Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2640; Kiranja mkuu wa dunia.

By | March 24, 2022

2640; Kiranja mkuu wa dunia. Ni cheo ambacho wengi wanakitaka, lakini hawawezi kukipata. Kwa sababu cheo hicho hakipo. Huwa tunapenda sana dunia iende vile tunavyotaka sisi. Lakini hilo haliwezekani, halipo kabisa ndani ya uwezo wetu. Tunataka kuwabadili watu, wawe na kufanya vile tunavyotaka sisi. Lakini hilo haliwezekani, hata uwe na (more…)

2639; Kama watu wangesimamia maneno yao.

By | March 23, 2022

2639; Kama watu wangesimamia maneno yao. Leo hii ungekuwa mbali sana. Hebu fikiria kama watu wote waliokuahidi watanunua unachouza, kama kweli wangenunua kama walivyoahidi si ungekuwa mbali sana? Hebu kumbuka wote waliokuambia wapo pamoja na wewe na watapambana kufa na kupona wakiwa upande wako. Kama wangefanya hivyo leo si ungekuwa (more…)

2638; Ni kujenga, siyo kuota.

By | March 22, 2022

2638; Ni kujenga, siyo kuota. Mafanikio huwa yanaanza na ndoto, mtu kuwa na picha ya kile unachotaka, ambacho kwa sasa huna. Lakini ili kufikia ndoto hiyo, ni lazima ujenge. Ndoto haitafikiwa tu kwa kuota, Bali itafikiwa kwa kujenga. Hatua unazochukua katika kuifikia ndoto ndizo zinaifanya ndoto hiyo kuwa uhalisia. Thamani (more…)

2637; Sahihi na siyo sahihi.

By | March 21, 2022

2637; Sahihi na siyo sahihi. Mtu mmoja amewahi kunukuliwa akisema kipimo cha akili iliyokomaa ni kuweza kushikilia kwenye akili mawazo mawili yanayopingana kwa wakati mmoja. Hili ni zoezi gumu mno kwa sababu kwa kawaida binadamu huwa tunapenda sana uhakika. Kukaa na mawazo mawili yanayopingana ni kukosa uhakika. Wengi huona ni (more…)

2634; Lakini unakosea.

By | March 18, 2022

2634; Lakini unakosea. Hayo ni maneno utakayoyasikia maisha yako yote, mpaka siku unayoondoka hapa duniani. Kwa maamuzi yoyote utakayofanya na chochote utakachofanya, kuna watu watakuambia unakosea. Sema unataka fedha na hicho ndiyo kipaumbele chako cha kwanza na kuna watu watakuambia unakosea, una tamaa sana ya fedha na fedha siyo kila (more…)

2633; Kafanyaje huyu?

By | March 17, 2022

2633; Kafanyaje huyu? Kuna picha ya kichekesho (meme) inayozunguka sana kwenye mitandao. Kwenye picha hiyo mtu anayeonekana kuzimia amebebwa kwenye machela na watu wawili. Mmoja anauliza mtu huyo aliyebebwa amefanya nini? Mwingine anajibu kitu alichofanya mtu huyo na kupata matokeo ambayo hakutegemea. Watu na taasisi mbalimbali wamebadili maelezo ya mtu (more…)

2632; Unachojali zaidi.

By | March 16, 2022

2632; Unachojali zaidi. Kila unachokijali zaidi kwenye maisha yako ndiyo kinapata kipaumbele kikubwa kwako. Hicho kitakuwa na nguvu ya kukusukuma ufanye au usifanye mambo muhimu unayopaswa kufanya. Chukua mfano unataka kupata fedha ili kufikia uhuru wa kifedha, lakini pia unataka kila mtu akupende. Kitendo cha kujali kuhusu kupendwa na kila (more…)

2631; Kujieleza na kujitetea.

By | March 15, 2022

2631; Kujieleza na kujitetea. Ukweli huwa unabaki kuwa ukweli, uwe unatetewa au hautetewi. Wakati mwingine ukijaribu sana kuutetea ukweli, unaanza kuonekana kama uongo. Uongo ndiyo unahitaji maelezo mengi na kutetewa ili ukubalike na wengine. Na uongo huwa unahitaji uongo mwingine mkubwa zaidi ili usianguke. Mara zote jua upo upande upi, (more…)