Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (95/366); Jua wakati wa kutoa na kupokea sifa.

By | February 3, 2022

#SheriaYaLeo (95/366); Jua wakati wa kutoa na kupokea sifa. Huwa tunapenda kupewa sifa kwa kile ambacho tumewezesha kifanyike au kikamilike. Ni kawaida kwetu binadamu kupenda kusifiwa, kwani huwa tunaona tumethaminiwa zaidi. Kama ambavyo tunajisikia vizuri tukisifiwa, ndivyo pia wengine wanajisikia vizuri wanaposifiwa. Na hapa ndipo unapaswa kujua wakati gani wa (more…)

2590; Kujipendekeza.

By | February 2, 2022

2590; Kujipendekeza. Sisi binadamu ni viumbe wa kihisia, huwa tunafanya maamuzi kwa hisia na kisha kuyahalalisha kwa mantiki. Chochote unachotaka kwenye maisha yako kinatoka kwa watu wengine. Unawategemea sana watu wengine, hakuna unachoweza peke yako. Ukiwafanya watu wajisikie vizuri, watakuwa tayari kukupa unachotaka. Ukiwafanya wajisikie vibaya hawatakuwa tayari kukupa unachotaka. (more…)

#SheriaYaLeo (94/366); Jua  nani mwenye mamlaka.

By | February 2, 2022

#SheriaYaLeo (94/366); Jua nani mwenye mamlaka. Katika eneo lolote lile, iwe ni taasisi, biashara au jamii, kuna watu wachache au mmoja ambaye ndiye mwenye mamlaka makubwa. Mara nyingi mtu au watu hao siyo wale wanaoonekana kuwa viongozi, wanaweza kuwa watu wengine kabisa, ambao wanafanya mambo yao nyuma ya pazia. Unapotaka (more…)

2589; Tarehe ya mwisho.

By | February 1, 2022

2589; Tarehe ya mwisho. Elon Musk, bilionea namba moja duniani kwa sasa, amekuwa akijisukuma sana katika kuyaendesha makampuni yake, kitu ambacho kimeyafanya yawe na ufanisi mkubwa. Katika kujisukuma huko amekuwa akijiwekea lengo na tarehe ya mwisho ya kulifikia. Wakati mmoja alipata tenda ya serikali ya kufunga umeme wa jua na (more…)

#SheriaYaLeo (93/366); Mfanye bosi wako ajione yuko juu zaidi.

By | February 1, 2022

#SheriaYaLeo (93/366); Mfanye bosi wako ajione yuko juu zaidi. Katika kujenga ubobezi na kufanya makubwa, kuna watu ambao wako juu yako, ambao wana nguvu fulani kwenye hatua unazotaka kupiga. Kitendo tu cha wewe kufanya makubwa, kinawaweka wao kwenye hatari, kwa kuwafanya wajione hawana umuhimu kwako.Hilo litaibua hisia mbaya kwao na (more…)

Ongea Na Kocha; Mjadala Wa Kitabu Billionaire In Training.

By | January 31, 2022

Habari Mwanamafanikio? Kwenye KISIMA CHA MAARIFA, tupo kwenye muongo (2020 – 2030) wa kufanya makubwa. Katika muongo huu kila mmoja wetu anapambana kufikia uhuru wa kifedha, ambapo ni kuweza kuwa na njia za kuingiza kipato kisichotegemea uwepo wa moja kwa moja (passive income) pamoja na kuwa na uwekezaji mkubwa unaokua (more…)

#SheriaYaLeo (92/366); Usimzidi Bosi Wako.

By | January 31, 2022

#SheriaYaLeo (92/366); Usimzidi Bosi Wako. Sisi binadamu huwa tuna tabia ya wivu na kutokujiamini. Pale mtu mwingine anapofanya vizuri kuliko sisi tunaona anapata fursa nyingi na nzuri zaidi. Unapojihusisha na watu wengine, hupaswi kujali sana kuhusu hilo, wewe pambana kuwa bora na kuzalisha matokeo makubwa. Lakini inapokuja kwa bosi wako, (more…)

#SheriaYaLeo (91/366); Sikiliza Sauti Yako Ya Ndani.

By | January 30, 2022

#SheriaYaLeo (91/366); Sikiliza Sauti Yako Ya Ndani. Ubobezi hautokani na uwezo ambao mtu amezaliwa nao au bahati. Bali ni matokeo ya mtu kusikiliza sauti yake ya ndani na kufuata vile inavyomsukuma. Kila mtu ana sauti hiyo ya ndani, ambayo inajua nini anataka kwenye maisha yake. Ni sauti inayotokana na uwezo (more…)