Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (113/366); Panda mbegu za mashaka.

By | February 21, 2022

#SheriaYaLeo (113/366); Panda mbegu za mashaka. Mashaka ni silaha yenye nguvu kubwa unayoweza kuitumia kumkabili adui. Unapovuruga sifa yake kwa kufanya watu wamtilie mashaka, anabaki na jukumu kubwa la kutunza sifa yake. Atajikuta njia panda katika kulikabili hilo. Akiamua kujitetea ili kuondoa mashaka hayo, bado kuna watu hawatamwamini. Wataona katika (more…)

#SheriaYaLeo (112/366); Usiwaonee huruma maadui.

By | February 20, 2022

#SheriaYaLeo (112/366); Usiwaonee huruma maadui. Maadui zako hawakutakii mema. Kitu pekee wanachotaka kuona ni wewe ukishindwa na kuanguka kabisa. Hivyo watafanya kila mbinu kuhakikisha wanakamilisha hilo. Katika kukabiliana na maadui zako, kamwe usiwaonee huruma. Pale unapoelekea kuwashinda wanaweza kutumia mbinu hiyo ya kutaka huruma kwako. Kwa kuonyesha wamesalimu amri na (more…)

#SheriaYaLeo (111/366); Watu wanakuchukulia vile unavyojiweka.

By | February 19, 2022

#SheriaYaLeo (111/366); Watu wanakuchukulia vile unavyojiweka. Jinsi unavyojiweka ndivyo watu wanavyokuchukulia. Kama unajithamini na kujiheshimu, watu pia watakuthamini na kukuheshimu. Kama unajidharau na kutokujithamini, hivyo pia ndivyo watu watakavyokuchukulia. Ukijiweka wa kawaida na wa bei rahisi, hivyo ndivyo watu watakavyokuchukulia, kwa ukawaida kabisa. Wote wanaoheshimiwa sana na kuthaminiwa ni kwa (more…)

#SheriaYaLeo (110/366); Sifia kwa umakini.

By | February 18, 2022

#SheriaYaLeo (110/366); Sifia kwa umakini. Njia nzuri ya kukubalika na wale walio juu yako ili wakupe fursa nzuri za kupata kile unachotaka ni kuwasifia. Sisi binadamu huwa tunapenda sana kusifiwa, inatufanya tujione ni wa muhimu sana. Lakini unapaswa kuwa makini sana kwenye kusifia kwako, kwani ni rahisi mtu kuona unamsifia (more…)

#SheriaYaLeo (109/366); Watoe maadui mafichoni.

By | February 17, 2022

#SheriaYaLeo (109/366); Watoe maadui mafichoni. Unaweza kuwa na maadui ambao wamejificha. Ambao kwa nje wanaonekana kama marafiki, lakini kwa ndani wana uadui mkubwa. Wanakuwa wanasubiri wapate fursa ili wakumalize. Na kwa kuwa hujui, basi inakuwa rahisi kwako kuwapa fursa ya kutimiza lengo lao. Katika safari ya mafanikio, adui usiyemjua ni (more…)

#SheriaYaLeo (108/366); Usijiingize kwenye migogoro ya wengine.

By | February 16, 2022

#SheriaYaLeo (108/366); Usijiingize kwenye migogoro ya wengine. Mara zote epuka sana kujiingiza kwenye migogoro ya watu wengine.Hilo halina manufaa kwako kwenye malengo yako ya kupata mafanikio makubwa. Watu watajaribu kukuvuta na kukushawishi uwe upande wao, lakini epuka sana ushawishi huo. Onyesha kuwaelewa na kujali, lakini epuka sana kujiingiza kwenye migogoro (more…)

#SheriaYaLeo (107/366); Usichukue upande wowote.

By | February 15, 2022

#SheriaYaLeo (107/366); Usichukue upande wowote. Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunapenda kuwa ndani ya kundi na hivyo huwa tunakimbilia kuchukua upande fulani katika pande zinazokuwepo. Lakini hilo huishia kukunyima wewe nguvu na fursa za kufanya makubwa zaidi. Unapochukua upande mmoja na watu wakaona wanakumiliki, wanakuchukulia kawaida. Unakuwa mtumwa (more…)

#SheriaYaLeo (106/366); Tengeneza wafuasi wanaokukubali.

By | February 14, 2022

#SheriaYaLeo (106/366); Tengeneza wafuasi wanaokukubali. Kwenye safari ya mafanikio unawahitaji watu. Unahitaji kuwa kiongozi ambaye una wafuasi wanaokukubali. Wafuasi ambao wanaendana na maono makubwa uliyonayo na ambao wapo tayari kuyasimamia na kuyapambania. Uzuri ni kwamba, kiongozi hahitaji kuwashawishi wafuasi. Wafuasi tayari wapo, wanachotafuta ni kiongozi wa kuambatana naye. Hivyo unapoyaweka (more…)

#SheriaYaLeo (105/366); Ione dunia kama hekalu lililoungana.

By | February 13, 2022

#SheriaYaLeo (105/366); Ione dunia kama hekalu lililoungana. Dunia ni hatari na maadui wako kila mahali. Siyo kila mtu anakutakia mema. Na kadiri unavyopambana kufanikiwa, ndivyo unavyotengeneza maadui wengi zaidi. Hilo linaweza kukufanya ujitenge na watu na kuamua kufanya mambo yako kivyako. Utadhani kufanya hivyo kunawanyima maadui zako fursa ya kukudhuru. (more…)

#SheriaYaLeo (104/366); Bora kushambuliwa kuliko kupuuzwa.

By | February 12, 2022

#SheriaYaLeo (104/366); Bora kushambuliwa kuliko kupuuzwa. Kwenye safari yako ya mafanikio, unapaswa kujijengea sifa fulani ambazo zinakutofautisha na watu wengine. Ujiwekee viwango ambavyo kila wakati utajisukuma kujifikia. Hilo unapaswa kuliweka wazi kwa watu wote, ili wajue unasimamia upande upi na wategemee nini kwako. Kufanya hivyo kutawafanya baadhi ya watu wasifurahishwe (more…)