Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2350; Uhalisia hauna mbwembwe…

By | June 7, 2021

2350; Uhalisia hauna mbwembwe… Angalia kipindi cha mapishi kwenye tv au mtandaoni. Kisha nenda kapike kwa hatua zote ulizojifunza kwenye kipindi hicho. Matokeo ya mwisho hayatakuwa kama unayoona kwenye tv. Kuna mahali utakosea tu, hata kama ni kidogo kiasi gani, labda ni chumvi utazidisha au kupunja, au mafuta yasitoshe au (more…)

2349; Nini Unajaribu Kuficha…

By | June 6, 2021

2349; Nini Unajaribu Kuficha… Huwa ipo kauli kwamba ukimuona mtu anajisifia sana kwa kitu fulani, jua hicho kitu hana au anatumia sifa hizo kuficha kitu kingine ambacho hataki kionekane. Mfano mtu anayesema mimi siyo muoga hata kidogo, huwa ndiye muoga zaidi. Anatumia kauli hiyo kuficha uoga wake. Hivyo pia ndivyo (more…)

2348; Kama hawajakuomba, usijisumbue…

By | June 5, 2021

2348; Kama hawajakuomba, usijisumbue… Moja ya kitu nimewahi kuandika na wengi wakauliza kwamba hawakuelewa ni hiki; usitoe ushauri kwa mtu ambaye hajakuomba, usipokee ushauri kwa mtu ambaye hujamuomba. Unaweza kuona kama watu wanahitaji sana ushauri wako, unaona kabisa wanakwenda kukosea na kwa kuwashauri utawasaidia wasiende kuanguka. Lakini unakumbuka umewahi kufanya (more…)

2347; Muda sahihi wa kufanya kitu kikubwa…

By | June 4, 2021

2347; Muda sahihi wa kufanya kitu kikubwa… Haujawahi kuwepo, Hakuna wakati utakaosema uko tayari kufanya kitu ambacho ni kikubwa. Kila wakati utaona unahitajika kusubiri zaidi kwa sababu muda bado haujawa sahihi. Iwe ni kuanzisha biashara, kubadili kazi au kuanza mradi wowote mkubwa, utaona bado muda haujawa sahihi. Hupaswi kuruhusu hili (more…)

2346; Kabla Hujabishana…

By | June 3, 2021

2346; Kabla Hujabishana… Wengi hupenda kubishana lakini ubishani wao huwa hauna manufaa yoyote kwao. Kwani huwa wanashindwa kuwashawishi wale wanaobishana nao. Huwa nashauri sana watu kuachana na ubishani wa aina yoyote ile. Lakini kuna nyakati ubishani haukwepeki, hasa pale unapotaka kusimamia kile kilicho sahihi. Lipo sharti moja muhimu unalopaswa kutimiza (more…)

2345; Mageuzi ya teknolojia yamepiku mageuzi ya akili…

By | June 2, 2021

2345; Mageuzi ya teknolojia yamepiku mageuzi ya akili… Tunachokiona kwenye maisha ya sasa, hasa zama hizi za mitandao ya kijamii, ni mageuzi ya teknolojia kwenda kasi kuliko mageuzi ya akili. Kwa mamilioni ya miaka, binadamu tulikuwa tunaishi kwenye makundi madogo madogo ya watu wasiozidi 30. Hiyo ilikuwa rahisi kumjua kila (more…)

2342; Muujiza Unaohitaji Sana Kuutumia…

By | May 30, 2021

2342; Muujiza Unaohitaji Sana Kuutumia… Watu wamekuwa wakiulizwa kama wakipewa nafasi ya kuchagua nguvu moja ya miujiza wangechagua ipi? Wengi hujibu kuwa na nguvu za kunyanyua vitu vizito au kuweza kuruka hewani. Hayo yamekuwa siyo majibu sahihi kwa sababu hata ukiwa na nguvu hizo hazina msaada wowote kwako. Watu wakikuona (more…)

2341; Visingizio ni vingi, sababu ni moja…

By | May 29, 2021

2341; Visingizio ni vingi, sababu ni moja… Muulize mtu yeyote kwa nini hajaanza kuziishi ndoto kubwa alizonazo na majibu huwa ni yale yale kwa wato wote; Sina muda, nimebanwa sana. Sina fedha, kipato hakitoshi. Sina ujuzi, sikupata elimu sahihi. Sina ‘koneksheni’, sijazungukwa na watu sahihi. Majibu hayo yanaweza kuonekana kama (more…)