Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2230; Usijishikize Na Matokeo, Jishikize Na Kusudi…

By | February 7, 2021

Chanzo cha wengi kuanguka na kukata tamaa ni kushikiza utu wao kwenye matokeo waliyopata au wanayotaka kuyapata. Lakini matokeo huwa yako nje ya uwezo wa mtu kuyadhibiti na kuyaathiri. Hivyo mambo huwa hayaendi kama mtu anavyotegemea na hapo ndipo kuanguka na kukata tamaa kunapotokea. Mahali sahihi pa kushikiza utu wako (more…)

2229; Usijichukulie Poa…

By | February 6, 2021

Usiwe na mashaka juu yako, maana palipo na mashaka hapawezi kuwa na kujiamini. Haijalishi unayokabiliana nayo ni magumu kiasi gani, jiamini na jua una uwezo wa kuyashinda. Kujiamini ni nusu ya kuweza kufanya chochote. Usipojiamini, hata kitu kidogo kitakushinda. Usijidharau, maana utawapa wengine nafasi ya kufanya hivyo na utashindwa kujisimamia (more…)

2228; Kumeza Na Kufyonza…

By | February 5, 2021

Kusoma kunafanana kabisa na kula, kama unavyoupa mwili virutubisho kupitia chakula, ndivyo unavyoipa akili virutubisho muhimu kupitia usomaji. Unajua kwenye ulaji unakula chakula kingi, kinameng’enywa na kisha sehemu kidogo ya chakula hicho inafyonzwa mwilini na kutumika kwenye kuujenga mwili. Sehemu kubwa inayobakia unaitoa kama uchafu kupitia kinyesi. Kwenye usomaji, unaweza (more…)

2227; Wanaojua Kila Kitu…

By | February 4, 2021

Wanaojua sana huwa hawaongei na wanaoongea sana huwa hawajui, hii ni kauli iliyotolewa miaka mingi iliyopita na mwanafalsafa wa China aliyeitwa Lao Tzu. Ungeweza kufikiri watu wangekuwa wamejifunza kuhusu hilo, lakini ni udhaifu wetu binadamu, tunajikuta tukiongea sana pale ambapo hatujui na kuwaamini wale wanaoongea sana. Na hapa swala siyo (more…)

2226; Maisha Yanayogusa Maisha Mengine…

By | February 3, 2021

Mshumaa unapowashwa kwenye chumba chenye giza, huwa unatoa nuru kwenye chumba kizima. Mshumaa huo hautaisha haraka iwapo utawekwa kwenye chumba kikubwa kuliko chumba kidogo. Kadhalika mshumaa huo hautaisha haraka kwa kuwasha mshumaa mwingine. Mawimbi ya bahari yanapoinuka, huwa yanainua kila kilicho kwenye bahari hiyo, hakuna kinachoachwa chini na wimbi linaloinuka. (more…)

2225; Kinga Ni Bora Kuliko Tiba…

By | February 2, 2021

Ni usemi ambao kila mtu anaujua, lakini kama tunavyojua, kujua na kufanya ni vitu viwili tofauti kabisa. Tunajua mengi, lakini hatuyafanyii kazi na hivyo hatunufaiki na yale tunayojua. Wakati mwingine tunasahau kama tunayojua tunapaswa kuyatumia. Tukirudi kwenye kinga ni bora kuliko tiba, kuzuia matatizo ni rahisi kuliko kuyatatua yakishatokea. Huwa (more…)

2224; Kazi Yako Ni Kazi Yako…

By | February 1, 2021

Kazi yako siyo kutetea kile unachokifanya, Kazi yako siyo kumridhisha na kumfurahisha kila mtu, Kazi yako siyo kutaka uonekane kwa unachofanya, Bali kazi yako ni kufanya kazi yako, kwa namna ambayo inaongeza thamani kubwa kwa wengine na kukuingizia wewe kipato cha kuendesha maisha yako kwa namna inayokuweka huru. Inashangaza jinsi (more…)

2223; Kura Yako Unapeleka Wapi?

By | January 31, 2021

Tukisikia mambo ya kura, fikra zetu zinakwenda moja kwa moja kwenye uchaguzi wa kisiasa au wa aina nyingine. Tunajua kwenye chaguzi hizo, wagombea wanakuja kujinadi kwetu, wakitupa sera zao na kutuambia kwa nini tuwachague. Kisha tunaangalia na kuona mgombea yupi sahihi na kumpa kura yetu. Kitu ambacho huelewi ni kwamba, (more…)

2221; Kuwa Makini Na Motisha Unaotoa…

By | January 29, 2021

Serikali ya India ilikuwa na tatizo la nyoka, nyoka walikuwa wengi kiasi cha kuhatarisha usalama wa watu. Njia mbalimbali za kuwatokomeza hazikufanikiwa. Mwisho wakajaribu njia ya kuwashirikisha wananchi, ambapo mtu aliyepeleka nyoka aliyekufa, alilipwa fedha. Njia hiyo ilifanya kazi, kwani kwa kipindi kifupi nyoka walipungua sana. Lakini cha kushangaza, nyoka (more…)