Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (48/366); Ukweli Unaouma.

By | December 18, 2021

#SheriaYaLeo (48/366); Ukweli Unaouma. Hakuna njia ya mkato ya kufika kwenye ubobezi. Hakuna namna unaweza kukwepa mafunzo na ufanyaji wa kina wa kile unachotaka kubobea. Hayo yanahitaji muda ambao hauwezi kuharakishwa kwa namna yoyote ile. Kwa wastani, inachukua angalau miaka 10 ya kujifunza na kufanya kwa kina ndiyo mtu aweze (more…)

2543; Zima Washa.

By | December 17, 2021

2543; Zima Washa. Kifaa chochote cha kielektroniki kikikusumbua, kabla hujapeleka kwa fundi, huwa unashauriwa kufanya kitu kimoja, kukizima kisha kukiwasha (restart). Iwe ni siku, redio, tv, kompyuta na vinginevyo, zoezi la kuzima na kuwasha huwa linatatua sehemu kubwa ya matatizo. Mara nyingi vifaa hivyo hukaa sawa baada ya kuzima na (more…)

#SheriaYaLeo (47/366); Jifunze na kufanya kwa

By | December 17, 2021

#SheriaYaLeo (47/366); Jifunze na kufanya kwa kina. Watu wengi huwa wanajifunza na kufanya vitu kwa juu juu. Huwa wanataka yale maeneo ya kufurahisha na kusisimua. Lakini hivyo sivyo ubobezi unavyojengwa. Ubobezi unajengwa kwa kujifunza na kufanya kwa kina. Kujifunza na kufanya kwa kurudia rudia yale ya kawaida na yanayochosha. Hayo (more…)

2542; Tiba Muda.

By | December 16, 2021

2542; Tiba Muda. Kuna mambo unaweza kuwa unalazimisha yawe kwa namna fulani lakini inashindikana. Unaweka juhudi za kila aina ili kupata matokeo unayotaka lakini inashindikana. Unaamua kuachana nayo kwa muda na baadaye unakuja kugundua yamejitatua yenyewe na matokeo yamepatikana bila hata ya kuhangaika sana. Muda ni tiba ya mambo mengi (more…)

#SheriaYaLeo (46/366); Umakini kwenye kujifunza

By | December 16, 2021

#SheriaYaLeo (46/366); Umakini kwenye kujifunza haujawahi kushindwa. Japo inaweza kuonekana inachukua muda mrefu kwenye kujifunza mpaka kufikia ubobezi wa hali ya juu, umakini, juhudi na muda unaowekwa kwenye kujifunza haupotei. Tafiti zilizofanywa kwenye eneo la ubobezi zinaonyesha kwamba mtu anahitaji kujifunza na kufanya kwa umakini mkubwa kwa angalau masaa elfu (more…)

2541; Unakopotezea nguvu zako.

By | December 15, 2021

2541; Unakopotezea nguvu zako. Waangalie watoto wadogo, huwa hawawezi kutulia sehemu moja kwa muda mrefu. Waweke watoto mahali na baada ya muda mfupi utawakuta wakirukaruka na kukimbizana. Hiyo ni kwa sababu ndani yao kuna nguvu kubwa inayochemka na inayotafuta mahali pa kutokea. Hiyo ndiyo inayowasukuma wafanye yale wanayofanya. Nguvu hiyo (more…)

#SheriaYaLeo (45/366); Ufuate Ukinzani.

By | December 15, 2021

#SheriaYaLeo (45/366); Ufuate Ukinzani. Sisi binadamu huwa tuna tabia ya kukimbia mambo ambayo ni magumu na yenye maumivu. Tunapenda kufanya yale ambayo ni rahisi kwetu na yasiyoonyesha udhaifu wetu. Kwa njia hii, tunashindwa kujijengea ubobezi, kwa sababu tunakuwa tumeweka nguvu na umakini wetu kwenye maeneo machache na ambayo ni rahisi (more…)

2540; Umakini uliogawanyika.

By | December 14, 2021

2540; Umakini uliogawanyika. Akili zetu zina uwezo mkubwa sana. Lakini uwezo huo unaweza kufikiwa kama umakini wa akili utawekwa kwenye kitu kimoja kwa wakati. Pale umakini wote unapowekwa kwenye kitu kimoja, uwezo wa akili unawezesha kifanyike kwa viwango vya juu sana. Lakini pale umakini unapogawanyika, nguvu na uwezo wa akili (more…)

#SheriaYaLeo (44/366); Jinsi ya kujifunza haraka na kwa kina.

By | December 14, 2021

#SheriaYaLeo (44/366); Jinsi ya kujifunza haraka na kwa kina. Unapoingia kwenye mazingira yoyote mapya, wajibu wako ni kujifunza mambo mengi iwezekanavyo. Ili kufanikisha hilo, unapaswa kurudi kwenye hali ya utoto, kwa kuona kwamba watu wengine wanajua kuliko wewe na unategemea kujifunza kwao ili na wewe uweze kubobea. Unapaswa kuweka pembeni (more…)

2539; Kujiridhisha kwa kujidanganya.

By | December 13, 2021

2539; Kujiridhisha kwa kujidanganya. Mambo mengi yanayotukwamisha na kutuangusha huwa hayatokei kwa kushtukiza. Bali yanakuwa na visababishi vinavyojulikana na ambavyo vipo wazi kabisa. Lakini mtu unachagua kutokuona visababishi hivyo, kwa sababu ukweli unaumiza. Hivyo unachagua kujiridhisha kwa kujifanganya. Ni pale unapojiambia utafanya kitu kesho au baadaye. Ukweli ni huna muda (more…)