Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2505; Siyo Pata Potea.

By | November 9, 2021

2505; Siyo Pata Potea. Kikwazo kikubwa cha watu kwenye mafanikio ni mtazamo wanaokuwa nao. Ndiyo maana unaweza kukuta watu wawili, wanafanya kazi au biashara ya aina moja, mmoja anafanikiwa sana na mwingine anashindwa. Kinachowatofautisha watu hao ni mtazamo. Kuna mitazamo mingi ambayo imekuwa kikwazo kwa wengi kufanikiwa. Lakini mmoja mkubwa (more…)

#SheriaYaLeo (9/366); Pata hamasa kutoka kwa mashujaa wako.

By | November 9, 2021

#SheriaYaLeo (9/366); Pata hamasa kutoka kwa mashujaa wako. Kuna watu ambao ukiwaona wanavyofanya kazi zao unapata hamasa kubwa sana ndani yako. Unavutiwa sana na aina ya maisha wanayoishi na yale wanayofanya. Watu hao wanakupa hamasa na msukumo wa kufanya makubwa kama wao wanavyofanya. Hao ndiyo mashujaa wako, ambao ukiwatumia vizuri (more…)

ONGEA NA KOCHA; Nguvu Ya Fikra, The Prophet, Sebastian Kalugulu.

By | November 8, 2021

Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo unakwenda kujifunza mambo matatu makubwa. Moja ni Nguvu ya fikra kwenye safari ya mafanikio. Hapa utajifunza jinsi fikra zako zilivyo na nguvu ya kuumba na jinsi ya kujenga fikra sahihi na kuzilinda. Mbili ni uchambizi wa kitabu cha The Prophet ambapo utajifunza (more…)

2504; Jenga Mahusiano Zaidi.

By | November 8, 2021

2504; Jenga Mahusiano Zaidi. Huwa kuna kauli kwamba haijalishi unajua nini, bali unamjua nani. Sehemu kubwa ya mafanikio yako inatokana na wale unaowajua kuliko yale unayoyajua. Hii ni kusema kwamba mahusiano yako na watu sahihi ni muhimu sana kwenye mafanikio yako. Kwa sababu kama unavyojua, kila unachokihitaji tayari kipo kwa (more…)

#SheriaYaLeo (8/366); Kubali Na Ishi Utofauti

By | November 8, 2021

#SheriaYaLeo (8/366); Kubali Na Ishi Utofauti Wako. Kila mtu ana utofauti fulani ambao upo ndani yake. Kuna namna ya ufanyaji wa mambo ambayo ni ya tofauti kabisa. Na pia kuna vitu vya tofauti kabisa vinavyomvutia mtu tofauti na wengine. Kwa walio wengi huwa wanapuuza utofauti wao na kuchagua kufanya yale (more…)

2503; Kukusanya Na Kutawanya.

By | November 7, 2021

2503; Kukusanya Na Kutawanya. Mwanga wa jua ukitawanywa unatoa tu mwangaza wa kawaida. Lakini mwanga huo huo ukikusanywa eneo moja, unatoa moto mkali wenye kuweza kuunguza chochote. Nguvu na umakini wako ukivitawanya unaishia kupata matokeo ya kawaida. Lakini ukikusanya vitu hivyo viwili kwenye maeneo machache, unazalisha matokeo makubwa sana. Kama (more…)

#SheriaYaLeo (7/365); Pesa Na Mafanikio.

By | November 7, 2021

#SheriaYaLeo (7/365); Pesa Na Mafanikio. Kwa walio wengi, hitaji la kupata pesa na mafanikio linaweza kuwa motisha mkubwa kwao kuwasukuma kufanya makubwa. Kwa watu wa aina hii huona hakuna haja ya kuhangaika kulijua kusudi la maisha yao. Huona huko ni kupoteza muda na hivyo huachana na hilo na kuhangaika na (more…)

2502; Hiyo Pesa Itafute Hapo Ulipo Kwanza.

By | November 6, 2021

2502; Hiyo Pesa Itafute Hapo Ulipo Kwanza. Fursa mpya zimekuwa haziishi na zinashawishi kweli kweli. Maana ni vigumu sana kuikataa pesa wakati una uhitaji mkubwa wa fedha. Hivyo zinapokuja fursa mpya, ambazo tunakua kabisa kwamba haziendani na kile tunachofanya, tukishaona kuna fedha tunaweza kupata, basi tunakimbilia kuifanya. Mwisho wake kinachotokea (more…)

#SheriaYaLeo (6/366); Mabadiliko Ni Sheria.

By | November 6, 2021

#SheriaYaLeo (6/366); Mabadiliko Ni Sheria. Mabadiliko ni sheria ya maisha. Hakuna kitu chochote kinachobaki kilivyo, kila kitu kinabadilika. Katika kukabiliana na mabadiliko kwenye kazi na biashara zako, endana na mabadiliko badala ya kuyapinga. Tambua kwamba hujafungiwa kwenye kufanya kitu cha aina fulani pekee. Uaminifu wako siyo kwenye kazi, biashara au (more…)

2501; Kama nafsi inakataa, isikilize.

By | November 5, 2021

2501; Kama nafsi inakataa, isikilize. Kuna wakati unaweza kuwa na fursa fulani mbele yako, fursa ambayo inaonekana ni nzuri kabisa, lakini nafsi yako inakataa kabisa kuikubali fursa hiyo. Mara nyingi hili hutokes pale unapohitaji kujihusisha na watu fulani. Labda ni kwenye kazi au biashara. Kwa nje wanaonekana ni watu wazuri (more…)