Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2500; Wewe Ndiye Mfano.

By | November 4, 2021

2500; Wewe Ndiye Mfano. Kama kuna watu wako chini yako na wanafanya vitu ambavyo huridhiki navyo, kuna mtu mmoja tu wa kumlaumu, wewe mwenyewe. Ni rahisi kuwaona watu wanakuwa mzigo na kukukwamisha. Lakini ukweli ni wao wanaiga mfano wako. Wale walio chini yako, wanaangalia zaidi kile unachofanya kuliko unachosema. Wataiga (more…)

2499; Ujuaji Mwingi.

By | November 3, 2021

2499; Ujuaji Mwingi. Nikiwa shule ya sekondari, nilikuwa na biashara ya kupiga picha pale shuleni. Siku moja walimu wakanitaka niwapige picha. Wakati wanajipanga ili niwapige picha, mwalimu mmoja akasema angalia hiyo picha isiye ikaungua (enzi hizo tunatumia kamera za analojia). Nilimjibu yule mwalimu mimi ni mzoefu kwenye hili zoezi la (more…)

2498; Jenga Mtaji Wa Biashara.

By | November 2, 2021

2498; Jenga Mtaji Wa Biashara. Kuna changamoto moja kubwa ambayo naiona kwa watu wengi walio kwenye biashara ndogo, hasa za huduma. Watu hawa wamekuwa wanaendesha biashara zao bila ya kuwa na mtaji. Wanasubiri wateja wawalipe na kisha kutumia kile wanacholipwa na wateja. Halafu wanasubiri tena kupata wateja au kukipwa tena (more…)

2497; Muda, Nguvu, Umakini.

By | November 1, 2021

2497; Muda, Nguvu, Umakini. Rasilimali kubwa tatu unazopaswa kuzitunza na kuzitumia vizuri kama unayataka mafanikio makubwa. Tumezoea kuona msisitizo ukiwekwa sana kwenye muda, jinsi ya kudhibiti na kutumia muda vizuri ili kuweza kufanya makubwa. Lakini siyo muda pekee ambao ndiyo rasilimali yenye uhaba na muhimu kwa mafanikio yako. Kuna nguvu (more…)

2496; Unachokosa siyo unachodhani.

By | October 31, 2021

2496; Unachokosa siyo unachodhani. Ni rahisi kuona hujapiga hatua kwenye maisha kwa sababu kuna vitu umekosa. Lakini kwa sehemu kubwa unachokosa siyo kile unachodhani. Unachodhani unakosa ni kikubwa na kilicho nje ya uwezo wako. Lakini unachokosa kwa uhalisia ni kidogo na kipo ndani ya uwezo wako. Hujakosa kipaji, bali unachokosa (more…)

2495; Unajua cha kufanya.

By | October 30, 2021

2495; Unajua cha kufanya. Wakati naanza huduma ya ushauri na ukocha, nilidhani watu hawafanikiwi kwa sababu hawajui cha kufanya. Hivyo nilikuwa na haraka sana ya kuwaambia nini wanapaswa kufanya, hasa wanapokuwa kwenye changamoto mbalimbali. Lakini kadiri ambavyo nimeendelea kufanya huduma hii, nimegundua kitu kimoja kikubwa sana. Watu hawafanikiwi siyo kwa (more…)

2494; Kuna neno hajasikia.

By | October 29, 2021

2494; Kuna neno hajasikia. Nikiwa kwenye sherehe fulani, mshereheshaji alikuwa anatumia njia mbalimbali kuwashawishi watu kutoka kwenye viti na kwenda kucheza muziki. Kwanza alianza kwa kutumia kigezo cha kupendeza, akisema wote mmependeza sana, na kwa kupendeza huko mje kucheza. Akaona siyo wengi wanaotoka kucheza, akasema wale ambao hawatoki hawajapendeza. Bado (more…)

2493; Unapoteza Ulichonacho.

By | October 28, 2021

2493; Unapoteza Ulichonacho. Changamoto nyingi kubwa kwenye maisha majibu yake huwa ni rahisi kabisa. Lakini tumekuwa hatukubali wala kufanyia kazi majibu hayo kwa sababu ya urahisi wake, tunaona hayawezi kuwa sahihi. Ni majibu hayo rahisi tunayoyapuuza kwenye maisha ndiyo yamekuwa kikwazo kikubwa kwetu kupiga hatua kubwa. Leo tuangalie mfano wa (more…)

2492; Kidogo kidogo halafu ghafla.

By | October 27, 2021

2492; Kidogo kidogo halafu ghafla. Mambo yote kwenye maisha huwa yanaanza kidogo kidogo kisha baadaye yanatokea ghafla. Lakini mara nyingi watu huwa hawaoni yanapotokea kidogo kidogo na kuchukua hatua sahihi, wanakuja kushtuka wakati yametokea ghafla na hawawezi tena kuchukua hatua kwa haraka. Hakuna mtu anaamka siku moja na kujikuta kwenye (more…)

2491; Hawabadiliki, wanachoka kuigiza.

By | October 26, 2021

2491; Hawabadiliki, wanachoka kuigiza. Watu huwa hawabadiliki, bali wanachoka kuigiza. Angalau siyo kwa haraka kiasi hicho, yaani hata kama watu watabadilika, haiwi haraka na rahisi. Hivyo unapojiambia mtu amebadilika, kuwa makini, mara nyingi anakuwa amechoka kuigiza na kuamua kuishi uhalisia wake. Kwamba mtu alikuwa mwaminifu na ghafla amekuwa siyo mwaminifu (more…)