Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2510; Kwa nini hubadiliki?

By | November 14, 2021

2510; Kwa nini hubadiliki? Kuna nukuu moja maarufu sana inayosema; miaka mitano ijayo utakuwa mtu yule yule uliye sasa isipokuwa kwa watu utakaokutana nao na vitabu utakavyosoma. Ni kauli rahisi lakini yenye funzo na maana kubwa sana. Kwamba mafanikio yetu kwenye maisha yanatokana na mabadiliko yanayotokea kwenye maisha yetu. Mabadiliko (more…)

2509; Kwa nini hupendi unachofanya?

By | November 13, 2021

2509; Kwa nini hupendi unachofanya? Kutokupenda kazi au biashara unayofanya ni kikwazo kikubwa cha mafanikio yako. Huwezi kufanikiwa kwenye kitu ambacho hukipendi, hata kama kinalipa kiasi gani. Huenda wewe ni mmoja wa wale ambao wanafanya wasichopenda, leo nataka upate jawabu hapa ili kuchukua hatua sahihi. Mahali pa kuanzia ni kujua (more…)

2508; Kama Huna Cha Kufanya, Usifanye Chochote.

By | November 12, 2021

2508; Kama Huna Cha Kufanya, Usifanye Chochote. Kuna mambo mawili makubwa yanaendelea kwenye zama tunazoishi sasa. Moja ni kila mtu amechoka kweli kweli, haijalishi amezalisha matokeo gani. Mbili ni ubunifu na uvumbuzi umepungua sana. Yote hayo yanasababishwa na tabia ya watu kukosa muda ambao hawana kitu cha kufanya. Kwenye zama (more…)

2507; Siyo wa tofauti kama unavyodhani.

By | November 11, 2021

2507; Siyo wa tofauti kama unavyodhani. Kuna vitu ambavyo huwa vinawatokea watu wengi kwenye maisha yao kutokana na yale wanayofanya au vile walivyo. Yaani wanachopata ni matokeo ya hatua walizochukua au namna walivyo. Inakuwa imezoeleka hivyo kiasi kwamba ukimwona tu mtu anafanya kitu fulani au yulo kwa namna fulani, unajua (more…)

2506; Kitakachokutoa Njia Panda.

By | November 10, 2021

2506; Kitakachokutoa Njia Panda. Mara kwa mara huwa tunajikuta kwenye njia panda fulani katika safari yetu ya maisha. Kutokana na mambo mbalimbali yanayokuwa yanaendelea, unakuwa hujui nini hasa ufanye kati ya mengi yaliyo mbele yako. Ni katika hali hizi za njia panda ndipo wanaofanikiwa na wanaoshindwa hutofautiana. Wanaofanikiwa huwa wana (more…)

2505; Siyo Pata Potea.

By | November 9, 2021

2505; Siyo Pata Potea. Kikwazo kikubwa cha watu kwenye mafanikio ni mtazamo wanaokuwa nao. Ndiyo maana unaweza kukuta watu wawili, wanafanya kazi au biashara ya aina moja, mmoja anafanikiwa sana na mwingine anashindwa. Kinachowatofautisha watu hao ni mtazamo. Kuna mitazamo mingi ambayo imekuwa kikwazo kwa wengi kufanikiwa. Lakini mmoja mkubwa (more…)

2504; Jenga Mahusiano Zaidi.

By | November 8, 2021

2504; Jenga Mahusiano Zaidi. Huwa kuna kauli kwamba haijalishi unajua nini, bali unamjua nani. Sehemu kubwa ya mafanikio yako inatokana na wale unaowajua kuliko yale unayoyajua. Hii ni kusema kwamba mahusiano yako na watu sahihi ni muhimu sana kwenye mafanikio yako. Kwa sababu kama unavyojua, kila unachokihitaji tayari kipo kwa (more…)

2503; Kukusanya Na Kutawanya.

By | November 7, 2021

2503; Kukusanya Na Kutawanya. Mwanga wa jua ukitawanywa unatoa tu mwangaza wa kawaida. Lakini mwanga huo huo ukikusanywa eneo moja, unatoa moto mkali wenye kuweza kuunguza chochote. Nguvu na umakini wako ukivitawanya unaishia kupata matokeo ya kawaida. Lakini ukikusanya vitu hivyo viwili kwenye maeneo machache, unazalisha matokeo makubwa sana. Kama (more…)

2502; Hiyo Pesa Itafute Hapo Ulipo Kwanza.

By | November 6, 2021

2502; Hiyo Pesa Itafute Hapo Ulipo Kwanza. Fursa mpya zimekuwa haziishi na zinashawishi kweli kweli. Maana ni vigumu sana kuikataa pesa wakati una uhitaji mkubwa wa fedha. Hivyo zinapokuja fursa mpya, ambazo tunakua kabisa kwamba haziendani na kile tunachofanya, tukishaona kuna fedha tunaweza kupata, basi tunakimbilia kuifanya. Mwisho wake kinachotokea (more…)

2501; Kama nafsi inakataa, isikilize.

By | November 5, 2021

2501; Kama nafsi inakataa, isikilize. Kuna wakati unaweza kuwa na fursa fulani mbele yako, fursa ambayo inaonekana ni nzuri kabisa, lakini nafsi yako inakataa kabisa kuikubali fursa hiyo. Mara nyingi hili hutokes pale unapohitaji kujihusisha na watu fulani. Labda ni kwenye kazi au biashara. Kwa nje wanaonekana ni watu wazuri (more…)