Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2340; Ukomavu Wa Kiroho…

By | May 28, 2021

2340; Ukomavu Wa Kiroho… Kama kuna kitu muhimu unachohitaji kwenye hii safari ya mafanikio basi ni ukomavu wa kiroho. Unapoianza safari hii ya mafanikio unakuwa mchanga kiroho, unakuwa na msukumo mkubwa wa kubadili maisha yako na kutaka kila anayekuzunguka abadilike mara moja. Utawalazimisha wabadilike na utawashangaa pale ambapo hawaelewi unachowashawishi. (more…)

2339; Mlango Wa Sita Wa Hisia…

By | May 27, 2021

2339; Mlango Wa Sita Wa Hisia… Tumeizoea milango mitano ya fahamu. Macho yanayoona. Masikio yanayosikia. Pua inayonusa. Ulimi unaoonja. Ngozi inayohisi. Milango hiyo mitano ndiyo tunayotumia kuwasiliana na dunia ya nje. Upo mlango wa sita wa fahamu ambao wengi hawaujui. Mlango huo siyo wa kuwasiliana na dunia ya nje, bali (more…)

2338; Maisha Kama Kombolela…

By | May 26, 2021

2338; Maisha Kama Kombolela… Kama unaukumbuka mchezo wa kombolela, una siri kubwa sana ya mafanikio kwenye maisha. Japo hatukuwa tunajua funzo lililo kwenye mchezo huo wakati tunacheza. Katika kucheza mchezo huo, kama wewr ndiye unayewatafuta wengine, kwanza lazima uwajue wote wanaoshiriki kwenye mchezo. Ukishawajua, lazima uwe na viashiria vya wapi (more…)

2336; Mtazamo Na Matendo…

By | May 24, 2021

2336; Mtazamo Na Matendo… Wengi husubiri mpaka wawe na mtazamo au hisia sahihi ndiyo wachukue hatua. Husubiri mpaka wawe na hamasa ndiyo waanze kufanya. Lakini hivyo sivyo mambo yanavyofanya kazi. Mtazamo na hisia havitangulii matendo, bali matendo ndiyo yanatangulia mtazamo. Kwa kuchukua hatua, unashawishi mtazamo na hisia zinazoendana na hatua (more…)

2335; Shamba lisilolimwa…

By | May 23, 2021

2335; Shamba lisilolimwa… Shamba lenye rutuba nzuri lakini halijalimwa, huwa halipotezi rutuba yake. Bali rutuba hubaki pale ikiwa imelala. Shamba hilo litaota magugu lakini nayo hayawezi kumaliza rutuba kubwa ya shamba. Siku akitokea mtu na kuona fursa nzuri iliyo kwenye shamba hilo na kuanza kulilima, ananufaika sana. Hivyo pia ndivyo (more…)

2334; Ushujaa Siyo Kupambana Pekee…

By | May 22, 2021

2334; Ushujaa Siyo Kupambana Pekee… Watu wengi hudhani ili wawe mashujaa lazima wapambane kwenye kila linalowakabili. Lakini ushujaa siyo kupambana pekee, wakati mwingine kuepuka mapambano ni njia sahihi na yenye manufaa kwako. Sun-Tzu aliyekuwa mwandishi wa kivita wa China ya kale na aliyeandika kitabu cha Art of War alishauri unaposhambuliwa (more…)

2332; Kupata Unachotaka…

By | May 20, 2021

2332; Kupata Unachotaka… Kutaka ni rahisi, kila mtu anataka kitu fulani kwenye maisha. Kila mtu anataka fedha zaidi, anataka maisha mazuri zaidi na anataka kufanikiwa zaidi. Lakini wachache ndiyo wanapata kile wanachotaka, huku wengi wakiwa hawana budi bali kukubali maisha ya kawaida ambayo ni ya chini kabisa. Kuna hatua muhimu (more…)

2331; Hupati Unachostahili, Bali Unachovumilia…

By | May 19, 2021

2331; Hupati Unachostahili, Bali Unachovumilia… Huo ndiyo ukweli wa maisha, wanachokupa wengine siyo kile unachkstahili, bali ambacho unakipokea, kukikubali na kukivumilia. Kujiamini kwako ndiyo kunakuwekea viwango vyako. Kama hujiamini na uko tayari kupokea viwango vya chini, hivyo ndiyo wengine watakupa. Kama unajiamini na unakubali viwango vya juu pekee ndivyo utapewa (more…)