Tag Archives: SIRI 50 ZA MAFANIKIO

SIRI YA 40 YA MAFANIKIO; Chagua Uwanja Sahihi Wa Mapambano

By | March 5, 2015

Utafanikiwa pale utqkapojua uwanja wa mapambano ambao ni bora kwako. Uwanja ambao unaweza kushinda na kufanikiwa. Watu wengi wanacheza kwenye uwanja ambao sio bora kwao. Wanajikuta kwenye kazi wasizozipenda, mahusiano mabovu na hata miungano isiyo na faida kwao. Kama wewe ni mmoja wa watu hawa basi unahitaji kujiweka huru. Unahitaji (more…)

SIRI YA 39 YA MAFANIKIO; Zitumie Vizuri Fursa Zinazojitokeza.

By | March 4, 2015

Fursa ni kama mawimbi ya bahari. Inabidi uanze kulifuata wimbi la sivyo unalikosa. Washidi hawasiti, wanatumia kila fursa inayojitokeza. Ukisita kutumia fursa unaikosa. “There is a tide in the affairs of men, which, taken at the flood, leads on to fortune; omitted, all the voyage of their life is bound in (more…)

SIRI YA 38 YA MAFANIKIO; Upende Mchakato Wote.

By | March 3, 2015

Mafanikio hayatatokea mara moja. Kuna mchakato mrefu ambao utaupitia mpaka ufikie mafanikio. Unahitaji kufanya kazi kwa juhudi ja maarifa, kuwa mbunifu na hata kuwa mvumilivu. Kama utachkua hatua yoyote ya mchakato huu utashindwa kufikia mafanikio. Furahia kila hatua unayopitia ya kukufikisha kwenye mafanikio. Maana kila kitu ni muhimu sana kwako. (more…)

SIRI YA 37 YA MAFANIKIO; Imani Nakupa Nguvu Ya Kuchukua Hatua

By | March 2, 2015

Imani ndio hatua ya kwanza ya kufikia mafanikio. Kuamini tu kitu kinawezekana ni jambonzuri sana. Baada ya kuamini unaweza kuanza kufanya kazi na kujua utawezaje kufikia lengo lako. Kutamani tu hakuna nguvu yoyote. Ile hali ya NITAWEZAJE KUFANYA inatokana na imani. Unapoamini unawakaribisha watu wengi wakusaidie kwa sababu wanaanza kuwa (more…)

SIRI YA 36 YA MAFANIKIO; Usitengeneze Sababu.

By | March 2, 2015

Watu waliofanikiwa hawatengenezi sababu. Wangeweza kufanya hivyo ila hawataki. Sababu ni kisingizio kinachomsaidia mtu kufia uso wake pale ambapo hazalishi kile alichotarajia kuzalisha. Hakuna mtu anayetaka kusikia sababu zako. Wanataka kujua ni kipi umejipanga kufanya ili kuzalisha kile unachotarajiwa kuzalisha.    “Excuses are a waste of time. Successful people don’t (more…)

SIRI YA 35 YA MAFANIKIO; Jinsi Ya Kujijengea Kujiamini.

By | March 1, 2015

1 – Fikiria mawazo chanya tu. 2 – Yabadilishe mawazo hasi kwa mawazo chanya. 3 – Tembea haraka. Tembea kwa dhumuni. 4 – Simama katika hali ya kujiamini, kichwa kiwe juu, angalia mbele, mabega yawe nyuma na tumbo liwe ndani. 5 – Waangalie watu usoni na tabasamu. 6 – Jitambulishe (more…)

SIRI YA 34 YA MAFANIKIO; Unakuwa Kile Unachofikiria.

By | February 27, 2015

Unapata kile unachofikiri unastahili kupata kwa sababu wengine wanakuona wewe kama unavyojiona mwenyewe. Kama unafikiria wewe ni wa chini, utafanya hivyo hivyo na watu watakuchukulia wewe ni wa chini. Jinsi unavyofikiri kunaamua jinsi unavyotenda na jinsi unavyotenda kutaamua wengine wakuchukulieje. Jinsi unavyojiheshimu mwenyewe ndivyo na wengine watakavyokuheshimu.   “Change your (more…)

SIRI YA 33 YA MAFANIKIO; Kuwa Mtu Wa Vitendo.

By | February 26, 2015

1 – Lenga kile unachoweza kufanya sasa. 2 – Usisubiri mpaka mambo yote yawe sawa. Kufanya ni bora kuliko kusubiri kila kitu kiwe tayari. 3 – Mawazo tu yenyewe hayana thamani. Mawazo yanayofanyiwa kazi yana thamani kubwa sana. 4 – Kama utatenda sasa na kuzikabili hofu zako, hofu zitapotea. 5 (more…)

SIRI YA 32 YA MAFANIKIO; Zishinde Changamoto.

By | February 25, 2015

Watu waliokata tamaa na maisha yao wana kitu kimoja kinachofanana. Wote walikutana na changamoto ambayo iliwafanya waache kile wanachofanya na watakuwa tayari kukuambia ni jinsi gani hali waliyokutana nayo ilikuwa ngumu kwao. Mara zote wanaendelea kulisha hofu zao. Watu waliofanikiwa wanatenda tofauti wakati wanapokutana na changamoto. Wanaamka, wanajifunza kwa kilichowaangusha (more…)