Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2220; Chagua Jumuia Sahihi Kwako…

By | January 28, 2021

Sisi binadamu ni viumbe wa kijamii, huwa hatuwezi kuwa na utulivu tukiwa peke yetu. Tunapata amani na utulivu tunapojua ni sehemu ya jumuia fulani. Ndiyo maana ni rahisi vijana wanaobalehe kuingia kwenye makundi yenye ushawishi mbaya kwao. Wanakuwa kwenye kipindi cha mabadiliko kwenye maisha yao, ambapo wanataka kuondoka chini ya (more…)

2219; Tatizo La Mawasiliano Ya Mbali…

By | January 27, 2021

Moja ya sababu zinazopelekea mahusiano ya mbali yasidumu, ni urahisi wa maneno kuchukuliwa tofauti na aliyeyasema alivyomaanisha. Moja ya sababu ya watu kutokuelewana na kutukanana mitandaoni, ni urahisi wa alichoandika mtu kuchukuliwa kwa namna tofauti na alivyomaanisha. Watu mnapokuwa ana kwa ana mazungumzo huwa yanaendana na muktadha. Kama mpo kwenye (more…)

2218; Unazalisha Nini?

By | January 26, 2021

Kama huipendi kazi au biashara unayofanya, kama unachofanya kinakupa msongo na huna hamasa ya kufanya kwa ukubwa zaidi, tatizo linaweza kuwa huzalishi matokeo ya kutosha au huoni athari ya matokeo unayozalisha. Ukitatua hayo mawili, kwa kuanza na unachozalisha na kisha ukafuatilia athari za unachozalisha, utapenda kile unachofanya na kuhamasika kufanya (more…)

2217; Kinapopatikana Unachotafuta…

By | January 25, 2021

Kile unachotafuta sana kwenye maisha yako, kinapatikana pale penye watu wachache wanaokitafuta pia. Na sehemu pekee yenye watu wachache, ni ile ambayo siyo rahisi, ambayo inahitaji kazi na uvumilivu kupata unachotaka. Kama tunavyojua, watu wanapenda urahisi na njia ya mkato kupata wanachotaka, hivyo hawapo tayari kuweka kazi na kujipa muda. (more…)

2216; Wewe Siyo Mtakatifu Au Mjuaji Sana…

By | January 24, 2021

Pope Alexander aliwahi kunukuliwa akisema maarifa kidogo ni hatari kwa yule anayeyapata hivyo mtu anapaswa kuyanywa kwa kina maji ya chemchem ya maarifa au asiyaonje kabisa. Wengi wamekuwa hawaelewi nukuu hiyo na ndiyo maana wanarudia makosa ambayo yamekuwa yakifanyika kwa miaka mingi. Mara zote wale wanaojua kitu juu juu huwa (more…)

2215; Vitu Vipya Na Vizuri…

By | January 23, 2021

Hii ndiyo njia ambayo dunia imekuwa inatumia kuwahadaa watu wasifanikiwe. Kila unapopanga na kuamua kuweka umakini wako kwenye yale muhimu zaidi kwako, hapo hapo dunia inakuja na kitu kipya na kinachoonekana kizuri, ambacho unaona hupaswi kupitwa. Unaacha ulichopanga na kuhangaika na kitu hicho kipya, baadaye unakuja kugundua haikuwa sahihi kwako. (more…)

2214; Usiwazuie Kushindwa…

By | January 22, 2021

Wazazi ambao walipitia magumu wakati wa utoto wao, hupambana ili watoto wao wasipitie magumu kama waliyopitia wao. Wanafanya hivyo kwa nia njema, lakini kama tulivyoona kwenye ukurasa wa jana, nia njema huja kuzalisha matokeo yasiyo mazuri. Katika kumzuia mtoto asipitie magumu, mzazi anaondoa kabisa kila nafasi ya kushindwa na hivyo (more…)

2213; Nia Njema Inapoleta Matokeo Mabaya…

By | January 21, 2021

Kila uovu huwa unaanza kwa nia njema, lakini kwa sababu ya udhaifu wetu binadamu, huwa hatujui wakati gani nia njema inakuwa na madhara, tunaendelea kufanya tunachoamini ni sahihi wakati siyo sahihi. Ndiyo maana katiba na sheria zimewekwa, ili kuhakikisha hata kama mtu ana nia njema kiasi gani, udhaifu wake binafsi (more…)

2212; Hayo Mashindano Yanakufikisha Wapi…

By | January 20, 2021

Kwa asili binadamu huwa tunapenda kushindana, mweleze mtu matatizo yako naye atakuambia hayo yako si kitu, atakueleza matatizo yake ambayo ni makubwa zaidi. Unaweza kuwa unaendesha gari barabarani na mbele yako kuna mtu mwingine anaendesha taratibu tu, anaonekana kutokuwa na haraka. Unaamua umpite kwa sababu una haraka na kile kitendo (more…)

2211; Safisha Akili Yako…

By | January 19, 2021

Wasiwasi huwa ni zao la msongamano wa mawazo na fikra kwenye akili yako. Akili inakosa nafasi ya kutosha kwa yale yaliyo muhimu. Ni kama ilivyo kwenye chumba au ofisi ambayo haijapangiliwa vizuri, ukitaka kutafuta kitu, inakuchukua muda mrefu mpaka ukipate. Muda mwingi unaishia kwenye kupangua vitu visivyo na matumizi na (more…)