Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

ONGEA NA KOCHA; Miminalist Entrepreneur, Tathmini Ya Robo Mwaka, Changamoto Ya Siku 100.

By | February 7, 2022

Habari mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo kuna mambo makubwa matatu. Moja ni uchambuzi wa kitabu kinachoitwa MINIMALIST ENTREPRENEUR kilichoandikwa na Sahil Lavingia. Hiki ni kitabu ambacho Sahil ameshirikisha safari yake ya kujenga biashara kwa kuzingatia yale ya msingi badala ya kuhangaika na sifa zisizo na tija. (more…)

2595; Kitakachomfaa kila mtu.

By | February 7, 2022

2595; Kitakachomfaa kila mtu. Ukitaka kuwa na kitu kitakachomfaa kila mtu, utaishia kuwa na kitu kisichomfaa yeyote. Hebu fikiria kama mvua na jua vingekuwa vinawaka na kunyesha kwa kuendana na matakwa ya watu. Nakuhakikishia kusingekuwa na majira yoyote. Maana sehemu moja pangekuwa na mvua na jua kwa wakati mmoja, maana (more…)

#SheriaYaLeo (99/366); Tawala hisia zako.

By | February 7, 2022

#SheriaYaLeo (99/366); Tawala hisia zako. Watu wenye hasira huwa wanaishia kudharauliwa na kuonekana hawana maana kwa sababu hisia zao huwa haziendani na kile kilichotokea. Hasira huwafanya watu wafanye mambo ambayo baadaye huja kuyajutia. Wanayapa mambo uzito uliopitiliza na hatimaye kujibu kwa kupitiliza. Wengi huona hasira ni sifa na kiashiria cha (more…)

2594; Rahisi kufanya.

By | February 6, 2022

2594; Rahisi kufanya. Kitu ambacho ni rahisi kufanya huwa kinafanywa na watu wengi. Kitu ambacho kinafanywa na watu wengi huwa kinakuwa na ushindani mkali. Kitu chenye ushindani mkali huwa kinakuwa na faida kidogo. Hii haimaanishi uende kufanya mapya kabisa. Bali inamaanisha chochote unachofanya, hakikisha kuna namna unafanya ambavyo wengine hawawezi (more…)

#SheriaYaLeo (98/366); Usiwe mkosoaji na mkatishaji tamaa.

By | February 6, 2022

#SheriaYaLeo (98/366); Usiwe mkosoaji na mkatishaji tamaa. Kwa wale unaoshirikiana nao, onyesha kukubali kazi zao. Usiwe mtu wa kukosoa na kuwakatisha tamaa wengine kwenye kila kitu. Kwani hilo litakujengea sifa mbaya na wengi watakuwa wanakukwepa. Hilo litaathiri ushirikiano wako na wengine na kuathiri kazi zako pia. Kadiri unavyokuwa mkosoaji na (more…)

#SheriaYaLeo (97/366); Jifanye mjinga.

By | February 5, 2022

#SheriaYaLeo (97/366); Jifanye mjinga. Kama lengo lako ni kufika ngazi za juu kabisa na kwa sasa uko ngazi za chini, kujionyesha kwamba ni mjuaji hakutakusaidia. Zaidi kutakuwa kikwazo kwako, kwani wale walio juu watakuona wewe ni hatari kwao na kutumia kila njia kukuzuia usipande juu. Lakini ukijifanya mjinga, walio juu (more…)

2592; Kula pipi na kubaki nayo.

By | February 4, 2022

2592; Kula pipi na kubaki nayo. Kutaka kula pipi na wakati huo huo kubaki nayo ndiyo kikwazo kikubwa kwa wengi kupata mafanikio makubwa. Yaani mtu anataka apate ambacho hana, lakini pia hataki kupoteza alichonacho. Hilo ni jambo lisilowezekana kwa namna yoyote ile, huwezi kupata ambacho huna bila kupoteza kile ambacho (more…)

#SheriaYaLeo (96/366); Jijenge Upya Kitabia.

By | February 4, 2022

#SheriaYaLeo (96/366); Jijenge Upya Kitabia. Tabia ulizonazo na vile watu wanavyokuchukulia siyo kilema ambacho hakiwezi kubadilishwa. Una nguvu ya kujijenga upya kitabia ili uweze kupata nguvu na madaraka ya kufika kule unakotaka kufika. Mara nyingi tabia unazokuwa nazo na vile watu wanavyokuchukulia inakuwa kikwazo kikubwa kwako kufika kule unakotaka kufika. (more…)

2591; Hakuna jipya.

By | February 3, 2022

2591; Hakuna jipya. Sisi binadamu wakati mwingine huwa tunashangaza sana. Tunapenda kufanya vitu kwa mazoea, lakini inapokuja kwenye kufanikiwa, tunapenda vitu vipya vipya. Kufanya kitu kile kile kwa kurudia rudia na kwa muda mrefu huwa inawachosha wengi. Wanakimbilia kutafuta vitu vipya vya kufanya, ambavyo vinawasisikua kwa upya wake, lakini haviwi (more…)