Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2579; Mpaka uelewe.

By | January 22, 2022

2579; Mpaka uelewe. Upo usemi wa Kiswahili kwamba asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Unaweza kupata maana mbalimbali kwenye usemi huo, lakini kuna maana moja nimeona ina nguvu kubwa sana. Iko hivi, mtoto anapokosea, mzazi humwadhibu. Kama mtoto ataendelea kukosea, mzazi hawezi kuendelea kumwadhibu, atafika mahali na kumwonea huruma. Na (more…)

2578; Huhitaji kutumia nguvy nyingi.

By | January 21, 2022

2578; Huhitaji kutumia nguvy nyingi. Kupumua ni kitu ambacho huwa hakihitaji nguvu kubwa. Unapojikuta ukitumia nguvu kubwa kupumua, hapo unajua wazi kwamba kuna shida kwenye mfumo wa upumuaji. Kadhalika kwenye kula na mengine yanayoendelea kwenye mwili. Huwa yanakwenda yenyewe kwa urahisi kabisa bila kuhitaji nguvu zako kubwa. Hivyo pia ndivyo (more…)

2576; Marudio.

By | January 19, 2022

2576; Marudio. Kama hujawahi kuelewa hili basi nikusisitize tena, kila kitu kwenye maisha kinategemea sana marudio. Hebu fikiria siku moja moyo wako ungesema umechoka kudunda na hivyo inabidi upumzike kwa siku chache. Ni hakika hakutakuwa na maisha. Kula, kupumua, kujifunza na hata kuchukua hatua ili ufanikiwe, inahitaji marudio yasiyo na (more…)

2575; Mabadiliko makubwa hayaletwi na wengi.

By | January 18, 2022

2575; Mabadiliko makubwa hayaletwi na wengi. Mabadiliko makubwa kabisa hayajawahi kuletwa na watu wengi. Bali huwa ni matokeo ya watu wachache waliojitoa kweli ili kuhakikisha wanakamilisha wanachotaka. Ni vigumu sana kwa watu walio wengi kuweza kukitoa kwa muda mrefu bila kuchoka. Kundi la watu wengi huwa ni rahisi kupotea kwa (more…)

2573; Hakuna kisicho na manufaa.

By | January 16, 2022

2573; Hakuna kisicho na manufaa. Kwenye maisha yetu, huwa tunapitia mambo mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Baadhi ya mambo hayo yapo ndani ya uwezo wetu, huku mengi yakiwa nje ya uwezo wetu. Kwa tafsiri zetu wenyewe, kuna baadhi ya mambo tunasema ni mazuri huku mambo mengine tukisema ni mabaya. Kama yanaendana (more…)

2572; Kipi kingine unachojali zaidi?

By | January 15, 2022

2572; Kipi kingine unachojali zaidi? Kile unachokijali zaidi, ndiyo unachokipa umakini wako na hicho ndiyo kinachokua zaidi. Kama una ndoto kubwa ambazo ndiyo unazijali zaidi, fikra zako zote zinakuwa kwenye ndoto hizo na mengine yote unayapuuza. Kila wakati unakuwa unapambana na namna ya kufikia ndoto ulizonazo na hicho tu ndiyo (more…)

2571; Machache kabla ya mengi.

By | January 14, 2022

2571; Machache kabla ya mengi. Mawazo unayoweza kuyafanyia kazi ni mengi. Fursa unazoweza kunufaika nazo ni chungu mzima. Lakini kuna ukomo wa rasilimali muhimu kama muda, nguvu na fedha. Ukomo huo unakutaka uweke vizuri vipaumbele vyako ili uweze kuzitumia rasilimali hizo vizuri. Lakini wengi wamekuwa wanashindwa na hilo, wanashindwa kuweka (more…)