Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2360; Unakokimbilia Ni Wapi?

By | June 17, 2021

2360; Unakokimbilia Ni Wapi? Ni rahisi kujikuta ukiharakisha mambo unayoyafanya, lakini umewahi kujiuliza unakokimbilia ni wapi? Hebu fikiria mtu anayeharakisha kufanya kazi yake, anashindwa hata kuifanya kwa umakini, halafu anakokimbilia ni kwenda kubishana. Au fikiria mtu anayeharakisha kumhudumia mteja kwenye biashara, anaharakisha mteja aondoke, ili tu aingie kwenye mitandao na (more…)

2359; Jipe Zawadi Ya Umakini…

By | June 16, 2021

2359; Jipe Zawadi Ya Umakini… Kama kuna zawadi bora kabisa unayoweza kujipa kwenye maisha yako, ni kuweka umakini wako wote kwenye kile unachofanya. Kadiri unavyoweka umakini wako kwenye kile unachofanya, ndivyo unavyoweza kukifanya kwa ubora wa hali ya juu sana. Na kama hiyo haitoshi, inakupunguzia kuhofia mambo yasiyo na umuhimu (more…)

2358; Fanya kwa ubora au usifanye kabisa…

By | June 15, 2021

2358; Fanya kwa ubora au usifanye kabisa… Una nafasi moja tu ya kuishi. Kila siku inayoisha ni siku unayoipunguza kwenye maisha yako, hutaweza kuipata tena. Kwa ukomo huo mkubwa ulionao, unapaswa kuwa makini sana na matumizi ya siku zako. Chochote unachochagua kufanya, kifanye kwa ubora wa hali ya juu kabisa. (more…)

2357; Jiweke kwenye fikra zao…

By | June 14, 2021

2357; Jiweke kwenye fikra zao… Mtu akikuambia nitakutafuta, usisubiri mpaka akutafute, utakuwa umechagua kumpoteza. Hasa pale wewe ndiye unayekuwa unahitaji zaidi kitu kutoka kwake. Ipo kauli inayosema kisichoonekana huwa kinasahaulika. Kadhalika kwa wale wanaokuambia watakutafuta, ni rahisi kusahau kama hakuna kinachowafanya wakukumbuke. Na hapo ndipo unapaswa kujiweka kwenye fikra zako, (more…)

2356; Usisubiri Yapoe…

By | June 13, 2021

2356; Usisubiri Yapoe… Kitu pekee ambacho nimekuwa nanufaika nacho kwenye maarifa mbalimbali ninayopata ni kujiuliza nawezaje kuyatumia na kisha kuchukua hatua mara moja, kabla hata maarifa hayo hayajapoa. Huduma zote ambazo nimeweza kuanzisha na kuboresha mpaka sasa ni kutokana na utaratibu huu wa kuyatumia maarifa yakiwa ya moto badala ya (more…)

2355; Utapiamlo Wa Akili…

By | June 12, 2021

2355; Utapiamlo Wa Akili… Watu wengi hasa kwenye zama hizi wana utapiamlo wa akili. Kama ilivyo kwamba usipoulisha mwili vizuri unapata utapiamlo wa mwili, ndivyo pia usipoilisha akili vizuri unapata utapiamlo wa akili. Ili kuondokana na utapiamlo wa akili, unapaswa kuilisha akili yako kilicho sahihi. Unapaswa kuwa na dayati maalumu (more…)

2354; Ng’ang’ana na lengo, siyo njia…

By | June 11, 2021

2354; Ng’ang’ana na lengo, siyo njia… Kitu muhimu kabisa na unachopaswa kung’ang’ana nacho kwenye maisha yako ni malengo makubwa uliyonayo. Piga, ua garagaza, hakikisha unapambana kwa kila namna kuyafikia malengo hayo makubwa. Lakini hupaswi kung’ang’ana na njia moja katika kuyafikia malengo yako. Njia zipo nyingi, kuna ambazo ni sahihi na (more…)

2353; Unaweza Kutabiri Kwa Haya Matano…

By | June 10, 2021

2353; Unaweza Kutabiri Kwa Haya Matano… Unaweza kutabiri iwapo biashara mpya itafanikiwa au kushindwa kwa kuangalia maeneo haya matano. Moja ni wazo, je wazo ni sahihi kwa mwanzilishi wa biashara. Kila wazo ni zuri, lakini inategemea sana nani anatekeleza wazo hilo. Kama mtekelezaji hana hamasa na msukumo mkubwa kwenye wazo (more…)

2352; Wanaokukosoa Wanakusaidia…

By | June 9, 2021

2352; Wanaokukosoa Wanakusaidia… Huwa hatupendi watu watukusoe au kutukatisha tamaa kwenye yale makubwa tunayoamua kufanya. Tunaona siyo sawa kwa watu kuchagua kutushambulia wakati tunachofanya kinaweza kuwa na manufaa makubwa kwa wengi. Lakini kama ambavyo tumekuwa tunashirikishana, huwa kuna upande mzuri wa kila jambo. Hata kama kitu unakiona ni kibaya au (more…)

2351; Laini, Ngumu Na Imara…

By | June 8, 2021

2351; Laini, Ngumu Na Imara… Nassim Taleb kwenye kitabu chake cha Antifragile anaeleza mifumo yote inaweza kuwa kwenye kundi moja kati ya haya matatu. Kundi la kwanza ni laini (fragile), hii huwa rahisi kuvunjika pale inapokubwa na tatizo. Mifumo laini huwa haiwezi kuhimili matatizo na changamoto mbalimbali. Mifumo hii inaweza (more…)