Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2370; Nje Na Ndani…

By | June 27, 2021

2370; Nje Na Ndani… Kwa kila unachofanya, kuna namna mbili za kukiangalia. Kukiangalia kwa nje na kukiangalia kwa ndani. Unakiangalia kitu kwa ndani pale unapofuatilia kila kinachofanyika kwa undani kwenye kitu hicho. Hapo unajali mambo madogo madogo yanayokijenga kitu hicho. Unakiangalia kitu kwa nje pale unapoangalia picha kubwa unayotaka kufikia (more…)

2369; Mambo Yanayoathiri Maamuzi Unayofanya…

By | June 26, 2021

2369; Mambo Yanayoathiri Maamuzi Unayofanya… Sehemu kubwa ya maamuzi unayofanya kwenye maisha yako, siyo maamuzi yako binafsi. Japo unaweza kujiambia umeyafanya mwenyewe, kuna vitu vingi vinavyoathiri maamuzi yako na kukushawishi ufanye maamuzi ya aina fulani. Maamuzi yoyote unayofanya ukiwa kwenye kundi kubwa la watu, ni tofauti kabisa na yale unayofanya (more…)

2368; Uhuru Siyo Rahisi…

By | June 25, 2021

2368; Uhuru Siyo Rahisi… Watu huwa wanapenda kuzungumzia uhuru, kueleza jinsi wanavyotaka kuwa na uhuru zaidi kwenye maisha yao. Lakini ukweli ni kwamba, uhuru siyo rahisi. Kwanza siyo rahisi kuupata. Na pili siyo rahisi kuutunza. Kuupata uhuru ni vigumu kwa sababu hakuna atakayekuwa tayari kukuacha uwe huru, unahitaji kupambana kweli (more…)

2367; Ngwe nyingine….

By | June 24, 2021

2367; Ngwe nyingine…. Igawe siku yako kwenye ngwe mbalimbali. Hiyo itakusaidia pale unaposhindwa kufanya ulichopanga, badala ya kusema utakifanya kesho, jiambie utakifanya kwenye ngwe nyingine. Huwa unaanza siku kwa kuipanglia vizuri, lakini huwa yanatokea mambo na kuvuruga mipango yako. Ni rahisi kuona siku imeharibika na kujiambia utafanya tena kesho. Lakini (more…)

2366; Mtu Sahihi Wa Kusikiliza Ukosoaji Wake

By | June 23, 2021

2366; Mtu Sahihi Wa Kusikiliza Ukosoaji Wake Kwako… Kitu chochote kile utakachofanya kwenye maisha yako, kuna watu watakukosoa. Watu watachagua kuwa na maoni kuhusu wewe kwa namna wanavyotaka wao wenyewe na siyo unavyotaka wewe. Ukisema umsikilize kila mtu au kutaka kumridhisha kila mtu, hutaweza kufanya kitu chochote kikubwa kwenye maisha (more…)

2365; Ingekuwa rahisi, kila mtu angefanya…

By | June 22, 2021

2365; Ingekuwa rahisi, kila mtu angefanya… Kama inanibidi nifanye maamuzi ya haraka kwenye kitu ambacho sina taarifa za kutosha, huwa ninaangalia aina ya watu wanaokubaliana na kitu hicho au kukipigia debe. Nikiona watu wengi wanakubaliana nacho na kukisifia, naweza kuwa na uhakika kwamba kitu hicho siyo bora na kinachoweza kumfikisha (more…)

2364; Jifunze, Nufaika, Fundisha…

By | June 21, 2021

2364; Jifunze, Nufaika, Fundisha… Kusudi kuu la maisha ya viumbe wote hapa duniani ni kuzaliana. Na siyo tu kuzaliana, bali kuzaliana kwa namna ambayo ni bora kabisa. Hivi ndivyo mageuzi yamekuwa yanatokea duniani, viumbe hai wanayakabili mazingira, wanabadilika kulingana na mazingira hayo na kisha kuzaa viumbe hai walio bora zaidi (more…)

2363; Hiyo siyo kazi yao…

By | June 20, 2021

2363; Hiyo siyo kazi yao… Unataka kila mtu akubaliane na wewe ndiyo ufanye kile unachotaka, unajichelewesha bure. Unataka kila mtu akupende ndiyo uone umekamilika, utasubiri sana. Unataka watu wakuheshimu ndiyo ujione una thamani, utazidi kujipoteza. Siyo kazi ya wengine kukupenda, kukukubali na kukuheshimu, hiyo ni kazi yako mwenyewe. Kinachowatofautisha wanaofanikiwa (more…)

2362; Fursa zilizo ndani ya changamoto…

By | June 19, 2021

2362; Fursa zilizo ndani ya changamoto… Tunaposema kila changamoto ina fursa ndani yake, siyo ru kujifurahisha kwa kuwa chanya, bali ndiyo uhalisia. Hata kama linalokukabili ni kubwa na baya kiasi gani, bado kuna mazuri mengi ndani yake ambayo unaweza kuyafanyia kazi. Kama huzioni fursa zilizo kwenye changamoto, siyo kwa sababu (more…)

2361; Kama Bado Unajiuliza, Jibu Ni Hapana…

By | June 18, 2021

2361; Kama Bado Unajiuliza, Jibu Ni Hapana… Kama bado unajiuliza kama una furaha au la, jibu liko wazi, huna furaha. Wenye furaha hawapotezi muda kujiuliza kama wana furaha au la, bali wanayafurahia maisha yao. Kama bado unajiuliza kama mtu anakupenda au la, jibu unalo, hakupendi. Upendo ukiwepo huwa uko wazi (more…)