Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2553; Mubashara na marudio.

By | December 27, 2021

2553; Mubashara na marudio. Ukiangalia mchezo wowote ule mubashara, kwa wakati ambapo unaendelea, unakuwa hujui nini hasa kitatokea muda wowote ujao. Hivyo unaangalia kwa shauku kubwa, ukijua chochote kinaweza kutokea. Ukiangalia mchezo huo huo kwa marudio, unakuwa huna shauku kubwa, kwa sababu tayari unajua nini kitakwenda kutokea. Kama ni magoli (more…)

#SheriaYaLeo (57/366); Toka nje ya mazoea yako.

By | December 27, 2021

#SheriaYaLeo (57/366); Toka nje ya mazoea yako. Kadiri unavyoendelea kujifunza kwa kufanya, utajikuta umejijengea aina fulani ya mazoea ambayo ndiyo unaridhika nayo. Mazoea hayo yanakuwa yametokana na wale ambao unakuwa umejifunza kutoka kwao, maana nao pia wanakuwa wamefikia kilele fulani na kufanya zaidi kwa mazoea. Huwezi kufikia ubobezi wa hali (more…)

#SheriaYaLeo (56/366); Endelea kutanua mipaka yako.

By | December 26, 2021

#SheriaYaLeo (56/366); Endelea kutanua mipaka yako. Unapoianza safari ya kujifunza ili kuelekea kwenye ubobezi wa hali ya juu, unakutana na ukweli ambao hukuwa unaujua. Ukweli huo ni safari hiyo ni ngumu na vikwazo ni vingi. Kikwazo kikubwa kabisa kitakuwa ni kupata watu sahihi kujifunza kutoka kwao ili kuweza kufikia ubobezi. (more…)

2551; Jua sheria kabla hujazivunja.

By | December 25, 2021

2551; Jua sheria kabla hujazivunja. Siyo sheria za nchi, bali zile taratibu mbalimbali za kijamii ambazo zipo na zimezoeleka na kila mtu. Kuzifuata taratibu hizo ni kuzuru, kunakufanya ueleweke na ukubalike na wengine kwenye jamii. Lakini huwezi kufikia ubobezi wa hali ya juu na kupata mafanikio makubwa kwa kuendelea kufuata (more…)

#SheriaYaLeo (55/366); Mpite Mwalimu Wako.

By | December 25, 2021

#SheriaYaLeo (55/366); Mpite Mwalimu Wako. Unapoanza kujifunza kwenye eneo unalotaka kubobea, unapaswa kufuata maelekezo unayopewa na mwalimu wako, ambaye tayari ameshabobea kwenye eneo hilo. Ukishaijua misingi yote muhimu ya eneo hilo ulilochagua, unapaswa kujifunza zaidi ya kile ambacho mwalimu wako anakufundisha. Unapaswa kuyageuza mafunzo yake yaendane na upekee na utofauti (more…)

2550; Mtu rahisi kumdanganya.

By | December 24, 2021

2550; Mtu rahisi kumdanganya. Mtu rahisi kabisa kumdanganya kwenye maisha yako ni wewe mwenyewe. Unaya ni hutajua wakati unajidanganya, ni mpaka baadaye sana na mambo yakiwa yameshaharibika ndiyo unagundua ulikuwa unajidanganya. Kwanza, kama unataka sana kitu kiwe kweli au kiwe sahihi kwako, hayo ndiyo utakayoona. Kutakuwa na viashiria kama kitu (more…)

#SheriaYaLeo (54/366); Usitosheke na maarifa.

By | December 24, 2021

#SheriaYaLeo (54/366); Usitosheke na maarifa. Ili kufikia ubobezi wa hali ya juu na kudumu kwenye ubobezi huo, hupaswi kuridhika na maarifa. Hupaswi kufika mahali na kuona tayari umeshajifunza vya kutosha na kujua kila kitu. Kila wakati unapaswa kuwa na njaa na kiu ya kuendelea kujifunza kwa kina zaidi. Jifunze kwa (more…)

2549; Taarifa ya upande mmoja.

By | December 23, 2021

2549; Taarifa ya upande mmoja. Pale ambapo kuna jambo linalohusisha pande mbili, kamwe usikubali taarifa ya upande mmoja pekee. Hata kama inashawishi na kuaminika kiasi gani, taarifa yoyote ile haijakamilika kama haina pande zote zinazohusika. Sisi binadamu huwa ni rahisi kuona makosa ya wengine lakini ni wagumu sana kuona makosa (more…)

#SheriaYaLeo (53/366); Fyonza Nguvu Yenye Kusudi.

By | December 23, 2021

#SheriaYaLeo (53/366); Fyonza Nguvu Yenye Kusudi. Katika safari yako ya kufikia ubobezi wa hali ya juu na mafanikio makubwa, unapaswa kuzungukwa na watu wenye nguvu ya kusudi na wanaopambana kufikia makubwa pia. Watu unaojihusisha nao, wanavyonza nguvu yako na wewe unafyonza nguvu yao pia. Kama utazungukwa na watu waliokata tamaa (more…)