Misingi Miwili Muhimu Kwenye Maisha Yako

By | July 8, 2023

Hapo zamani za kale, jamii ya kiyahudi ilikuwa na misingi na sheria inayowaongoza na walikuwa amri mia sita kumi na tatu. Ilikuwa ni ngumu kwa binadamu wa kawaida kuzishika zote. Baadaye wakalalamika, ndipo mtume na nabii wao Musa alipoenda kuongea na Mungu katika mlima Sinai akawapunguzia amri kutoka amri zaidi (more…)

Njia Bora Ya Kulipa Kisasi

By | June 24, 2023

Kiasili sisi binadamu ni watu wa kulipa kisasi, pale mtu anapotutendea ndivyo sivyo huwa hatukubali tunahakikisha tunalipa kisasi. Tusipolipa kisasi katika jamii zetu ni kama vile kuonekana mjinga, ila unapolipa kisasi ndiyo unaonekana mjanja. Jamii imekuwa inakomeshana kwa njia ya visasi. Yote hii ni kwa sababu ya chuki iliyombika ndani (more…)

Barua ya VIII; Jinsi ya kuishi kifalsafa ili kufanikiwa.

By | June 23, 2023

Barua ya VIII; Jinsi ya kuishi kifalsafa ili kufanikiwa. Rafiki yangu Mstoa, Watu wengi wanaposikia kuhusu kuishi kifalsafa, huwa wanaona hiyo siyo kwa ajili yao.Huwa wanadhani kuishi kifalsafa ni kwa ajili ya wale waliosomea falsafa au waliopo kwenye dini na imani za aina mbalimbali. Lakini ukweli ni kwamba, kama unataka (more…)

Jinsi Ya Kutengeneza Mahusiano Bora Na Wale Wanaotuzunguka

By | June 10, 2023

Sisi binadamu asili yetu ni viumbe vya kijamii. Maisha yetu yamejengwa katika misingi ya mahusiano. Kila mtu yuko hapa duniani kwa sababu tayari kuna watu ambao anahusiana nao. Hatuwezi kuishi kwa kujitegemea wenyewe kwa kila kitu. Tunawahitaji wengine ili maisha yetu yaende. Ni kama vile viungo vya mwili vilivyokuwa na (more…)

Barua ya VI; Kushirikishana Maarifa.

By | June 9, 2023

Barua ya VI; Kushirikishana Maarifa. Rafiki yangu Mstoa,Tunaishi kwenye zama za maarifa na taarifa, ambapo nguvu kubwa ipo kwa wale wenye maarifa na taarifa sahihi na kufanyia kazi. Pamoja na maarifa na taarifa kupatikana kwa wingi kwenye zama hizi, bado wengi sana wameshindwa kuzipata na kufanyia kazi, kitu ambacho kimepelekea (more…)

Pima Siku Yako Kabla Ya Kulala

By | June 3, 2023

Mwanafalsafa Socrates aliwahi kunukuliwa akisema, maisha ambayo hayatathiminiwi ni maisha ambayo hayana maana kuishi. Kwa msingi huo basi, tunatakiwa kufanya tathmini zetu kujua siku zetu zimekwendaje, unapoamka asubuhi na kuanza siku yako ni kama vile umepanda na jioni ni muda wa kuvuna kile ulichopanda na kuvuna ni kupitia siku yako (more…)

Barua ya V; Kuhusu Kuishi Kwa Falsafa Na Maisha Ya Mafanikio.

By | June 2, 2023

Barua ya V; Kuhusu Kuishi Kwa Falsafa Na Maisha Ya Mafanikio. Rafiki yangu Mstoa,Moja ya vitu vinavyofanya watu wengi wasiyafurahie maisha ni kutokuishi maisha halisi kwao.Wengi wanaishi maisha ya kuiga na kuwaridhisha wengine.Wengi sana wanaishi maisha ya maigizo kwa nje, huku ndani yao wakiwa tofauti kabisa. Tumekuwa tukiona watu ambao (more…)