Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2548; Kutulia siyo tu kwenye kile unachofanya, bali na kwenye maisha pia.

By | December 22, 2021

2548; Kutulia siyo tu kwenye kile unachofanya, bali na kwenye maisha pia. Tumezungumza mara nyingi hapa umuhimu wa kuchagua fursa moja na kutulia nayo kwa muda mrefu ndiyo uweze kupata matunda mazuri. Tunapaswa kuacha kuhangaika na kila fursa mpya, maana huko ni kupoteza nguvu kusiko na tija. Wapo wanaofanya hivyo, (more…)

#SheriaYaLeo (52/366); Tengeneza Kuhitajika.

By | December 22, 2021

#SheriaYaLeo (52/366); Tengeneza Kuhitajika. Wakati unajijengea ubobezi wako, tengeneza kuhitajika kwako na watu wengine. Wafanye wale unaowalenga kwenye kile unachofanya wakutegemee wewe zaidi. Hakikisha bila uwepo wako kuna mambo muhimu wanakosa au vitu vyao muhimu vinakwama. Hili ni muhimu sana kwa sababu kadiri unavyobobea ndivyo unavyozidi kutoza gharama kubwa kwenye (more…)

2547; Safari ya mafanikio haitofautiani na maisha.

By | December 21, 2021

2547; Safari ya mafanikio haitofautiani na maisha. Kwenye maisha, huwa tunajua jinsi vitu vilivyo na kuenda navyo kwa namna vinavyoenda. Kama umeoa au kuolewa, umekaa na mwenza wako kwa muda mrefu na mtaendelea kukaa kwa muda mrefu. Hukai naye ukijiambia kuna kitu fulani unataka kukipata kisha kutokuendelea naye tena. Mwenzako (more…)

#SheriaYaLeo (51/366); Elewa jinsi ubongo unavyofanya kazi.

By | December 21, 2021

#SheriaYaLeo (51/366); Elewa jinsi ubongo unavyofanya kazi. Huwa tunadhani tunaweza kuruka hatua, kuepuka mchakato, kutumia kanuni rahisi au vipaji vyetu kufikia ubobezi kwa muda mfupi bila kuweka kazi. Ujio wa teknolojia umetufanya tuone kuna namna tunaweza kuukwepa mchakato mzima wa ubobezi. Kwa sababu teknolojia zimerahisisha mengi, tunadhani zinaweza pia kurahisisha (more…)

Ongea Na Kocha; Andika, Dedicated, Selemani Mbwambo.

By | December 20, 2021

Habari Mwanamafanikio? Karibu usikilize kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambacho kina mambo makubwa na muhimu kama ifuatavyo; Kwenye somo la juma utajifunza umuhimu wa Kuandika vitu ili uweze kufikiri vizuri na kuweza kuvikamilisha. Unapofikiria tu vitu huvipi msisitizo mkubwa kama ukiviandika chini. Hivyo unapaswa kujijengea utamaduni wa kuyaandika malengo yako (more…)

2546; Kila kitu kina umuhimu.

By | December 20, 2021

2546; Kila kitu kina umuhimu. Jambo moja kuhusu maisha ni kwamba kila kitu kina umuhimu. Lakini kwa bahati mbaya sana, huwa hatuoni umuhimu wa kitu mpaka pale tunapokuwa tumeshakipoteza. Unapokuwa na kitu unakizoea na kuona ubaya au madhaifu yake kuliko manufaa yake. Ni mpaka pale unapokuwa umekipoteza ndiyo unaona jinsi (more…)

#SheriaYaLeo (50/366); Chagua muda.

By | December 20, 2021

#SheriaYaLeo (50/366); Chagua muda. Chochote unachochagua kubobea, unahitaji muda wa kutosha kuweka juhudi ili kuweza kupata matokeo makubwa. Kama una majukumu mengine mengi yanayochukua muda wako mwingi na kukuchosha, itakuwa vigumu kwako kifikia ubobezi unaotaka. Kile unachotaka kubobea kinapaswa kuwa ndiyo kipaumbele kikubwa kwako, hivyo kitengee muda wa kutosha. Yarahisishe (more…)

2545; Kuwa fursa inayotafutwa.

By | December 19, 2021

2545; Kuwa fursa inayotafutwa. Kwenye maisha kuna watu wa aina mbili. Aina ya kwanza ni wale ambao kila wakati wanatafuta fursa mpya. Kila wakati kuna kitu kipya wanafanyia kazi. Hawakai kwenye kitu kimoja kwa muda mrefu, kwa sababu wanaposikia kuna kingine kipya na kizuri zaidi, wanaacha walichokuwa wanafanya na kwenda (more…)

#SheriaYaLeo (49/366); Aina mbili za kushindwa.

By | December 19, 2021

#SheriaYaLeo (49/366); Aina mbili za kushindwa. Kuna aina mbili za kushindwa. Aina ya kwanza ni kushindwa kabla hata ya kuanza. Hapa unahofia kufanya kwa sababu unaona utashindwa au kwa sababu unaona bado muda haujawa sahihi, hujawa na maandalizi ya kutosha. Kwenye aina hii ya kushindwa hakuna chochote unachojifunza. Woga wako (more…)

2544; Hujuma.

By | December 18, 2021

2544; Hujuma. Kama unaweka juhudi kubwa ili uweze kufanikiwa, lakini juhudi hizo hazileti matunda mazuri na kila wakati unakutana na vikwazo na magumu mbalimbali, jua kuna hujuma zinaendelea. Kuna nguvu kubwa inayopinga kila juhudi unazoweka na ndiyo maana hupati matokeo mazuri. Hujuma zinaweza kuwa zinatoka ndani yako mwenyewe au kutoka (more…)