Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2569; Kuadhibiwa na unachokitaka.

By | January 12, 2022

2569; Kuadhibiwa na unachokitaka. Werevu wamewahi kusema ukitaka kumwadhibu mtu, mpe kile anachokitaka, tena kwa namna anavyokitaka. Ni kauli ambayo wengi huwa hawaielewi, ila twende kwenye mifano tuweze kujionea uhalisia wake. Chukua mtu anayecheza bahati nasibu, wote tunajua anataka ushindi. Sasa chukua mtu aliyeshinda bahati nasibu, baada ya muda maisha (more…)

2568; Uhakika upo kwenye mchakato.

By | January 11, 2022

2568; Uhakika upo kwenye mchakato. Ukienda kununua baadhi ya vifaa, mfano simu, tv, redio n.k, huwa unapewa uhakika. Kwamba kifaa hicho kitafanya kazi vizuri na kama kitakuwa na shida basi unaweza kukirudisha na kupewa kingine. Hii ni njia ya masoko ambayo imekuwa na nguvu kwa sababu binadamu tunapenda sana uhakika. (more…)

2567; Kwa sababu wengine wanafanya.

By | January 10, 2022

2567; Kwa sababu wengine wanafanya. Sisi binadamu tunashawishiwa sana na binadamu wengine kuliko kitu kingine chochote. Ni rahisi sana kufanya kile ambacho wengine wanafanya, hata kama umejiambia hutafanya. Mambo yote, mazuri na mabaya huwa yanafanyika kwa sababu hiyo. Pale mtu anapoona wengine wanafanya, basi anaona siyo vibaya na yeye akifanya. (more…)

2566; Vichache na vingi.

By | January 9, 2022

2566; Vichache na vingi. Kwenye zama tunazoishi sasa, kuna mambo mengi sana ya kufanya. Na unaweza kufanya karibu kila kitu. Hebu angalia tu biashara zinazofanyika kwenye eneo ulilopo, karibu zote unaweza kuzifanya. Na wakati mwingine unajiambia kabisa, yaani hawa wanaweza hivi, hata mimi siwezi kushindwa. Hilo linaweza kukushawishi uhangaike na (more…)

2565; Ni juhudi zipi ambazo umeweka?

By | January 8, 2022

2565; Ni juhudi zipi ambazo umeweka? Kuna kitu unachotaka, lakini vikwazo na changamoto zinakuzuia usipate kitu hicho. Ni rahisi kutumia hiyo kama sababu ya kukosa unachotaka, na kujifariji kwamba hakuna namna. Kabla hujaendelea kujifariji, nikukumbushe kitu kimoja muhimu, hakuna aliyefanya makubwa ambaye hakukutana na vikwazo na changamoto. Kwa hakika, pale (more…)

2563; Warahisishie.

By | January 6, 2022

2563; Warahisishie. Jukumu kubwa kabisa na ambalo kila mmoja wetu analo kwenye kazi au biashara anayofanya ni kuwarahisishia wale ambao anawalenga. Kwa wale ambao kazi au biashara yako inawalenga, wanachotafuta ni urahisi zaidi. Kuna matokeo ambayo wanayataka na wanataka kuyapata kwa urahisi. Inaweza kuwa urahisi kwenye bei, urahisi kwenye kutumia (more…)

2562; Kuna kitu hakipo sawa.

By | January 5, 2022

2562; Kuna kitu hakipo sawa. Kwa asili, mtoto akizaliwa anatakiwa aendelee kukua. Nguvu ya ukuaji tayari ipo ndani yake. Kama mtoto hakui vizuri, kuna kitu kinazuia au kuathiri ile nguvu iliyo ndani yake. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye kazi na biashara. Kadiri muda unavyokwenda, kile unachofanya kinapaswa kukua zaidi. Nguvu (more…)