Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (123/366); Wakabili wanaocheza rafu.

By | March 3, 2022

#SheriaYaLeo (123/366); Wakabili wanaocheza rafu. Katika safari ya mafanikio na maisha kwa ujumla, utakutana na watu ambao wanacheza rafu. Hawa ni wale ambao wapo tayari kutumia kila namna kupata kile wanachotaka. Kwa nje watu hao hujionyesha ni wema, wastaarabu na wanaojali. Ila kwa ndani watu hao ni sumu, wenye mbinu (more…)

#SheriaYaLeo (122/366); Kila mtu yupo kwenye mchezo.

By | March 2, 2022

#SheriaYaLeo (122/366); Kila mtu yupo kwenye mchezo. Kwenye safari ya maisha, kila mmoja yupo kwenye mchezo wa madaraka. Kuna kitu kila mtu anapigania kukipata. Iwe ni fedha, mafanikio, utajiri, madaraka, umaarufu na mengine. Lakini sasa, watu wamegawanyika katika makundi matatu. Kundi la kwanza ni wanaojifanya hawapo kwenye mchezo. Hapa kuna (more…)

#SheriaYaLeo (121/366); Usionekane mkamilifu sana.

By | March 1, 2022

#SheriaYaLeo (121/366); Usionekane mkamilifu sana. Unapokuwa kwenye eneo au kundi ambalo unashirikiana na wengine ili uweze kupata mafanikio unayoyataka, kuonekana mkamilifu sana ni kikwazo kikubwa kwako. Kadiri unavyoonyesha uwezo wako mkubwa na usivyokuwa na mapungufu, ndivyo wengi wanavyojenga wivu na chuki juu yako. Unaweza kudhani kuonyesha uwezo na ukamilifu wako (more…)

#SheriaYaLeo (120/366); Usitabirike.

By | February 28, 2022

#SheriaYaLeo (120/366); Usitabirike. Watu huwa wanajaribu kusoma sababu iliyo nyuma ya kila hatua unayochukua. Ukiwa mtu wa kuchukua hatua kwa namna fulani na sababu zinazoeleweka, unatabirika kirahisi. Na watu wakishaweza kukutabiri, wanakutawala kirahisi. Sisi binadamu ni viumbe wa kitabia, huwa tunafanya yale tuliyozoea kufanya na hilo linapelekea tutabirike kirahisi. Mara (more…)

#SheriaYaLeo (119/366); Kupuuza ni kisasi bora.

By | February 27, 2022

#SheriaYaLeo (119/366); Kupuuza ni kisasi bora. Pale tunapofanya makosa, halafu tukatumia nguvu kubwa kutaka kuyaondoa au kuyaficha, huwa tunatengeneza makosa makubwa zaidi. Pale watu wanapotukosea, halafu tukapanga kulipa kisasi, tunafanya mambo kuwa makubwa zaidi. Namna bora ya kushughulika na makosa yako au kulipa kisasi, hasa kwa mambo yanayohusisha wengine ni (more…)

#SheriaYaLeo (118/366); Epuka vitu vya bure.

By | February 26, 2022

#SheriaYaLeo (118/366); Epuka vitu vya bure. Epuka sana vitu unavyopewa na wengine bure, kwa sababu huwa vina mtego wa kukunasa uwe mtumwa kwao. Watu wanaokupa au kukufanyia vitu bure bila kudai malipo yoyote, baadaye huja na matakwa makubwa kwako ambayo yanazidi hata fedha ambayo ungewalipa. Wengine kwa kukusaidia watatumia hilo (more…)

#SheriaYaLeo (117/366); Yafanye mafanikio yako yaonekane siyo ya juhudi kubwa.

By | February 25, 2022

#SheriaYaLeo (117/366); Yafanye mafanikio yako yaonekane siyo ya juhudi kubwa. Sisi binadamu huwa tunavutiwa na mafanikio ya watu wengine. Huwa tunakubali pale mtu anapoweja juhudi na kupata mafanikio makubwa. Lakini inapotokea mtu amepata mafanikio makubwa bila kuonekana akiweka juhudi kubwa, tunamkubali zaidi. Tunaona ana uwezo mkubwa na vipaji vya kipekee. (more…)

#SheriaYaLeo (116/366); Chukua Hatua Kwa Ujasiri.

By | February 24, 2022

#SheriaYaLeo (116/366); Chukua Hatua Kwa Ujasiri. Wengi wetu huwa ni waoga. Tunapenda kuepuka mivutano na migogoro na tunataka kukubalika na wote. Tunaweza kufikiria kufanya jambo la kijasiri, lakini huwa vigumu kutekeleza. Huwa tunaficha woga wetu kwa kujiambia tunajali wengine na hatutaki kuwaumiza. Lakini huo siyo ukweli, tunachohofia zaidi ni wengine (more…)

#SheriaYaLeo (115/366); Epuka muungano wa uongo.

By | February 23, 2022

#SheriaYaLeo (115/366); Epuka muungano wa uongo. Hakuna mtu anayeweza kufanikiwa peke yake kwenye maisha bila ya kuungana na wengine. Tunategemeana sana katika safari ya maisha na mafanikio. Lakini siyo kila muungano una manufaa kwako. Kuna muungano wa uongo na muungano wa kweli. Unapaswa kujua tofauti za aina hizo za muungano (more…)

#UkurasaWaLeo (114/366); Waepuke wenye kisirani.

By | February 22, 2022

#UkurasaWaLeo (114/366); Waepuke wenye kisirani. Kuna watu mbalimbali ambao wamepitia magumu na kushindwa kwenye maisha. Huwa tunasukumwa kuwaonea huruma watu hao na kuchukua hatua mbalimbali kuwasaidia. Lakini siyo wote wanaofaa kusaidia. Wapo ambao magumu na kushindwa wanakopitia wanakuwa wamejitakia wenyewe. Hao ni watu wenye kisirani na mikosi ambao kwa tabia (more…)