Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (90/366); Ona Zaidi Ya Kinachoonekana.

By | January 29, 2022

#SheriaYaLeo (90/366); Ona Zaidi Ya Kinachoonekana. Watu wa kawaida ambao hawajafikia ubobezi, huwa wanaona yale tu yanayoonekana. Hiyo ni kwa sababu wanakuwa hawajaweka umakini mkubwa kwenye kitu na kukielewa kwa undani. Lakini wale waliofikia ubobezi wa hali ya juu kwenye kile wanachofanya, huwa wanaona zaidi ya kinachoonekana. Kwa sababu wanakuwa (more…)

#SheriaYaLeo (89/366); Unganisha akili na machale.

By | January 28, 2022

#SheriaYaLeo (89/366); Unganisha akili na machale. Kadiri unavyozama kwenye kukifanya kitu, unapata uelewa wa ndani kabisa na kuweza kuona vitu ambavyo wengine hawaoni kirahisi. Unakuwa na machale yanayokuwezesha kujua vitu ambavyo huwezi kuvielezea. Unapata hisia fulani pale kitu kinapokuwa sahihi au siyo sahihi. Unakuwa na uwezo wa kuiona dunia na (more…)

2584; Nyama zipo chini.

By | January 27, 2022

2584; Nyama zipo chini. Maisha ni kama kunywa mtori, Haijalishi utautikisa vipi, Nyama utazikuta chini. Ni lazima uunywe mtori wenyewe kwanza ndiyo uweze kuzifikia nyama. Mtori ndiyo maisha yetu ya kila siku na nyama ndiyo kile tunachokitaka. Watu wengi huhangaika na njia za mkato za kupata wanachotaka. Lakini huishia kupoteza (more…)

#SheriaYaLeo (88/366); Nenda zaidi ya akili.

By | January 27, 2022

#SheriaYaLeo (88/366); Nenda zaidi ya akili. Wakati wa kuanza kufanya kitu, mtu anatumia zaidi akili kufikiri na kufanya. Hilo linapelekea mtu kufanya kwa namna ambayo wengine pia wanafanya. Ni baada ya kufikia ubobezi wa hali ya juu ndiyo mtu anakuwa amezama kweli kwenye kile anachofanya, kiasi kwamba ufanyaji unakuwa sehemu (more…)

2583; Wateja.

By | January 26, 2022

2583; Wateja. Kuna wateja wanajua thamani ya kile unachouza au kufanya, ambao wapo tayari kulipia mara moja na kupata thamani hiyo. Wateja hawa siyo wasumbufu na wananufaika kweli na kile unachowauzia. Kuna wateja ambao wanaona unatoza sana na hivyo kutaka uwapunguzie. Watalalamika sana, wakionekana wanakihitaji kweli kitu ila kinachowakwamisha ni (more…)

#SheriaYaLeo (87/366); Nguvu ya kuzama kwenye ufanyaji.

By | January 26, 2022

#SheriaYaLeo (87/366); Nguvu ya kuzama kwenye ufanyaji. Ugumu mkubwa uliopo kwenye safari ya ubobezi ni muda mrefu unaohitajika kwenye kufanya kile ulichochagua kufanya. Huku pia ukiwa unashawishiwa na tamaa mbalimbali za vitu vinavyoweza kuwa na manufaa ya muda mfupi ila siyo ya muda mrefu. Unalazimika ujitoe kweli kweli na utoe (more…)

2582; Nafasi ya kujua ujinga wako.

By | January 25, 2022

2582; Nafasi ya kujua ujinga wako. Bradley Sugars kwenye kitabu cha Billionaire in Training anashirikisha nukuu inayosema; watu wengi huwa wanafikiri mabosi wao ni wajinga, mpaka pale wanapokuja kuwa mabosi wao wenyewe. Ni rahisi sana unapoona mtu mwenye nafasi fulani anakosea kwa maamuzi anayokuwa anafanya. Lakini unapokuja kuwa kwenye nafasi (more…)

#SheriaYaLeo (86/366); Angalia kinachokosekana.

By | January 25, 2022

#SheriaYaLeo (86/366); Angalia kinachokosekana. Ni kawaida yetu binadamu kuangalia kile kilichopo na kisha kufikiri kwa namna hiyo. Kwa kutumia kilichopo ndiyo tunafanya maamuzi mbalimbali. Lakini kuna taarifa nyingi kwenye yale yanayokosekana. Kuna vitu ambavyo vilitakiwa viwepo ila havipo. Kwa kuanza kuvofikiria vitu hivyo, tunaweza kuja na ubunifu wa kipekee. Kwenye (more…)