Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

SheriaYaLeo (43/366); Rudia rudia kufanya.

By | December 13, 2021

SheriaYaLeo (43/366); Rudia rudia kufanya. Mfumo wa elimu unafundisha vitu kwa nadharia, kwa mwanafunzi kusoma na kufanya mitihani. Katika kipindi chote cha elimu mwanafunzi anajifunza kwa kupewa maarifa na taarifa tu. Haishangazi kwa nini mwanafunzi anapohitimu masomo na kwenda kwenye dunia halisi anajikuta hakuna anachoweza kufanya. Anaweza kuwa na vyeti (more…)

2538; Nafasi ya kukosea.

By | December 12, 2021

2538; Nafasi ya kukosea. Ukikuta daraja limeandikwa tani 10, yaani mwisho wa uzito wa kupita hapo ni tani 10, haimaanishi ukipitisha tani 11 litavunjika. Hata kwa dawa nyingi, unapoambiwa dozi ni vidonge viwili, haimaanishi ukinywa vitatu utakufa hapo hapo. Mifumo mingi imewekewa nafasi kubwa ya kukosea bila ya kuleta madhara (more…)

#SheriaYaLeo (42/366); Jinsi ya kujifunza kwa kasi.

By | December 12, 2021

#SheriaYaLeo (42/366); Jinsi ya kujifunza kwa kasi. Kwa chochote unachojifunza, unajifunza kwa kasi zaidi kupitia kufanya kuliko kupitia kusoma au kusikiliza maelekezo. Mwanzo wa kufanya huwa ni mgumu, lakini kadiri unavyoendelea kufanya ndivyo inavyokuwa rahisi. Unajifunza kwa kasi na ubora zaidi kwa kufanya kile unachojifunza. Hata kama ni lugha mpya (more…)

2537; Fursa mchepuko.

By | December 11, 2021

2537; Fursa mchepuko. Nimewahi kuandika kwamba hofu ni lile unachokiona pale unapoondoa umakini wako kwenye ndoto zako kubwa. Leo nakwenda kuongezea hilo kwamba unaziona fursa mchepuko pale unapoondoa umakini wako kwenye ndoto zako kubwa. Fursa mchepuko ni zile fursa zinazoonekana kuwa nzuri na zenye manufaa sana kwako, lakini ili uzifanyie (more…)

#SheriaYaLeo (41/366); Jifunze Kutoka Kwenye Kila

By | December 11, 2021

#SheriaYaLeo (41/366); Jifunze Kutoka Kwenye Kila Kitu. Kila jukumu unalopewa au kuwa nalo linakupa fursa ya kujifunza kuhusu kile unachofanya, watu na dunia kwa ujumla. Hakuna jukumu ambalo halina fursa hiyo ya kujifunza na hakuna taarifa ndani ya kitu ambazo ni ndogo na zisizo na uzito. Kila kitu unachosikia au (more…)

2536; Makubaliano ya kuridhishana.

By | December 10, 2021

2536; Makubaliano ya kuridhishana. Kwenye maisha na shughuli mbalimbali huwa tunakutana na hali za kutokukubaliana kwenye mambo mbalimbali. Kutokana na uelewa, imani na mazoea tofauti ambayo watu wanayo, kwenye jambo moja watu wanaweza kuwa na mtazamo au maoni tofauti. Kila mtu ataona upande wake ndiyo sahihi zaidi na kuamini upande (more…)

#SheriaYaLeo (40/366); Raha itokane na unachofanya

By | December 10, 2021

#SheriaYaLeo (40/366); Raha itokane na unachofanya. Kadiri unavyoendelea kujifunza na kujijengea ujuzi wako, unaendelea kubadilika na kuwa bora zaidi. Unagundua uwezo mkubwa ulio ndani yako ambao ulikuwa umelala, ambao unaamshwa kadiri unavyokwenda. Unakua kiakili na kihisia na maana ya raha kwako inabadilika. Vitu vinavyotoa raha ya haraka kama ulevi mitandao (more…)

#SheriaYaLeo (39/366); Menta Sahihi Kwako.

By | December 9, 2021

#SheriaYaLeo (39/366); Menta Sahihi Kwako. Kupata menta sahihi kwako, angalia mtu ambaye kazi zake zinakuvutia sana, zinakupa hamasa na msukumo wa kuwa kama wao. Angalia mtu ambaye mtindo wake wa maisha na kazi anazofanya unakupa shauku kubwa, unajiona unaweza kufanya kwa namna kama yake. Pia angalia ni mtu wa aina (more…)

2534; Kazi haikwepeki, inaweza kuhamishwa.

By | December 8, 2021

2534; Kazi haikwepeki, inaweza kuhamishwa. Kazi haiwezi kukwepeka, ila inaweza kuhamishwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine. Mwandishi mmoja amewahi kusema kama umeweza kusoma kitu kwa urahisi, jua mwandishi ameweka kazi kubwa kwenye kuandika. Na kama kitu ni kigumu kusoma, jua mwandishi hajaweka kazi. Maana yake ni rahisi, (more…)