Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Ongea Na Kocha; Billionaire In Training, Helanane Ilomo.

By | January 24, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo kuna mambo makubwa mawili. Jambo la kwanza ni uchambuzi wa kitabu cha BILLIONAIRE IN TRAINING. Hiki ni kitabu muhimu sana kwenye safari yetu ya kuelekea kwenye uhuru wa kifedha. Na ndiyo kitabu kitakachokuwa mwongozo mkuu kwetu. Kwenye uchambuzi huo tutajifunza (more…)

#SheriaYaLeo (85/366); Jenga uwezo wa kupokea usiyokubaliana nayo.

By | January 24, 2022

#SheriaYaLeo (85/366); Jenga uwezo wa kupokea usiyokubaliana nayo. Ni kawaida kwetu binadamu tukishajenga mazoea fulani ndiyo huwa tunaendelea nayo. Tunaona hiyo ndiyo namna sahihi ya kufanya kitu husika. Pale tunapokutana na namna ya tofauti na tulivyozoea, huwa tunaikosoa na kuipinga kwamba siyo sahihi. Tunatetea namna yetu kwa kuona ndiyo sahihi (more…)

#SheriaYaLeo (84/366); Akili kama msuli.

By | January 23, 2022

#SheriaYaLeo (84/366); Akili kama msuli. Akili zetu huwa zipo kama msuli. Msuli unapotumika unakua na kuimarika. Na msuli usipotumika unasinyaa na kuwa dhaifu. Akili ikitumika inakua na kuimarika na isipotumika inasinyaa na kuwa dhaifu. Kinachofanya akili isinyae isipotumika ni mambo mawili. Moja ni kupenda mazoea. Tukishakuwa na fikra au njia (more…)

2579; Mpaka uelewe.

By | January 22, 2022

2579; Mpaka uelewe. Upo usemi wa Kiswahili kwamba asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Unaweza kupata maana mbalimbali kwenye usemi huo, lakini kuna maana moja nimeona ina nguvu kubwa sana. Iko hivi, mtoto anapokosea, mzazi humwadhibu. Kama mtoto ataendelea kukosea, mzazi hawezi kuendelea kumwadhibu, atafika mahali na kumwonea huruma. Na (more…)

#SheriaYaLeo (83/366); Sikiliza Kuvurugwa Kwako.

By | January 22, 2022

#SheriaYaLeo (83/366); Sikiliza Kuvurugwa Kwako. Kwa chochote unachofanya, huwa unaanza na hamasa na msukumo mkubwa, ambao unakuwezesha kufanya kitu hicho kwa muda bila kuchoka. Lakini baada ya muda unajikuta kwenye hali ya kuvurugwa, ambapo unakutana na mkwamo mkubwa na ugumu mkubwa wa kuendelea. Huo ndiyo wakati wenye fursa nzuri, kwa (more…)

2578; Huhitaji kutumia nguvy nyingi.

By | January 21, 2022

2578; Huhitaji kutumia nguvy nyingi. Kupumua ni kitu ambacho huwa hakihitaji nguvu kubwa. Unapojikuta ukitumia nguvu kubwa kupumua, hapo unajua wazi kwamba kuna shida kwenye mfumo wa upumuaji. Kadhalika kwenye kula na mengine yanayoendelea kwenye mwili. Huwa yanakwenda yenyewe kwa urahisi kabisa bila kuhitaji nguvu zako kubwa. Hivyo pia ndivyo (more…)

#SheriaYaLeo (82/366); Fanya Tahajudi.

By | January 21, 2022

#SheriaYaLeo (82/366); Fanya Tahajudi. Safari ya ubobezi na kuelekea kwenye mafanikio makubwa inahitaji ukomavu, utulivu na umakini wa muda mrefu. Wengi huanza safari hiyo wakiwa na hamasa ya hali ya juu sana. Lakini kadiri muda unavyokwenda hamasa hiyo inapoa na wanajikuta wakirudi kwenye mazoea. Mawazo yao yanahama hama na hayawezi (more…)