeo mabovu pamoja na kuingia kwenye matatizo makubwa. Amekuwa akieleza kwamba ameshaanzisha biashara 20, 18 kati ya hizo zikashindwa kabisa. Anaeleza amewahi kuuza kampuni yake na kuwa milionea, lakini miaka (more…)

2245; Kutatua Matatizo Makubwa…

By | February 22, 2021

Kwanza ni lazima uwe na mtazamo mkubwa kuliko tatizo lenyewe, lazima ufikiri kwa ukubwa kiasi kwamba tatizo linaonekana ni dogo. Kwa sababu usipofanya hivyo, tatizo litaonekana ni kubwa kuliko uwezo wako. Pili inabidi ujitofautishe na tatizo hilo, uweze kuliona kama vile mtu mwingine anavyoweza kuliona, uache kujishikiza nalo kihisia. Hisia (more…)

2242; Vipi Kama Wewe Ndiye Unayekosea?

By | February 19, 2021

Wakati bado nafanya kazi ya kufundisha shule ya sekondari, siku moja tukiwa ofisini na mwalimu mwingine aliyekuwa anasahihisha kazi za wanafunzi alilalamika kuhusu wanafunzi kukosa swali moja kwa majibu yanayofanana. Nikamwambia kwa utani, kama wanafunzi wote wamekosa swali hilo na majibu yao yanafanana, huenda wewe ndiye uliyekosea kwenye jibu lako. (more…)

2241; Sababu Tano Za Biashara Kushindwa…

By | February 18, 2021

Biashara zote zinazoshindwa, huwa zinakuwa zimepitia moja au baadhi ya sababu hizi tano. Moja ni kutokujulikana, wateja hawajui kama biashara ipo na hivyo hawaji kununua. Hapa tatizo ni masoko hayafanyiki kwa uhakika, hivyo biashara inakuwa na bidhaa au huduma nzuri, lakini wanaolengwa hawajui kama ipo. Dawa ya hii ni kuwa (more…)