Category Archives: KUTOKA KWA KOCHA

Hizi ni makala kwa wasomaji wote wa KISIMA CHA MAARIFA.

Karibu kwenye jamii ya tofauti ya Kisima Cha Maarifa.

By | October 27, 2023

⭐️KARIBU KWENYE JAMII YA KISIMA CHA MAARIFA. Habari Rafiki, Napenda kuchukua nafasi hii kukukaribisha kwenye jamii ya tofauti ya KISIMA CHA MAARIFA. Hii ni jamii ya watu walioamua kushika hatamu ya maisha yao na kujenga maisha ya mafanikio makubwa. Kupitia jamii hii, watu wanajifunza kwa kupata maarifa sahihi na kuchukua (more…)

2909; Vipaumbele.

By | December 18, 2022

2909; Vipaumbele. Kwako rafiki yangu mpendwa unayelalamika kwamba huna muda wa kufanya baadhi ya mambo ambayo unapaswa kuyafanya. Kiuhalisia, tatizo lako siyo muda, bali tatizo lako ni vipaumbele. Kila siku unapata masaa yako 24, yaliyojaa kabisa na wewe ndiye unayepanga unayatumiaje masaa hayo. Unapolalamika huna muda, unajua kabisa kwamba siyo (more…)

2905; Wanakudanganya.

By | December 14, 2022

2905; Wanakudanganya. Kwako rafiki yangu mpendwa unayeshangazwa na jinsi ambavyo watu wanabadilika na kudanganya. Unakuta unawaamini sana watu, lakini ghafla wanakuja kubadilika na kuwa wadanganyifu. Ni vigumu sana kwa watu kubadilika ghafla. Watu huwa wanang’ang’ana sana na tabia zao. Hivyo kama kuna mtu unaona amebadilika, kwa sehemu kubwa anakuwa hajabadilika, (more…)

2899; Njia haipotezi.

By | December 8, 2022

2899; Njia haipotezi. Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye umekuwa unajaribu njia mbalimbali lakini hupati matokeo unayotaka. Ni rahisi kujiambia tatizo lipo kwenye njia. Kwamba njia hiyo siyo sahihi na inapoteza. Lakini huo siyo ukweli, tatizo halipo kwenye njia, bali lipo kwenye namna unavyofanyia kazi njia hiyo. Kwa mfano, njia ya (more…)

2871; Maajabu, hakuna anga.

By | November 10, 2022

2871; Maajabu, hakuna anga. Kwako rafiki yangu unayedhani kuna vitu haviwezekani kwenye maisha yako. Jibu ni moja tu, hakuna chochote kisichowezekana kwenye maisha yako. Wazungu huwa wana kauli inayosema; sky is the limit. Wakimaanisha anga ndiyo ukomo. Lakini unapokuja kuangalia, anga ni nini? Anga ni mwisho wa macho yetu kuona. (more…)

#SheriaYaLeo (259/366); Achana na mazoea.

By | July 17, 2022

#SheriaYaLeo (259/366); Achana na mazoea. Majenerali bora wa kivita na wanamikakati wabunifu huwa wanafanikiwa siyo kwa sababu ya ujuzi walionao, ila kwa sababu wanaweza kuachana na mazoea na kuweka umakini wao kwenye wakati uliopo. Hivyo ndivyo ubunifu unavyochochewa na fursa kutumiwa. Maarifa, ujuzi na uzoefu huwa vina ukomo. Hakuna kiwango (more…)

MWONGO WA KUFIKIA UBILIONEA (2020 – 2030).

By | April 11, 2022

MWONGO WA KUFIKIA UBILIONEA (2020 – 2030). Muongo wa 2020 – 2030 ni muongo wa kufikia kiwango cha utajiri cha UBILIONEA kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Hiki ni kipindi ambacho kila mwanachama anapaswa kufikia uhuru wa kifedha kwenye maisha yake. Ni kupitia uhuru huo wa kifedha ndipo kila mwanachama anaweza kuwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUBADILI MAISHA YAKO, BADILI HADITHI YAKO…

By | August 31, 2021

Hadithi unayijiambia kila siku na kuiamini ndiyo inayojenga maisha yako. Kama unataka kuyabadili maisha yako, anza kwa kuibadili hadithi unayojiambia. Tengeneza hadithi mpya inayoendana na kile unachotaka, jiambie hadithi hiyo mara kwa mara na kuiamini. Jipime jinsi unavyoiishi hadithi yako na endelea kuboresha kadiri unavyokwenda. Kwa kusimama kwenye hadithi yako (more…)

#TAFAKARI YA LEO; ISHI MAISHA YAKO…

By | August 30, 2021

Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunajali sana wengine wanatuchukuliaje. Hilo lilikuwa muhimu kipindi cha nyuma, ambapo tuliishi ndani ya kundi lisilozidi watu 150 wanaojuana. Kama kikundi chako kidogo kingekukataa, huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yako. Lakini sasa tunaishi ndani ya kundi kubwa la watu na hakuna mwenye (more…)

#TAFAKARI YA LEO; RAHISI VS SAHIHI…

By | August 29, 2021

Fanya vitu rahisi na utakuwa na maisha magumu. Fanya vitu sahihi na utakuwa na maisha rahisi. Vitu rahisi kufanya siyo sahihi na vitu sahihi kufanya siyo rahisi. Kila unachofanya, jiulize kwanza unakifanya kwa sababu ni rahisi au sahihi? Utajikamata mara nyingi ukifanya vilivyo rahisi wakati vilivyo sahihi vipo mbele yako (more…)